Next Level
JF-Expert Member
- Nov 17, 2008
- 3,153
- 180
Haya kaka naona laptops zimekuchanganya....mweka hazina wa Tanzanet kumwangusha Dr Mwakyembe.....hii itakuwa sawa na Osama Bin Laden kuwa Papa wa Roman Catholic, tunasubiria hiyo 2010 tuombe uzima Gwamaka K
Masa,
Hapo nilipo highlight umeniacha mbavu zangu zimevunjika.....huu ulinganisho never imagined! OBL to be RC Pope?....!
Huku nyuma tulishasema Mtanzania ndiye Mwakalinga, tukatukanwa, leo hii imedhihiri. Tulitishwa kwamba anazo data za wachangiaji fulani hadi mmoja kutilia mashaka MODs kwamba yawezekana kuna uwezekano ID za watu zinafichuliwa. Naamini JF ni jamvi lenye malengo yake mazito kwa taifa hili kuliko siasa za Kyela, lakini Mwakalinga a.k.a Mtanzania aliligeuza kuwa jamvi la siasa za Kyela, waelewa tulilishitukia hilo na tukaamua kukaa kimya. Naye ID yake ilipobainika kupitia uchangiaji wake akakimbia, najua bado yupo kwa jina jingine anapochangia kwenye siasa za Kyela.
Tatizo haliko kwa yeye kugombea Kyela, la hasha bali ni pale alipogeuza jamvi hili kama jukwa lake la kufanyia kampeni na hata kinachoendelea hapa ni kumpamba aonekane ni mzalendo wa kweli wakati sio kweli, na wakati ukifika itabainika kama ilivyo sasa.
Mwandishi wa Majira hajapika kitu, huyu ni mpambe wake na ndio maana hakutaka waandishi wa habari wengine wahusike. Hivyo hajatafuniwa maneno, kilichoandikwa ndicho alichotaka kitoke, na hapa ndipo udhaifu wake unapojibainisha kwa mara nyingine tena.
Mwakalinga haelewi kuwa utaratibu kura za maoni umebadilika, amekumbatia UVVCCM ambao siku zote chaguzi kwao ni gulio la rushwa, na tayari wameanza kupingana wenyewe kwa wenyewe kila mtu kutaka kuwa karibu naye, na watamla kweli kweli.
Kutokana na kujitambulisha kwake kuwa mwanzilishi wa JF ni lazima aweke bayana humu isije ikawa ndiye MOD mwenyewe, la sivyo JF inapoteza umaarufu wake siku si nyingi, wengine sio wataalamu wa IT, tutakosa imani na jamvi hili kwa sababu litakuwa na sura ya mtu au watu.
Pamoja na kumkaribisha Kyela, yeye pamoja na wapambe wake wanapaswa kufahamu mambo makuu ya muhimu kwa siasa za Mbeya.
1. Unapotaka kugombea ni lazima ujiridhishe kuwa unakubalika na wananchi a sio viongozi wa CCM. Dr Mwakyembe tangu ajitose Kyela hakuwa chaguo la CCM, viongozi wote waliimba wimbo wa Mwakipesile akiwemo shemeji yake aliyekuwa Mwenyekiti CCM Wilaya, lakini aliwabwaga, na hadi leo ngome yake kuu ni wananchi na wala sio viongozi wa CCM.
2. Kuingia kwa gia ya kupigiwa debe na kina Mwakipesile, RA na EL ni mweleka tosha katika siasa za Mbeya, huku hawataki viongozi wa kuchongewa, na hilo ndilo linalomtesa Thom Mwang'onda. Mwakalinga anaeleweka kuwa kapelekwa na Mwakipesile kwani huyo RC anapita akiwaeleza wananchi huko kuwa anawapelekea kijana toka UK, utapigiwaje kampeni na mtu aliyechafuka! Alimpigania THOM kwenye U-NEC akitumia ma DC wote na viongozi wa CCM bado alibwagwa vibaya.
