Kwenye Utawala wa awamu ya 5, Viongozi wa Chadema walikamatwa, walitekwa, walifungwa jela, walipotezwa, walijeruhiwa na wengine waliuawa

Kwenye Utawala wa awamu ya 5, Viongozi wa Chadema walikamatwa, walitekwa, walifungwa jela, walipotezwa, walijeruhiwa na wengine waliuawa

Tunaendelea na nyuzi zetu za mwezi huu wa 3, ambao ni Mwezi wa Mungu.

Kwenye utawala wa Awamu ya 5, ulioongozwa na Dkt. John Magufuli, Karibu viongozi wote wa Chadema wa ngazi zote walitekwa, walikamatwa, walijeruhiwa, waliuawa na walirundikwa selo ama walifungwa jela, kwa kesi za uongo ili kuwakomoa.

Wanaouliza kwanini tunayaleta haya leo , jibu lake ni hili , ni kwa sababu hatutaki uchafu huu urudiwe tena kwenye Nchi yetu nzuri, Never and Never again.

Alphonce Mawazo alikuwa kiongozi wa mwanzo kabisa kuuliwa baada ya awamu ya 5 kutwaa madaraka, huyu alipigwa mashoka kuliko hata yale wanayopigwa ng'ombe wa nyama machinjioni.

View attachment 2936409

Alphonce Mawazo ni miongoni mwa watu walioua CCM Kanda ya Ziwa, hii ndio sababu kubwa ya kuuawa kwake , serikali ya Jiwe ikazuia mazishi yake kwa siku kadhaa , yaani wamemuua lakini hawataki azikwe , Mawazo anaingia kwenye historia ya Taifa kuwa mwanasiasa wa kwanza kuzikwa kwa Hati ya Mahakama .

Mwl Nyerere aliwahi kunukuliwa akisema kwamba anayekula nyama ya mtu haachi, hakika ndivyo ilivyokuwa, baada ya Mawazo mambo ya kukamata viongozi wa Chadema yakashika kasi, Godbless Lema akakamatwa na kupewa kesi na kisha kunyimwa dhamana kwa tuhuma za kutoa unabii hadharani , hata hivyo unabii huo ulikuja kutimia bila hata kupunja .

View attachment 2936423View attachment 2936426

Kama haitoshi viongozi wa Chadema wakaanza kuwindwa na kukamatwa kama kuku wa Pasaka, Tundu Lissu akapigwa risasi zisizo na idadi kwa lengo la kumuua, ikaelekezwa azikwe haraka na hotuba ya kusomwa kwenye mazishi yake ikaandaliwa.

Mbunge wa Mbeya Mjini, Sugu akakamatwa na kufungwa jela kwa kesi ya uongo, Hakimu aliyemfunga jela Michael Mteite akapandishwa cheo.

View attachment 2936433View attachment 2936434

Viongozi wote wa Chadema Tunduma walikamatwa akiwemo Meya wa Mji huo Ally Mwafongo na kupewa kesi ya uzushi ya mauaji, yaani viongozi 57 wote wanadaiwa kuua mtu mmoja tu wa CCM haya ndio mambo ya awamu ya 5.

Mdude akatekwa na kuteswa nusu ya kufa, shukrani ziwaendee Wazungu walioingilia kati hadi akapatikana.

Karibu viongozi wote wa Kamati Kuu ya Chadema akiwemo Freeman Mbowe walikamatwa na kuswekwa gerezani kwa tuhuma za uongo za kusababisha mauaji ya Akwilina, Ambaye alipigwa risasi na Polisi chini ya Lazaro Mambosasa aliyekuwa RPC, viongozi wa Chadema wakahukumiwa kifungo au kulipa faini ya Mamilioni ya hela za kitanzania, unaweza kushangaa walioua ni Polisi, lakini waliohukumiwa ni Chadema!

