Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
safi sana kabla hajawa mbunge tayari ametoa ajira kubwa jimboni.sasa DR.wa sheria ya Katiba kafanya nini zaidi kwa wanaKyela?kwanini asijikite kwenye Corporate Law?
Financial crisis ni sooo.....lazima wafulie....unajua mie hii kitu inanikera sana....ati ku;eta mabadiliko lazima uwe mbunge? nakereka sana mwangalieni kijana kama mwakaL atakavyofulia.....Nikweli George anagombea Kyela kwa kupitia CCM, na nime confirm hilo kutokana na mmoja wa washauri wake ambaye anaishi hapa USA na amekwenda Tanzania kuungana na yeye.
1.joji 2.wiliamu 3.? labda nyani ngabu,masanilo au fidel80......- Jamii Forum, kutoka Jambo Forum baada ya TEF, kabla ya BCS. JF yaani Taasisi ya Great Thinkers, finally ime-produce vijana watatu watakaojitosa kwenye kinyanga'nyiro cha ubunge wa Tanzania katika majimbo matatu ya taifa,
Du mjadala mtamu sana, wengine tunangoja muda mwafaka risasi zenyewe chache kwa hiyo inabidi kuzitumia kwa uangalifu sana.
Kifupi nilienda Mbeya na kuzunguka kwenye majimbo ya Kina Mwakyembe, Mwakyusa na Mwandosya nikagundua mambo mengi ya kuchekesha na kuhuzunisha sana.Mnaelewa siasa za Kyela na Mbeya kwa ujumla ni ngumu sana kuliko sehemu yoyote Tanzania. Mtasikia na kwa Prof. Mwandosya nako muda si mrefu
Wakati mwingine hata ukipata vichwa, tatizo linakuwa ni sera za vyama kwa maana inafika wakati wanalazimika kuhubiri sera za chama na si yale wanayoyaamini wao wenyewe. Kama kungekuwa na utaratibu wa wagombea binafsi, hapo ndipo tungeshuhudia vichwa vikishindana kikwelikweliIli kuleta ushindani wa kweli kwenye chaguzi majimboni ni vizuri sana kupambanisha vichwa kwa vichwa, hii inasaidia sana wagombea kuwa makini katika kumwaga sera zao na kuhakikisha zinatekelezwa ipasavyo.
Umeme wengine wamevuta kwa kupitisha maeneo ambapo hawataki kushirikiana na majimbo ya wenzao ambao wapo majimbo jirani hivyo umeme unaenda kwenye jimbo la mmoja na hataki wenzake waunganishe kwenye line ileile.
Endapo Mwakyembe atashindwa Ubunge itakuwa ni simanzi kubwa katk nchi nzima na nafurahi kwa sababu sioni uwezekano wa hilo kutokea Kyela 2010. Ata Mwang'onda alileta upinzani kwa Mwandosya kwenye UNEC mkoa na kwa mishemishe nyingi kama alizoanza nazo Mwakalinga lakini mwisho wa siku wote tunajua matokeo yalikuwaje,na hilo ndilo litakalotokea Kyela 2010.
Mimi wote Mwakyembe na Mwakalinga najua ni JF members ambao wanatumia Pen names, lakini kwa aliyeenda Kyela na kujionea hali halisi hawezi kusema Mwakyembe kafanya kitu cha ajabu kwa wana Kyela mpaka mawe yaongee.Hujui alichofanya Dr. mpaka mawe yanaongea!! nchi inatikisika!! hujui tuuu!!
Nakumbuka wakati naongea na Mwakalinga alisema haya:
Sasa sitashangaa kama kaamua kugombea rasmi, yaelekea ndo maana hata SteveD hajatia neno katika topic hii, atakuwa alipata kanusho toka kwa Mwakalinga na anashtushwa na habari hizi!
- Si kweli kuwa nimekuja Tanzania rasmi kugombea Ubunge, ikiwa hivyo nitawafahamisha watu wazi bila kificho.
- Mwakyembe anajaribu kunimaliza hata kabla sijafikiria kupambana naye kwa kutumia gazeti la Majira. {Mwezi Machi aliwahi kunipigia simu akinieleza kuwa Mwakyembe (ambaye pia ni member wa JF) alikuwa akimsumbua sana kwenye PM na alidai kuwa anatumia gazeti la Majira kuendeleza propaganda dhidi yake.}
- Hata kama nikigombea Kyela kwani jimbo hilo Mwakyembe ana hati miliki nalo?
Sasa hizi siasa za chuki ndo zinaiua Mbeya kwa ujumla!Kikubwa unajua wananchi wa Kyela na wa Tukuyu hawaivi kabisa.
Malafyale,Steve D na Field Marshal,kunisakama sana kwa habari yangu iliyofanyiwa uhakiki sana wilayani Kyela ya kugombea Mwakalinga sasa tunawaomba toeni tamko maana mlituhakikishia kabisa kuwa Mwakalinga HANA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KYELA 2010!
Mwakalinga George nahisi sisi wana Kyela tunamfahamu zaidi kuliko hawa akina SteveD na Field Marshal ambao najua wanamjua kwa sababu tu ya kukutana kwao makazini au kwenye mahusiano ya mitandao kama vile hapa JF na kwingineko!
Kwa taarifa zaidi Mwakalinga sasa wanashirikiana na mkuu wa Mkoa wa Mbeya mzee Mwakipesile kufanya kampeni kumuangusha Mwakyembe;na habari zaidi mwenyekiti wa Mwakalinga wa kampeni kijana mnyakyusa mzaliwa wa Kyela , profesa,msomi wa elimu-mafuta anayefanya kazi zake nchini USA jinbo la California kawasili Dar jana na leo anaelekea Kyela tayari kabisa kufungua rasmi kampeni za chinichini za Mwakalinga!
Yatakayojiri zaidi tutawaeleza na plz Steve D na Field Marshala tupeni tamko la Mwakalinga maana nyie ni kama vile mlitaka tuamini kama vile ndiye wasemaji wake na wala si huyu Profesa anayeingia leo hapa Kyela!
Kwa taarifa zaidi Mwakalinga sasa wanashirikiana na mkuu wa Mkoa wa Mbeya mzee Mwakipesile kufanya kampeni kumuangusha Mwakyembe;na habari zaidi mwenyekiti wa Mwakalinga wa kampeni kijana mnyakyusa mzaliwa wa Kyela , profesa,msomi wa elimu-mafuta anayefanya kazi zake nchini USA jinbo la California kawasili Dar jana na leo anaelekea Kyela tayari kabisa kufungua rasmi kampeni za chinichini za Mwakalinga!