3. Ujasiri na misimamo ni moja ya sifa za kuwa kiongozi Kyela, Mwakalinga ameshaonyesha woga, leo aseme sigombei, akiandikwa kidogo kuwa anagombea anatuma wake wapambe kutishia waandishi wa habari, halafu anakuja tena kutangaza anagombea, hawezi kubalika. Moja ya kete nzito ya Dr Mwakyembe Kyela ni ujasiri, anachukuliwa kuwa taswira hasa ya watu wa Kyela, hasa pale alipoisoma ripoti ya Richmond bila kupepesa macho.
4. Fitina, uongo na inda anavyovionyesha hapa kupitia baadhi ya wachangiaji kuhusu Dr havimsaidii kabisa zaidi ya kumwonyesha kuwa yeye ni mtu wa aina gani. Mara amejenga ghorofa kwa fedha za KDF, mara sijui huko Dodoma kaja na lexus, mara hana nyumba Kyela nk.
5. Kampeni za kuwafanya wana Kyela kuendelea na utegemezi hazimsaidii chochote, e.g kila mtu laptop, nitaibadilisha Kyela kuwa kama Ulaya, nitatoa ajira, zinaeleweka kuwa ni ghiliba za CCM miaka nenda rudi, kwani walishambiwa Maisha bora kwa Kila Mtanzania na hawayaoni.
6. Akumbuke kuwa tunahita kiongozi mwenye mtanzamo wa Tanzania na sio kieneo- Kyela, matatizo ya kitaifa kama vile ufisadi uliopo huko juu ndio ukoma unaoitafuna nchi, tukisafisha huko juu ni wazi huku chini kila kitu kitaenda sawa.
Mwisho niseme kwamba ni mjinga tu ambaye hawezi tambua mchango wa Dr. Mwakyembe kitaifa na jimboni mwake Kyela.
Mwakalinga a.k.a Mtanzania karibu sasa Kyela utugawie hizo laptop nasi tukawauzie wenye kuelewa jinsi ya kuzitumia kisha pesa tukanywee KADANSANA kutoka Malawi!!!!!
George Mwakalinga mwana Kyela aliyekuwa anaishi na kufanya kazi kama mtaalaum wa kompyuta nchini UK amewasili Kyela majuzi na tayari ametangaza kuwania ubunge wa wilaya ya Kyela ndani ya CCM!
Mwakalinga ametoka kuongea na wana Kyela sasa hivi kwenye hotel ya kisasa ya Sativa na watu waliokuwepo hapo wanasema hapana shaka Mwakalinga kaletwa Kyela na vigogo ndani ya CCM na serikalini na dhahiri anaungwa mkono na mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mzee Mwakalinga na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Japhet Mwakasumi!
Kwa mujibu wa habari za watu wa Kyela,kama uchaguzi wa kura za maoni ndani ya CCM utafanyila leo kwenye kata 15 zinazounda wilaya hiyo, Mwakalinga na Dr Mwakyembe watashinda kata 6 kila mmoja na kata 3 zikiwa ni "swing states".
Kata ya Kyela mjini,kata ya Matema na kata ya Ngonga sehemu ambapo wana siasa hawa wanapotokea ndiyo kata pekee za"swing states"lkn kata ya Kyela mjini ikianza kuegemea upande wa Mwakalinga na kumpa sasa likely kama anaongoza kwa kata 7 kwa 6 za Dr Mwakyembe!
Bila ubishi kata ya Ikolo,kata ya kajunjumele,kata ya Katumba Songwe,na kata 3 za mashariki ya Kyela hizo zitachukuliwa na Dr Mwakyembe ili hali kata ya Ipinda,kata ya Lusungu,kata ya Makwale na kata 3 kuzunguka upande wa Magharibi hasa kuanzia mpakani mwa Kasumulu na mgodi wa Kiwira zitachukuliwa na Mwakalinga kwa kile wanachosema Dr Mwakyembe kashindwa kazi ya kuwasadia wahanga waliofukuzwa kazi kwenye mgodi huo na vijiji jirani!
Mwakalinga,ambae pia ana vitege uchumi vingi sana wilayani Kyela zikiwemo hotel kubwa za kisasa tayari yupo Kyela,na kaanza kuzunguka kwa kasi vijijini kujinadi kwa wana CCM na kuna kila ukweli kuwa viongozi wa CCM wilayani na mkoani wamebariki kuanza huku kwake kampeni kabla ya muda wake.
