Naomba kupata ufafanuzi wakati wanagawana bara la Afrika nani alipewa Tanganyika, na Muingereza alipewa kututawala ama kutusimamia mpaka tukipata uwezo wa kujisimamia wenyewe ama?
Nashindwa elewa hapo, je uhuru tuliupata baada ya mjeruman kunyang'anywa na muingereza akapewa kutusimamia tu ama atutawale?
Kama alipewa kutusimamia kwanini alichukua mali zetu? Mwingereza lichukua madini na kujenga Nairobi Kenya ambako ndiko kulikuwa na Head Quater zao, Je hatuwezi kumdai kwa alichochukua kwetu wakati huo akiwa kapewa kutuangalia tu mpaka tuweze kujisimamia?Mkutano wa Berlin ulimpa Ujerumani koloni linaloitwa Deutsch-Ostafrika ambalo lilikuwa ni mchanganyiko wa Tanganyika na Rwanda-Urundi. Lakini baada ya Ujerumani kushindwa vita ya kwanza ya dunia Umoja wa mataifa wa wakati huo uitwao The League of Nations uliamua kuyagawa makoloni ya Ujerumani chini ya usimamizi (Mandate Territories) wa mataifa yaliyoshinda. Tanganyika alipewa Uingereza na Rwanda-Urundi akapewa Ubelgiji.
Baada ya vita ya pili ya dunia kuisha mwaka 1945 Umoja wa Matafia uliamua kuyaacha haya makoloni chini ya usimamizi ule ule wa Uingereza na Ubelgiji. Kipindi hichi yaliitwa Trusteeship Territories, lakini ukiangalia kiundani zaidi huu haukuwa usimamizi bali ni mfumo uliohalalisha ukoloni kwa kutumia sheria za kimataifa.
Ukisoma vizuri utakuja kukuta kwamba Mandate or Trusteeship Territories yalikuwa hayana utofauti wowote ule na makoloni mengine duniani. Jina na aina ya unyonyaji vilikuwa ndivyo tofauti, kwamba Ujerumani alitumia Direct Rule na Uingereza alitumia Indirect Rule lakini features of colonial states were very present.
Katika historia hakuna aliyepewa Tanganyika. Maana hali halisi Mkutano wa Berlin wa 1885 hawakugawa Afrika. (mkataba wake unaweza kusoma hapa General Act of the Berlin Conference on West Africa, 26 February 1885 ). Hakuna kugawana. Eneo 1 tu lilitajwa kama mali ya Mzungu, ni Kongo. Lakini walipatana kuhusu utaratibu wa kudai utawala kuhusu maeneo ya Afrika kama nchi ilitaka kuenea pale. Mapatano haya yalisababisha ugawaji uliofuata, ukifungua General Act, ni vifungu 34 + 35. Maana kila nchi iliyotaka kuleta madai kuhusu maeneo ya Afrika ilitakiwa kuonyesha ya kwamba walikuwepo hali halisi. Njia bora ilikuwa kuanzisha kituo fulani na kuonyesha bendera.Naomba kupata ufafanuzi wakati wanagawana bara la Afrika nani alipewa Tanganyika, na Muingereza alipewa kututawala ama kutusimamia mpaka tukipata uwezo wa kujisimamia wenyewe ama?
Nashindwa elewa hapo, je uhuru tuliupata baada ya mjeruman kunyang'anywa na muingereza akapewa kutusimamia tu ama atutawale?