Kwenye mkataba nimemwandika kama mrithi Ila yeye kamwandika baba yake

Kwenye mkataba nimemwandika kama mrithi Ila yeye kamwandika baba yake

sepema

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2019
Posts
591
Reaction score
1,001
Salaam kwenu,

Niko kwenye ndoa mwaka wa 8 saivi na tumejaaliwa kuwa na watoto wawili. Mimi na mwenzangu tumeajiriwa Kwenye taasisi moja ya umma japo kwenye vituo tofauti.

Mwezi huu kukatokea agizo la kuhuisha taarifa za wafanyakazi ili ziwe za kisasa na halisia kuliko mwanzo.
Zoezi hili lilihusisha urekebishaji wa baadhi ya taarifa zilizopo kwenye mikataba ya wafanyakazi ambayo waliijaza walipoajiriwa.

Kwa kuwa wakati tunaanza kazi hatukuwa na familia, sehemu ya warithi kwenye mikataba tulikuwa tumeweka wazazi na ndugu zetu. Sasa kutokana na kuwa na familia tulichopanga mimi na mwenzangu ni kwamba kwenye maboresho tujiandike sisi wenyewe Kama warithi wa kwanza pamoja na watoto wetu. Mimi kwenye mkataba nikamweka mke na watoto wangu Kama tulivyokubaliana.

Nimekuja kushtuka baada ya kuona mkataba wa mke wangu ambapo yeye kamwandika baba yake mzazi pamoja na watoto. Mimi hakuniandika kabisa.

Mkataba wake nimefanikiwa kuuona baada ya kuongea na mhusika aliyekuwa anaikusanya Kisha kuipeleka sehemu husika. Hadi sahivi mke hajui kwamba nimegundua kitendo hicho.

Najiuliza, hili tukio mke kalifanya kwa makusudi au bahati mbaya.

Au kitaalam sio lazima mwanamke kumwandika mumewe Kama mrithi?

Je, niendelee kujifanya sijui au nimuulize nijue nia yake ya kufanya hivyo?

Wasalaam!
 
Tuishi nao kwa akili! Chunguza zaidi yaweza tokea wewe ukaandika mkopo ukaulenga kuboresha familia yenu (wewe mke na watoto) chunguza mkopo wake atauelekeza kusaidia / kujengea wazazi wake! Hawa ndio wanawake zetu, TUISHI NAO KWA AKILI
 
Tuishi nao kwa akili,!!! Chunguza zaidi yaweza tokea wewe ukaandika mkopo ukaulenga kuboresha familia yenu ( wewe mke na watoto) chunguza mkopo wake atauelekeza kusaidia / kujengea wazazi wake! Hawa ndio wanawake zetu, TUISHI NAO KWA AKILI
Acha amjengee kwani Ni mume ndio kamsomesha acheni ujinga. Sasa mume anajenga kwako kwa wazazi wake Kama fadhila ila mke akijenga inakuwa nongwa.

Mimi nadhani mke yuko sahihi kwa kumjali Baba yake Kwanza zilioni shida kabisa.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Acha amjengee kwani Ni mume ndio kamsomesha acheni ujinga Sasa mume anajenga kwako kwa wazaz wake Kama fadhila ila mke akijenga inakuwa nongwa

Mm nadhni mke Yuko sahih kwa kumjali Bab ake Kwanza zilioni shida kbsa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Lakini kwa makubaliano sio kwa kificho, na hayo ndio huleta migogoro mingi kwenye familia mpaka kuzalisha michepuko
 
Hili nalo la kuomba ushauri kama mlishakubaliana mbadilishe yeye bado akagoma. Trust me hiyo will ya kufanya ivoo imebarikiwa na wakwe.

Huyo hakufai kuligundua hilo mpaka uje upigike haswa mfano kupoteza kazi maana hamna mwili mmoja tena hapo.

Anyway Piga chini au ishi nae kimkakati
 
Hakuna Utumwa mbaya kama ule wa kujiona upo Free.... NDOA..

Mkuu achana na kufuatilia urithi wa Mkeo, wewe zingatia urithi wako unahitaji kina nani wafaidike nao..

Ila huyo MKE jambo nnaloweza kukuhakikishia ni kuwa yupo na wewe kwa ajili ya maslahi yake. Siku ukiyumba kiuchumi hakika utajua hujui, ISHI NAE KWA AKILI NYINGI SANA.... uchunguzi ufanye kwa kuangalia ushiriki wake katika mambo ya msingi ya kifamilia....

Be a Man, Stay Taliban.
 
