Kwenu mnatumia dawa gani za asili kutibu magonjwa

Magna Carta

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2014
Posts
4,347
Reaction score
6,652
Hasa hasa napenda kuulizia dawa moja nasikia iko huko Bukoba inatibu magonjwa mengi sana wenyeji wa huko mtaniambia, Lakini kikwetu dawa matata bingwa wa yote ni mwarobaini

Karibuni
 
Kwe
Hasa hasa napenda kuulizia dawa moja nasikia iko huko Bukoba inatibu magonjwa mengi sana wenyeji wa huko mtaniambia, Lakini kikwetu dawa matata bingwa wa yote ni mwarobaini

Karibuni
KweTu mwarobaini tunautumia kurogea. Kama unataka kumroga mtu ili maisha yake yawe machungu basi unatumia mwarobaini.
 
Mwarobaini ukichemshwa ni sumu... itaua ini lako. Mwarobaini usichemshwe

Nashukuru kwa kujibu uzi wangu maana nilishasahau, je ni dawa au sio, vipi kuhusu kuchemsha kwa nini inakua vibaya.
Asante
 
Kwe
KweTu mwarobaini tunautumia kurogea. Kama unataka kumroga mtu ili maisha yake yawe machungu basi unatumia mwarobaini.

Napenda kusikia hili kwa Mshana pia, nyie hamnywi na kwa nini?
 
Habari mkuu. Mimi natumia majani ya msongwa kutibu taifodi ni mwaka 3 sasa sijatumia cipro, UTI majani ya rozela(juisi) na asali, magonjwa mengine yote natumia habbat soda ya unga, maji safi ya kunywa kutibu maumivu ya kichwa na tumbo, limao kutibu kiungulia kikali (heart burn)
 

Mkuu kiungulia nacho ni tatizo ninaomba wataalamu watusaidie kinasababishwa na nini, mimi nilichokariri ni viazi vitamu tu? Ila naona mwarobaini ni dawa nzuri, hata mlonge nasikia ila sijajaribu!
 
Nashukuru kwa kujibu uzi wangu maana nilishasahau, je ni dawa au sio, vipi kuhusu kuchemsha kwa nini inakua vibaya.
Asante
Mwarobaini ni dawa inayotibu magonjwa mengi, ila inapochemshwa inakuwa na sumu nyingi ambazo ni hatari sana kwa afya ya figo na ini lako, ndio maana unashauriwa uutwange, kisha uuloweke kwenye maji kwa masaa 12
 
Mwarobaini ni dawa inayotibu magonjwa mengi, ila inapochemshwa inakuwa na sumu nyingi ambazo ni hatari sana kwa afya ya figo na ini lako, ndio maana unashauriwa uutwange, kisha uuloweke kwenye maji kwa masaa 12

Nashukuru kwa mbinu hii
 
Mkuu kiungulia nacho ni tatizo ninaomba wataalamu watusaidie kinasababishwa na nini, mimi nilichokariri ni viazi vitamu tu? Ila naona mwarobaini ni dawa nzuri, hata mlonge nasikia ila sijajaribu!
Sijui chanzo cha kiungulia ni nini, Ila Dawa ya kiungulia ni MAGADI(Sijui kitaalamu yanaitwaje), Ila lamba kiasi kidogo sana, muda huo huo unapona.
 
Sijui chanzo cha kiungulia ni nini, Ila Dawa ya kiungulia ni MAGADI(Sijui kitaalamu yanaitwaje), Ila lamba kiasi kidogo sana, muda huo huo unapona.

Sikuwahi kulijua hili, ni likua najua Magadi yanatumika hata kwenye kikohozi pamoja na asali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…