Juhudi zinafanywa ili mazungumzo ya Mwakalinga akiwa kyela ambako tayari sasa kafanya ndiyo makazi yake yapatikane na yaletwe hapa ili wana JF wayachambue!
Naamini kama umekwenda shule utajua maana ya kuwekeza kwenu na faida yake. Kila siku Rais wako anazunguka huku na huko kutafuta wawekezaji, wewe unanufaika vipi? Debe tutapiga na kwenye ukweli tutasema tu. Ajira watu wa Kyela watapata wakiwemo wadogo zako wa Ipinda. Mbona Mwakyembe amepeleka power pool Singida, Watu wa Kyela wananufaika vipi? Huyo sio mwenzetu na hatumtaki na kumdhihirishia hilo tutamkataa kwenye kura subiri kilio. Mwambie afanye kudeclare interest, huo ni ufisadi.
Kgwamaka
Nadhani fisadi ni neno pana na labda linakushinda kulifafanua.Sasa kama mlikuwa mkishirikiana na Mwakipesile alipokuwa Mbunge mbona hizo ajira hatukuziona?au mmefunuliwa upya safari hii, teh teh teh!!! na NI KWELI MWAKYEMBE SIO MWENZENU,KWANI YEYE NI MPIGANAJI ANAYEPAMBANA NA MAFISADI WAKATI NYIE MNAJINYENYEKEZA KWA MAFISADI KWA KUTAFUTA MANUFAA YENU BINAFSI NA SIO YA WANA KYELA WALA WATANZANIA,hamuwezi kuwa timu moja.
Haya kaka naona laptops zimekuchanganya....mweka hazina wa Tanzanet kumwangusha Dr Mwakyembe.....hii itakuwa sawa na Osama Bin Laden kuwa Papa wa Roman Catholic, tunasubiria hiyo 2010 tuombe uzima Gwamaka K
Hivi MTUME PAULO kabla hajawa Paulo alikuwa nani vile? Yohana Mbatizaji?
Mh Spika naomba mwogozo hili swali halieleweki.....!
Nadhani fisadi ni neno pana na labda linakushinda kulifafanua.
Hata yeye ni fisadi, ziko wapi pesa za KDF? ana mengi ya kuja kutueleza mwakani, tunavuta pumzi
huku nyuma tulishasema mtanzania ndiye mwakalinga, tukatukanwa, leo hii imedhihiri. Tulitishwa kwamba anazo data za wachangiaji fulani hadi mmoja kutilia mashaka mods kwamba yawezekana kuna uwezekano id za watu zinafichuliwa. Naamini jf ni jamvi lenye malengo yake mazito kwa taifa hili kuliko siasa za kyela, lakini mwakalinga a.k.a mtanzania aliligeuza kuwa jamvi la siasa za kyela, waelewa tulilishitukia hilo na tukaamua kukaa kimya. Naye id yake ilipobainika kupitia uchangiaji wake akakimbia, najua bado yupo kwa jina jingine anapochangia kwenye siasa za kyela.
Tatizo haliko kwa yeye kugombea kyela, la hasha bali ni pale alipogeuza jamvi hili kama jukwa lake la kufanyia kampeni na hata kinachoendelea hapa ni kumpamba aonekane ni mzalendo wa kweli wakati sio kweli, na wakati ukifika itabainika kama ilivyo sasa.
Mwandishi wa majira hajapika kitu, huyu ni mpambe wake na ndio maana hakutaka waandishi wa habari wengine wahusike. Hivyo hajatafuniwa maneno, kilichoandikwa ndicho alichotaka kitoke, na hapa ndipo udhaifu wake unapojibainisha kwa mara nyingine tena.
Mwakalinga haelewi kuwa utaratibu kura za maoni umebadilika, amekumbatia uvvccm ambao siku zote chaguzi kwao ni gulio la rushwa, na tayari wameanza kupingana wenyewe kwa wenyewe kila mtu kutaka kuwa karibu naye, na watamla kweli kweli.