Salaam kwenu

Niko kwenye ndoa mwaka wa8 saivi na tumejaaliwa kuwa na watoto wawili.
Mimi namwenzangu tumeajiriwa Kwenye taasisi moja ya umma japo kwenye vituo tofauti.
Sasa cha ajabu nini?? Ni wapi uliona mwanamke anamweka mume kama mrithi my friend. Mimi ni mtumishi sijawahi kuona.. Hata uwaulize au kuwashauri huwezi kubadilisha hiyo mitazamo yao..

So why ukae uumize kichwa kwa vitu none sense. Unajua wazi kwa nini huwa wanafanya hivyo. Kwa hiyo usiumize kichwa. Au una uhakika atatangulia kufa yeye? If not why bother?

Wote ndio Hali hiyo hiyo na maisha ya naendelea tena kwa furaha na Amani.

Kwani akitangulia wewe utashindwa kutunza watoto mpaka uwe concern na nini aliandika?

Baada ya kifo wanaotesekaga ni wajane (Wanawake) na sio wagane.

Mwanamke anaamini yeye akifa utaoa mke mwingine ambaye ndiye atakayekuja kula vyote alivyochuma au mlivyochuma pamoja na atawanyanyasa watoto wake aliowaacha.... Na wanaona mifano hai kila siku na ni kweli.

Sasa utatumia mbinu ipi kumwaminisha kuwa kwako haitakuwa hivyo?

Kumbuka mwanaume ndio mwenye maamuzi ya kuoa au kutooa.. Tofauti na mwanamke akifiwa kuolewa ni ngumu sana Maana Hana maamuzi juu ya mwanaume. Labda achukue viserengeti. Ingawa wapo wachache wanaoolewa tena.

So relax chapa kazi, lea familia achana na hivyo vitu vidogo kama you're machured enough kwenye ndoa.

Jenga future bora ya familia yako hata usipo kuwepo una uhakika hakuna kikaragosi kutoka kwenye ndugu zako atakae ingilia future na rasilimali ulizoacha vinginevyo usipoteze muda na akili.

Wanaume ndio tunaopaswa kujenga Mifumo ya kuaminika na wenzi wetu vinginevyo mtaishia kuharibu ndoa.

Njia ya kwanza ni kudhihirisha kwa vitendo kuwa huna na huhitaji chochote chake(isipokuwa responsibilities za kawaida kwenye family, mahitaji, maendeleo, Ada etc.) lakini Mali no no.. Jinsi ambayo utakuwa huonyeshi interest kwenye maeneo hayo ndivyo atakavyo kuamini na kukabidhi mwenyewe Mali na mirathi.

Kadiri unavyoonesha interest kwenye vitu hivyo ikiwemo mirathi uliyo Sema ndivyo atazidi kuikimbiza mbali nawe Maana ni Ishara ya kutoaminika.

Be Gentle man my friend utaishi kwa raha, Amani na furaha na mkeo.
 
Salaam kwenu

Niko kwenye ndoa mwaka wa8 saivi na tumejaaliwa kuwa na watoto wawili. Mimi namwenzangu tumeajiriwa Kwenye taasisi moja ya umma japo kwenye vituo tofauti.

Mwezi huu kukatokea agizo lakuhuisha taarifa za wafanyakazi ili ziwe zakisasa na halisia kuliko mwanzo.
Zoezi hili lilihusisha urekebishaji wa baadhi ya taarifa zilizopo kwenye mikataba ya wafanyakazi ambayo waliijaza walipoajiriwa.

Kwa kuwa wakati tunaanza kazi hatukuwa na familia, sehemu ya warithi Kwenye mikataba tulikuwa tumeweka wazazi na ndugu zetu. Sasa kutokana nakuwa na familia tulichopanga mimi na mwenzangu nikwamba kwenye maboresho tujiandike sisi wenyewe Kama warithi wakwanza pamoja na watoto wetu.Mimi kwenye mkataba nikamweka mke na watoto wangu Kama tulivyokubaliana.

Nimekuja kushtuka baada ya kuona mkataba wa mke wangu ambapo yeye kamwandika baba yake mzazi pamoja na watoto. Mimi hakuniandika kabisa.

Mkataba wake nimefanikiwa kuuona baada ya kuongea namhusika aliyekuwa anaikusanya Kisha kuipeleka sehemu husika.Hadi saivi mke hajui kwamba nimegundua kitendo hicho.

Najiuliza,hili tukio mke kalifanya kwa makusudi au bahati mbaya.

Au kitaalam sio lazima mwanamke kumwandika mumewe Kama mrithi?

Jee, niendelee kujifanya sijui au nimuulize nijue nia yake yakufanya hivyo?

Wasalaam!
Muulize akizingua na wewe mwandike baba yako au mama,upuuzi huu!
 
Back
Top Bottom