Kwenu wanawake: Lini mtatuelewa wanaume!

Kwenu wanawake: Lini mtatuelewa wanaume!

Mr DIY

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2016
Posts
1,188
Reaction score
2,553
Kuna mwenzenu huku (wife) amenitumia msj zenu za ku forward sijui katoa wapi akisisitiza niisome (nita share hapo chini), nikakumbuka wanawake wengi huwa wanasahau kwamba wanaume hatujaumbwa kusikiliza maneno mengi ili kupata point moja, niliishia kusoma heading na pale mwisho nikagundua alie andika ni jinsia ya Ke akitaka kutushauri kwa maneno mengi wanaume, wanawake mjifunze huwezi mbadili mwenzio kwa maneno mengi!

Ujumbe wenyewe sasa👇

Tafiti zinaonyesha kwamba kwa wastani mwanamke kwa siku anaongea maneno walau elfu ishirini mpaka elfu ishirini na nne (20000 -24000) huku mwanaume akiongea walau maneno elfu sita mpaka elfu saba kwa siku(.6000-7000)

Hii ina maana kwamba mwanaume huongea mara tatu zaidi ya Mwanaume. Hivyo basi na wanawake wanapoongea hawaongei peke yao kama vichaa bali huwa wanahitaji mtu wa kuwasikiliza hayo maneno yao.

Ikitokea mme haupo ukirudi kaa kitako mke ayaongee maneno yote 20000 zidisha siku ambazo haukuwepo
Wanaume wengi hufanya makosa ya kujifanya wako busy na hivyo kutokukaa kusikiliza maneno ya wake zao.

Mara nyingi utagundua kwamba wanawake au watu wa jinsia ya kike sio kwamba wanavutiwa na watu wenye fedha sana bali wanavutiwa na mtu anayeweza kukaa na kuwasikiliza hata kama wanayoyaongea ni pointless.Mara nyingi mwanamke aliyeolewa aweza kujikuta ameingia kwenye mahusiano na mtu ambaye ana uwezo wa kukaa na kumsikliza hata kama hampi kitu chochote..

Mme pamoja na ratiba yako ngumu ya kutafuta pesa za kujenga na kulipa ada za watoto usiache kutenga muda wa kumsikiliza mkeo.
Maana mtu mwingine akijua kuwa mkeo hasikilizwi akampa Attention yake aweza jikuta amemuiba kihisia

Mwanaume uliyeoa ni lini mara ya mwisho ulipata muda wa kukaa kitako kumsikiliza mkeo?
Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.(1 Petro 3:7)
Wanaume nimekuja kuwakumbusha tu.
Wakati mwingine hatuhitaji mafedha mengi wala magari we only just need your attention, kusikilizwa tu.
Wasaalamu
Pst Winnie Kilemo
0769 141105
 
Yaani unakuta baba hagusi kitu maana akitaka kunywa juice anaambiwa hiyo usiguse ni ya mtoto,mayai ni ya mtoto.Yeye anapikiwa ugali maharage na majani ya kunde chukuchuku.Chai anapewa chai ya rangi na kiporo.Sikia nikwambie hao watoto wanakua,wataenda shule baadaye watawaacha kila mtu ataenda kuanzisha maisha yake ,hawataishi na ninyi milele.Sasa siku wakiwaacha ninyi wawili tu kwenye uzee wenu ndo utajua umuhimu wa kumjali mwenzako.
Ogopa hii isikukute,
 
Sisi wanawake tumeumbwa kuongea sana, muwe mnatusikiliza tusiongee wenyewe.

Ni matumaini yangu haijazidi sentesi moja.
Mimi simpendi mwanamke anaeongea sana

Nampenda mwanamke mwenye ulimi mzito
Nikiona mwanamke anaongea km cherehani basi kazi ni moja nasuuza parachichi langu kisha napita kushoto sipendi makelele
 
Sisi wanawake tumeumbwa kuongea sana, muwe mnatusikiliza tusiongee wenyewe.

Ni matumaini yangu haijazidi sentesi moja.
Hivi kidogo tutakusikilizeni... Maneno machache yaliyojaa point!
 
Back
Top Bottom