Kutokana na kujitambulisha kwake kuwa mwanzilishi wa jf ni lazima aweke bayana humu isije ikawa ndiye mod mwenyewe, la sivyo jf inapoteza umaarufu wake siku si nyingi, wengine sio wataalamu wa it, tutakosa imani na jamvi hili kwa sababu litakuwa na sura ya mtu au watu.
Pamoja na kumkaribisha kyela, yeye pamoja na wapambe wake wanapaswa kufahamu mambo makuu ya muhimu kwa siasa za mbeya.
1. Unapotaka kugombea ni lazima ujiridhishe kuwa unakubalika na wananchi a sio viongozi wa ccm. Dr mwakyembe tangu ajitose kyela hakuwa chaguo la ccm, viongozi wote waliimba wimbo wa mwakipesile akiwemo shemeji yake aliyekuwa mwenyekiti ccm wilaya, lakini aliwabwaga, na hadi leo ngome yake kuu ni wananchi na wala sio viongozi wa ccm.
2. Kuingia kwa gia ya kupigiwa debe na kina mwakipesile, ra na el ni mweleka tosha katika siasa za mbeya, huku hawataki viongozi wa kuchongewa, na hilo ndilo linalomtesa thom mwang'onda. Mwakalinga anaeleweka kuwa kapelekwa na mwakipesile kwani huyo rc anapita akiwaeleza wananchi huko kuwa anawapelekea kijana toka uk, utapigiwaje kampeni na mtu aliyechafuka! Alimpigania thom kwenye u-nec akitumia ma dc wote na viongozi wa ccm bado alibwagwa vibaya.
3. Ujasiri na misimamo ni moja ya sifa za kuwa kiongozi kyela, mwakalinga ameshaonyesha woga, leo aseme sigombei, akiandikwa kidogo kuwa anagombea anatuma wake wapambe kutishia waandishi wa habari, halafu anakuja tena kutangaza anagombea, hawezi kubalika. Moja ya kete nzito ya dr mwakyembe kyela ni ujasiri, anachukuliwa kuwa taswira hasa ya watu wa kyela, hasa pale alipoisoma ripoti ya richmond bila kupepesa macho.
4. Fitina, uongo na inda anavyovionyesha hapa kupitia baadhi ya wachangiaji kuhusu dr havimsaidii kabisa zaidi ya kumwonyesha kuwa yeye ni mtu wa aina gani. Mara amejenga ghorofa kwa fedha za kdf, mara sijui huko dodoma kaja na lexus, mara hana nyumba kyela nk.
5. Kampeni za kuwafanya wana kyela kuendelea na utegemezi hazimsaidii chochote, e.g kila mtu laptop, nitaibadilisha kyela kuwa kama ulaya, nitatoa ajira, zinaeleweka kuwa ni ghiliba za ccm miaka nenda rudi, kwani walishambiwa maisha bora kwa kila mtanzania na hawayaoni.
6. Akumbuke kuwa tunahita kiongozi mwenye mtanzamo wa tanzania na sio kieneo- kyela, matatizo ya kitaifa kama vile ufisadi uliopo huko juu ndio ukoma unaoitafuna nchi, tukisafisha huko juu ni wazi huku chini kila kitu kitaenda sawa.
mwisho niseme kwamba ni mjinga tu ambaye hawezi tambua mchango wa dr. Mwakyembe kitaifa na jimboni mwake kyela.
mwakalinga a.k.a mtanzania karibu sasa kyela utugawie hizo laptop nasi tukawauzie wenye kuelewa jinsi ya kuzitumia kisha pesa tukanywee kadansana kutoka malawi!!!!!
duh njaa kweli mbaya,mwakyembe akishindwa ndo we kula hakuna?jifunzeni kujitegemea wa nyumbani....unasema mambo ya kitaifa inamaana mwakyembe hawezi kuendesha mambbo ya kitaifa na yale ya kyela kwa pamoja?
NSESI,
Kama amevaa joho la Kikwete basi ajitangaze kuwa yeye ni Rais wa Tanzania. Naona umekiri kuwa kwao kakimbia na kuvamia kwenye kaya za wenzake.
Mkataa kwao ni mtumwa na zama hizi hatumtaki mtu kama huyo. Huwezi kukimbilia juu ya mti bila kupanda kwa kuanzia chini. Kachaguliwa na wana Kyela, na alitakiwa aanzie pale ndipo aende huku juu, au kama ataweza ayafanye yote kwa wakati moja.