Hivyo ndivyo Hakimu Thomas Simba alivyoona, Shukrani sana kwa Watanzania walioamua kuchanga fedha zao ili viongozi hao wa Chadema wasiozee jela

Wanachadema waliopotea, kuteswa na kufungwa ni wengi, akiwemo Bernard Saa Nane ambaye hadi leo hajulikani aliko

Nitasema kweli Daima fitina kwangu mwiko
Safi..👏👏👏👏👏
 
Hilo uliloandika limeongeza wigo halijamtoa jiwe kwenye uhusika
Ukumbuke pia hapa sio Mahakamani.

Narudia, ukiwa unatuhumu Serikali wakati wa Utawala wake J.P.M... Msisahahu kuwaweka Wahusika wote. Zaidi ya hapo hizi kampeni zenu, kwa jicho la kisheria, kama ilovyokuwa kwa Cyprian Musiba ni Defamation.

Magulification will go on, no doubt.

CHADEMA hamna kesi, this is slandering

Ngoja nikumbushe tu na hili chini.
Viongozi wa jf ni ajabu kubwa mno kuuacha uzi wa uongo na uchochezi wa kiwango cha kutisha namna hii .
 
Tupe tafsiri ya tusi tafadhali la sivyo tutakuona punguani tena takataka. Vile vile utupe na mfano wa matusi Lissu aliyotukana pamoja na Mdude. Ukishindwa tutakuona wewe ni takataka tu
Matusi ya Mdude_Nyagali alitamka pale Tabata Baracuda mwezi Juni mwaka 2021 alipotoka gerezani kwa msukumo wa Samia.

Lissu alisema maamuzi ya Rais Samia ni akili au matope baada ya mkataba wa DP WORLD mwaka 2023 Agosti
 
Kwamba Mbowe alifungwa awamu ya Tano ?

No wonder watu wanadhani mmekula mlungula ili mgeuke kuwa Propagandists wa Samia...
 
Ilikuwa usanii tu,waliojiteka walijiteka,waliokunywa konyagi wakaanguka kwenye ngazi wakasema wamepigwa, Mwenyekiti wa Chadema Temeke,ndugu Yona alisema alitekwa na Chadema,Dr Slaa,Katibu Mkuu wa Chadema akasema walinzi wake walimwambia wao ndio walimteka Yona,hao Chadema wakaita waandishi wa habari wakalaumu usalama wa Taifa ndio wanateka,ilikuwa ni usanii tu kutafuta kiki.
 
Ilikuwa usanii tu,waliojiteka walijiteka,waliokunywa konyagi wakaanguka kwenye ngazi wakasema wamepigwa, Mwenyekiti wa Chadema Temeke,ndugu Yona alisema alitekwa na Chadema,Dr Slaa,Katibu Mkuu wa Chadema akasema walinzi wake walimwambia wao ndio walimteka Yona,hao Chadema wakaita waandishi wa habari wakalaumu usalama wa Taifa ndio wanateka,ilikuwa ni usanii tu kutafuta kiki.
Kwenye utekaji, dhalimu magu hasafishiki.
 
Kwamba Mbowe alifungwa awamu ya Tano ?

No wonder watu wanadhani mmekula mlungula ili mgeuke kuwa Propagandists wa Samia...
Nani aliaema hayo unayoandika ? usichangie kama hujaelewa
 
Ukumbuke pia hapa sio Mahakamani.

Narudia, ukiwa unatuhumu Serikali wakati wa Utawala wake J.P.M... Msisahahu kuwaweka Wahusika wote. Zaidi ya hapo hizi kampeni zenu, kwa jicho la kisheria, kama ilovyokuwa kwa Cyprian Musiba ni Defamation.

Magulification will go on, no doubt.

CHADEMA hamna kesi, this is slandering

Ngoja nikumbushe tu na hili chini.
Ukipinga uzi wangu huu utashangaliwa hadi na vichaa ,kama tunaandika uongo weka ukweli
 
Back
Top Bottom