Kweli ukoloni mamboleo umetushika......lo!

only83

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2010
Posts
5,343
Reaction score
2,527
Nimekuwa nikijiuliza kwanini watanzania wengi wanapenda kushabikia na kushangilia timu za ulaya..utakuta mtu mweusi kutoka kule Musoma amevaa jezi imeandikwa Chacharito,Rooney nk...katika moja ya policy ya kuingiza ukoloni mamboleo ni kuwafanya watu weusi wadharau mambo yao..ni watu wachache sana wanaovaa jezi za timu kama Simba,Yanga,Azam FC,Mtibwa nk.....Tuacheni utumwa huo jamani turudini nyumbani tuone namna ya kukuza soka letu.....
 


Broda naona umekosea jukwaa na kuja kututukana wapenzi wa footy ... ila tumekusikia kwa heri, next time ukirudi Njoo mada yenye kichwa na miguu.. katika soccer hakuna siasa, hakuna udini hakuna ukoloni mambo leo.. NUKTA
 

Kama umekosa la kuandika afadhali ukae kimya!
 
sidhani kama ni vibaya kuvaa jezi hizo za timu ya kizungu. Sio kuwa hatutaki kuzipenda timu zetu za nyumbani, lakini kuna raha gani kuitukuza timu ambayo kila siku inakupa homa kwa migogoro isiyoisha? Ndani ya mwaka mmoja timu inakuwa haijafanya chochote cha maana, zaidi ya uongozi kuvurugana na kutuhumiana mambo mbalimbali. hata hizo jezi za wachezaji wa kibongo zipo kwani? maana wenzetu kila mchezaji ana namba yake, hata timu ikiwa na wachezaji 40, huku timu ina wachezaji 30, jezi 18, jezi za kubadilishana.

tunachohitaji ni kujitambua kuwa sisi watanzania na nchi nyingine za kiafrika hatuitendei haki sekta ya michezo. hatuna mipango madhubuti ya kuiimarisha, ambapo ingekuwa ni moja ya sehemu ya kutengenezea ajira kwa vijana mbalimbal
i
 

Mapenzi ya soka hayana mipaka. Ndio maana jamaa wenye hela zao wametoka Umangani, Russia, US etc kwenda kununua timu kule UK.
Kuhusu kushabikia timu za ulaya na kusahau timu zetu, mmmhhnn...kama zingekuwa zina maendeleo yoyote nina imani watu wangezisupport, lakini timu hizo Sima/Yanga hazina mbele wala nyuma. Kila kukicha migogoro isioisha.
Hii ni era ya globalization bana!
 
Umeshawahi kuwauliza kwa nini wanavaa hizo jezi za nje.Halafu kwani umeshajicheki juu mpaka chini umevaa vitu vya wapi THINK BIG.Ati ukoloni ukisikia mjomba ako anatakiwa kwenda juu utaomba asirudi tena.Tafuta mada.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…