Kweli nimeamini elimu tuliorithi kutoka kwa wakoloni ni chanzo cha umasikini mkubwa sana Tanzania na Afrika kwa ujumla wake

Kam ulidanganya wataujuaje umri halisi?
Upo vizuri kweli ? Unaona sawa mtu adanganye umri azekee kazini na afie kazini.
Wenzio wanastaafu miaka 60 wewe 68. Unaona sawa.
Isitoshe wenzio wana anza maisha mapema na kuoa na kupata watoto mapema wewe unachelewa kupata kuoa na kupata watoto.
Unaona sawa haya yoye yakutokee ?
Wewe unaweza kuwa sio muajiliwa, usingesapoti hoja ya kudanganya umri kisa ulichelewa shule.
NI HASARA KUBWA SANA KUCHELEWA KUANZA SHULE.
 
Watu wanadanganya pande zote, wala hakuna jipya hapo, Nimeona wengi sana tu. Binafsi nilimshuhudia mzee mmoja, alikuja ofisini kueleza ukweli lakini mkurugenzi alimkatalia kustaafu, akamwambia tukikubali maelezo yako, utashitakiwa kuidanganya serikali, utafungwa, utaamriwa kurudisha mishahara yote uliyowahi kuchukua.
Alichomsaidia alimwambia we njoo nitakubadirishia majukumu. Lakini Kisheria na file lako umri wako wa kustaafua bado.
 
Hujakosea!
 

Attachments

  • Mohamed Mawinda Tai - THAT_S WHY AFRICANS ARE POOR.....Education System. - 2104139433063289(SD).mp4
    4.6 MB
Mbona kuna utaratibu mpya unaanza nadhan mwakani watoto wataishia darasa la 6

Waliopata kujua zaidi wataelezea
 
Wazo lako kwa wastani ni jema tu.Lakini,umejiuliza hivyo vichwa vya kufanya matarajio hayo kwa muda mfupi viko wapi?Ni vya kuchagua na ni nadra.Ila,kwa kuanzia si mbaya.
 
Soma vizuri comment . Usome comment zote mbili utaelewa. Kiufupi nipk kinyume na wanaodanganya umri ili wabaki milele serikalini.
Kwa sababu hukusoma nilipoanzia ni kwamba wengi wanaopunguza umri ni wale waliochelewa kuanza shule au kazi.
Hivyo basi msiwacheleweshe watoto shule wasije danganya umri kisha wakazeekea kazini ma kufia kazini.
Juu niliandika comment kuwa nimeanzisha watoto wangu shuke std 1 miaka 4.5 na 5 ili kuwaepusha na suala la kuanza kazi na umri mkubwa.
 
That's not true.
Alafu hapo unaongelea muda au ubovu wa education system? Sababu tatizo la wasomi kuwa useless sio muda bali mfumo wa elimu. Hata ukimaliza chuo na miaka 7, kama elimu yako haina msaada kwako, wewe bado ni useless na utabaki masikini.
Nafahamu watu wengi kutoka nje ya nchi kama Marekani. Wote wanalalamika education system yao ni mbovu na haiwasaidii. Hili tatizo sio Tanzania tu. Bali dunia nzima.

Except kwetu linaweza kuwa kubwa zaidi sababu ya umasikini.
 
naamini hujanielewa! ninavyo sema kujifunzia karakana, hospitali n.k namaanisha mafunzo kwa vitendo.. hebu jifunze kutafakari kwa kina.....

pia kwa maelezo yako, ina maana kwamba kila anacho fanya mzungu ni sahihi na kinapaswa kuigwa, si ndivyo? kisa baadhi ya nchi za wazungu wanamaliza shule wakiwa na miaka 25 kwako ni sawa si ndivyo? na kama hujui kwa taarifa yako kwa kozi ya sheria kuna sehemu wameweza kidogo... ukienda pale law school muda mwingi wanatumia kwenye moot court na bado haitoshi wakimaliza ile miezi sita bado wanaenda tena intership miezi 6.....

hizo kozi za lugha ustawi na maendeleo ya jamii n.k kuna utaratibu wake tu wa kujifunza kwa vitendo... na vitendo ni njia bora zaidi ya kujifunza.....

nadhani mkuu wewe umesoma ili unibishie wala hukufakari kwanza ndo unijibu,,, na hiyo yote ni kwa sababu wanadamu wengi wa sasa ni wabishi sana......
 
Lengo kuu la elimu sio kusoma na kwenda kuajiriwa lengo kuu ni kupata maarifa hata kama una miaka 40 ukiwa na maarifa utakuwa na impact kubwa sana kuliko mtu aliyeenda kuajiliwa
 
ukitaka kuharibu kizaz cha nchi fulani dont go to war, vuruga education yao then wait.

Hii elimu ya mkoloni miaka ya uhuru ilikuwa quality lakini after 70s tulitakuwa tuchange kabisa hii elimu, bahati mbaya walioko ni wagumu kubadili hilo, why inawetengeneza kizazi cha wajinga ambacho ni rahisi kuwatawala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…