Kwenye mkutano wa ACT-Wazalendo Lindi hakukuwa na Mwananchi mwenye Elfu 10 mfukoni. Halafu tunaambiwa tuna Uchumi wa Kati

Mkuu unaongelea masuala makubwa kama vile unaongelea habari za kina Haji Manara na Antonio Nugaz.

..uchumi wa kati, ni kweli au siyo kweli?

..umma uliokusanyika kumsikiliza Bernard Membe umetoa majibu.
 

Taarifa kutolewa na uhalisia ni vitu tofauti.

Na huwezi kuwakwepa maskini popote utakapoenda duniani.

Serikali inatengeneza mazingira wezeshi ya uchumi kukua, wenye maarifa na kujituma wanayatumia katika kujipatia maendeleo.

Wenye kupenda sarcasm wanaishi kufanya kejeli mitandaoni.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]...mbinguni huingii
 
..uchumi wa kati, ni kweli au siyo kweli?

..umma uliokusanyika kumsikiliza Bernard Membe umetoa majibu.

Sampling ya waliohudhuria ni ndogo mno mkuu.

Hao kina Membe wamepiga siasa nyepesi za kampeni. Na wameweza “kuwapata” baadhi ya wenye kuitazama dunia kijuujuu tu.
 
..Hold on!!

..kwa hiyo inawezekana kabisa serikali ya Magufuli wamewapa WB data za uongo zilizopelekea tukapandishwa daraja.

..kwa kweli sikuwahi kulifikiria suala hili ktk angle hiyo.
Kama tu za corona zimelifichwa,kipi kinashindikana
 
Unaenda kwny Mkutano wa Mafundi Gereji halaf unauliza mwenye nyavu…akikosekana una conclude Nchi haina wavuvi?

Au unaenda kwny Mkutano wa Waganga wa kienyeji halaf unauliza mwenye thermometa akikosekana unasema jamii hiyo haina Daktar?

Unakusanya wavivu halaf unategemea watapataje pesa?
 
Kusini kurudia kosa ni kuhalalisha zuluma ya soko la korosho, mbaazi na ufuta kwa Utawala huu Hakuna tegemeo la korosho kuja kupanda bei,
Piga kura ya hapana Ni heri lakini umeitendea haki nafsi yako hata Kama atarudi kubabe
 
pesa ziko kwenye mpesa, ni jpm tu ndio anakaa nazo kwenye boot ya gari
 
Dah!

We jamaa nilikuwa nakuchukulia mtu makini sana,angalia unapoelekea mkuu.
 

Labda walikuwanazo kwenye simu zao au kule benki kama wana akaunti benki.
 
Walikuwa nazo kwenye mpesa,tigo pesa ,airtel money na benki.Yeye aliuliza walionazo mfuko wakasema hatuna
 
Wahudhuriaji wengi wa hayo mambo ndio walivyo, Watu hawawezi kuacha ofisi au biashara Mkuu.
Naam so far hao watu ni wengi na ni watanzania basi we are not doing something right...., after all hawa watawala si wapo pale kuhakikisha majority are not left behind ?, au mimi ndio nipo out of touch?
 
Siku hizi mitandao ya benki na huduma za pesa imeenea.

Watu hawatembei na hela mifukoni...
 
Wewe unatarajia 'watu wasiotaka kufanya kazi, watu wasiofanya kazi, watu wanaosubiri kipindi cha uchaguzi ndio "wavune", wana siasa uchwara" and the like wapate wapi pesa? Na sio wakati huu tu; 2000 nilibahatika kwenda kufanya uwezeshaji kwenye wilaya tano za Lindi na Mtwara, tulikuwa tukitoa posho ya shilingi 15000/ kwa kila mshiriki na hiyo ni mbali na msosi wa asubuhi na mchana, kwa hali hii, kiongozi mmoja alikuja kwenye mafunzo na mkewe pamoja na vijana wake wawili (kama washirika) - posho hiyo. Ninachosisitiza hapa ni kuwa - hali hii ya "umasikini wa kipato" iko huko siku nyingi hata wakati Membe akiwa Mbunge wao, SIYO KWELI KUWA IMEANZA LEO.
 

..sera nzuri za uchumi na maendeleo za Pombe Magufuli zilipaswa kuinua maisha ya watu wa kusini.

..halafu kuna malalamiko nimeyasikia kwamba kusini wameendelea kutengwa na kudharauliwa kwa muda mrefu sasa.

..kwamba wao wamejengewa barabara kuu tu, wakati maeneo mengine wanajengewa mpaka barabara za kwenda wilayani na vijijini.

..labda fedha zilizotumika Chato Int airport, daraja la busisi, na daraja la coco beach, zilipaswa kuelekezwa kujenga barabara za mikoa ya kusini.

cc tindo
 
Sema Membe alifanya uhuni jana, ameiba comment yangu niliyoiandika humu jf lakini ameshindwa hata kuni acknowledge.
 
Sema Membe alifanya uhuni jana, ameiba comment yangu niliyoiandika humu jf lakini ameshindwa hata kuni acknowledge.

..lakini bango lililotia fora ktk kampeni ni lile lililoandikwa, " uchumi wa kati bila ajira ni sifa za kijinga. "
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…