Kwenye awamu ya 5 viongozi wote Wastaafu na waliokuwa madarakani mawasiliano yao yalidukuliwa na kuanikwa hadharani. Faragha zao zilipuuzwa

Kwa tafsiri Ujiko ni sifa , huwezi kutafuta sifa kwa ID fake
 
Kama isingekuwa kuna vinyongo na visasi ndani ya Jamiiforums, nyuzi hii isingepita hata kidogo.

Magulification will go on
Nani hapa Jf ambaye hafahamu haya ninayoyaandika ? unasema kinyongo , unadhani hicho kinyongo kimetokana na nini ? je unaweza kuthibitisha hicho kinyongo ?
 
Nani hapa Jf ambaye hafahamu haya ninayoyaandika ? unasema kinyongo , unadhani hicho kinyongo kimetokana na nini ? je unaweza kuthibitisha hicho kinyongo ?
Kama JF wote tunafahamu haya unayoyandika, sasa unarudia kuyaandika Ili iweje? Kumkumbusha nani ilhali wote tunayafahamu kwa mujibu wako?. Ujinga mtupu.
 
Uzuri Watanzania sio wasahaulifu.

Mahakama zilimtia hatiani Cyprian Musiba kwa defamation.

Watanzania watakumbuka Cyprian Musiba alihusishwa na Uvujaji wa "Vidukuo" hivi hivi tu kwamba mengi yalikuwa ni fabrication. Na hivyo kufanya taarifa hizi za Erythrocyte kuwa ni Fabrication tu.

Tukirudi hapa kwa Erythrocyte na JamiiForums , Familia au Estate ya J.P.Magufuli inaweza kuwafungulia hawa kesi za Defamation kwa kuchukua screenshots za Uzi kama huu na kutumia kama ushahidi wa- na kuzitaka/kuitaka mahakama kuwalazimisha Jamiiforums watoe taarifa za huyu Erythrocyte au za Kusitisha kashfa hizi.

Yaani cease and desist au watoe taarifa zitakazo tumika kupelekwa kwa Erythrocyte kufikisha mahakamani.

Somewhere somehow these shenannigans have to stop.

Na hao wastaafu wapeleke madai yao mahakamani. Na wathibitishe haya madai na tuhuma za Erythrocyte kuwa ni kweli yaliwatokea. Bila hivo Nchi hii itatumbukia kwenye Siasa za Visasi na Vinyongo. Bila hivyo haya ni Maoungo tu.
 
Vitisho !
 
Picha za hao uliowabandika hapo juu ndio wamekutuma?

Wewe ni Chadema lakini unashadadia watu wanaoendelea kuwatesa kisa eti mmpewa ruksa kuandamana !!!

Kwa taarifa yako simu zako tano na vishikwambi vyako viwili vinafuatiliwa kwa kasi sana ni wakati tu utaingia kwenye kumi na nane zao.

Unafikiri hao vijana wanane wanaodaiwa kukamatwa Dar imetokea pasipo kudukua kwanza?

Umekuwa mlamba uchafu kutoka kwa watu wachafu kupiliza na hata hadhi ya uhabarishaji wako hauna maana tena kazi yako kutwa kucha kumsimanga JPM uklifikiri unajipa alama za kukubalika kumbe ndio unatumbukia shimoni.

Huo ni ujinga uliokomaa na utakugharimu sana na wenzio wanaokutuma serikali zinabadilika kwa hiyo usijipe moyo na uropokaji usiofaa unaoendelea nao hivi sasa.
 
Ukimaliza utuletee na kisa cha mwenyekiti kuvunjika mguu kwa kimada!
 
Una kasirika nini sasa?
Fitina Umeandika wewe.
Raisi Samia Suluhu Hassan alikuwemo kwenye hiyo Awamu ya Tano au hakuwemo?
Raisi Samia Suluhu Hassan ni Mwanachama wa CCM ama sio?
Maandiko yako are just slanderous na ina wa target watu mahususi.
Kutumia Nukuu ya Jakaya Kikwete, ni kutaka kulazimisha Uwingi-Basi usisahau kumweka Rais Samia. Vinginevyo Utumiaji wa nukuu hiyo ni kutaka kulazimisha 'your defamation pursuit' kuwa una uhalali.
 
Picha ya hao wanne uloweka picha zao na kikundi Chao Cha Wachache ndio Hasa wanalitesa Taifa hili Hadi sasa.

Ninakushauri simama upande wa wananchi Si kundi dogo la Mafisadi.
 
Mimi nitaendelea Kusema.

Familia ya John Pombe Magufuli ifike mahakamani haraka sana.

Hii kesi watashinda kwa kishindo.
 
Hata wakati wa chadema wakiwa moto enzi za katibu mkuu Slaa walikuwa wakidukua sana viongozi wa Serikali na kilipua mabomu kwenye mikutano yao ndio maana chadema kipindi hicho ilipendwa sana kipindi hicho maana waliongea kwa nyaraka zilizodukuliwa au kivujishwa,hata Sasahivi Serikali ya Samia inafanya hivyo ndio maana unaona pangua pangua na kuamisha,kusifu na kuabudu nikwingi, kufukunyua mawasiliano ya Watu sio kwa Magufuli duniani kote wanafanya hivyo,sema hakina Kinana walikuwa washamba hauwezi kumteteta Rais wa nchi hivyo,ingelikuwa Rwanda kwa Kageme Sasahivi waliisha sahaulika.
 
Mbona hakuna rejea za cheusi mangala kuzungumza hayo unayomzushia?
 
Hapa wala husemi ukweli Bali unasema ujinga
 
Mbona hakuna rejea za cheusi mangala kuzungumza hayo unayomzushia?
Hakuzungumza , yeye alileta nyuzi za Udukuzi hapa JF , Ingia kwenye ID yake nyuzi zote zimejaa tele na wala hazijafutwa
 
Naomba nikukatalie kauli yako uliyoanza nayo ya kuwa huu ni mwezi wa mungu.Ni hayo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…