Kama ni kitaifa basi subiri wamchague kitaifa, lakini Kyela mwakani tutamhukumu kwa kutudanganya kwa ahadi kibao ambazo ameshindwa hata kitu kimoja kutekeleza.
Kama na wewe unataka kuja njo tutakupima kwa uwezo wako, vinginevyo hatutaki waimbaji ambao nyimbo zinaishia ukumbini au majukwani, tunataka wanamaendeleo.
Kwa nini majimbo mengine yanapiga hatua na Kyela inabakia gizani? Kwani wale ni malaika? Baado kitambo kidogo, hukumu hiyo.
Kgwamaka
SteveD kafulia mbaya na waraka wake.......yaani ni ile nitoke vipi......alafu kumbe mwakalinga alikuwa kwa ma mvi kudaka mishiko? steveD lazima andike waraka mwingine.....SteveD,
Vipi leo vidole na lips vimebanwa kwa SUPERGLUE mkuu? Talk!Talk!Talk please ....nasubiri comments zako on this mkuu!
Mwakalinga asome kwanza ramani. comments zake kwamba atatumia uzoefu wa kufanya kazi ulaya na pia ameacha kazi nzuri ulaya kuja kuwasaidia wana Kyela tayari zinaonyesha ubabaishaji wa hali ya juu. Hizi nazifananisha na propaganda za siasa za akina Osca Kambona na Abrahamani Babu walipokuwa ukimbizni huko ughaibuni.
Wao walikuwa wanaiona vema Tanzania na kuelewa zaidi jinsi ya kutatua matatizo ya Tanzania kwa kupitia mirror kuliko mtanzania anayeishi hapa Tanzania. Watu wa Kyela kama ni walevi chakari watampa Mwakalinga kura kwani huwezi kuchukua solutions za Ulaya uka zi impose Kyela zikafanya kazi. Kama nabisha muulize Nyerere aliyehamisha zana ya Ujamaa kutoka Israel akaiweka Tanzania bila kupima, ujamaa uko wapi?.
Ushauri wangu ni kwamba Mwakalinga hakuja na gunia la fedha za kugawa wala hana mpango wa kuwagawia wana Kyela vitega uchumi vyake bali amekuja na mdomo wa kuongea kama wanasiasa wengine. Mbaya zaidi kwa habari za kujua wanachohitaji wana kyela ni kama njozi kwake, yaani udhanifu zaidi kuliko uhalisia.
Plse amwache Dr. Mwakembe amalizie kazi ya kuwatoa mochwari mafisadi awazike then baada ya hapo aendelezee hapo la sivyo kikombe cha Mwakembe kikiachwa hakijaisha shubiri ya mafisadi kinaweza kuwa cha moto kwake akakitema.
Kuhusu Mwakembe kushindwa issue moja hiyo isiwe sababu ya kumhukumu plse tuangalie na mazuri aliyofanya kama ni machache kuliko hayo. Watu muelewe kuwapa watu ajira si jambo rahisi haswa katika ulimwengu tunaoishi kipindi hiki Mwakalinga mwenyewe pia hataweza labda awafukuze wafanyakazi kwenye projects zake awalete waliofukuzwa migodini.
Namshauri Mwakalinga atulize boli kwanza tumewaona wengi waliokuja kwa pupa za Ulaya na hatukuona difference. Fedha za maendeleo hutolewa na serikali na kama hawajatoa au wamepunguza utafanya nini kama si kubaki ukilaumiwa na wananchi kama mbunge yeyote ambaye hata hajafika Ulaya.
Please kubali ushauri wangu usidhalilike
Mtaalamu wa Rural Changes & social research
Gerad
Arusha
Subirini 2010 sio mbali na msije kukimbia baada ya kuukosa huo ubunge. Ushauri mdogo tu, msimdangaye jamaa kwa ajili ya kukomba vijisenti vyake anavyosotea huko Ulaya!!!!!
Kumbe Rai ilisema kweli, wapambe wanasubiri kumchuna, na watamchuna kweli akamuulize Thom Mwng'onda!!!!!!