Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM


*** Baada ya muda, simu inaingia*****

.... harooo sukaka (nick name ya morani1)..

mpiga simu -- wewe sukaka nipe waziri mkuu
morani1 -- wasiri mkuu hayupo nani mwensangu?
mpiga simu -- Mwakipesile hapa kwani umenisahau
Morani1 -- Samahani msee, ........ gghahggjfhgjhhhhaggffffggg

----baada ya kimya na kelele zisizoeleweka--

Morani1 (kwa mbali) -- fureghiii fureghiiiiii fureghiiii msee yuko wapi

----- sauti kwa mbali zisizoeleweka.

Lowasa - waziri mkuu hapa na raisi mtarajiwa wa Tanzania.

*** itaendelea****
 

1. Wananchi bado hawajamkinai Mwakyembe, sasa woga wa nini?

2. Hata kama anaamini sana watu na kutapeliwa, wee inakuuma nini? Mwisho si pesa za Rostam Aziz na Lowassa au tuseme pia kuwa ni zao.

3. Upeo wa elimu yake uko chini? Je Wa Mwakyembe uko juu? Juzi anasema wananchi wa Mara waishitaki Barick Gold badala ya kwenda kuwasaidia waishitaki BG? Sasa elimu yake anaitumiaje? Kuanzisha umeme wa UPEPO Sindida na Rostam Azziz? Kama unabisha muulize Dr. Slaa.

4. Mwakipesile aliondolewa ubunge kwa msaada mkubwa sana wa Mwakalinga. Mwakipesile pia aliipiga vita KBS. Leo hii eti kawa mtetezi? I can sence the missing link somewhere.

5. Wazee walikwenda mbio sana, speed gani hiyo? Duu, hao wazee waenda mbio nataka niwaone na mbio zao za sanaaa....

6. Kwa hiyo huo mwongozo umetoka kwa RC, wee umeupitia na kuu-PIMP aka tunning na kutupakulia hapa. Sasa kama umeandikwa na RC, inamhusu nini Mwakalinga? Aliyekuwa anamtumia TAKURURU ninani? Mbona hiyo hujaiandika hapa? Haya, kesho Mwakalinga tunaye hapa na mtu mzima utaaibika. Watu kama nyie ni kuwabana kwa point tu.

Mwisho ni kuwa kama wewe ni kweli ulikuwa kambi ya Mwakalinga, usingelikuja kumpaka hapa namna hiyo. Kama ungelikuwa na lako jambo basi ungelisema hukohuko na haswa mbele yake. Watu wanaokuja kuandika hapa kwa kutumia majina FEKI na huku ulikuwa na mtu hapo Mbeya siku zote kwangu mie huwa nawaona ni ma-FISI fulani hivi. Ni tabia za wanaume wa Mombasa au maneno ya akina mama huko nyuma ya nyumba. Wee Mwanaume mzima unamuogopa mwanaume mwenzio, tena unasema jamaa anaamini sana watu. Si ungelimwambia basi na wewe maoni yako na si kuja hapa kubwabwaja na unategemea watu wenye akili zetu tukuamini? Watakuamini adui zake Mwakalinga na rafiki zake Mwakyembe. Next time ukumbuke wimbo huu hapa chini:

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=d6FwaKlKlb0"]YouTube - Broadcast Yourself.[/ame]
 


Huyu Ridhiwani itabidi atafute kazi nyingine ya kufanya na sio Kyela kupigia kampeni mafisadi wenzake.
 

USHAURI WA BURE KWA MWAKALINGA:

(1) Katika siasa, jifunze kuepuka "personal attacks" ambazo ni rahisi wewe mwenyewe kugeuziwa kibao maana historia yako George mwenyewe ina mushkeri kidogo. Tusibishane, tumesoma wote! Mwakalinga kumbuka daima kuwa: "Ukiwa unaishi kwenye nyumba ya kioo, achana na tabia ya kutupia mawe watu wengine!" Mwongozo au hoja namba 1 hapo juu, achana nayo kabisa maana inaongelea mambo ya UDSM ambako George hukumaliza masomo!

(2) Hoja namba 13-20 ni hoja za chuki binafsi za Mwakipesile zinazotukuza ukabila na majungu na kuwaingiza watu wengine (akina Kifukwe n.k.) kwenye suala lisilowahusu. George ndugu yangu : NENDA KWENYE HOJA"!

(3) Ukirejea tena Bongoland, epuka takrima na events za kuchinja ng'ombe n.k. nyama hiyo itakujakutokea puani! Alfred (unamfahamu) anasema mlichinja ng'ombe kuwafanyia karamu wananchi wa Kata ya Katumba Songwe unakotoka. Leo kakulinda Mwakipesile, kesho hatakuwepo!

(4) Ulitoa kauli Katumba Songwe kuwa umetumwa kumwondoa Mwakyembe. Pengine mwenzetu amekaa mno Ulaya! Hoja kama hiyo ni suicidal mbele ya safari!

(5) There are times brother unajisahau sana na kuwatetea akina Lowassa, Rostam na Mwakipesile ili mradi unamponda Mwakyembe. Staili hii kwa Kyela na sehemu zingine Tanzania ni kujimaliza mwenyewe!

(6) Achana na wapigadebe wa Mwakipesile, tafuta wa kwako! Hizo ndo real politics. Pengine huelewi kuwa Mwakipesile kapoteza kabisa mvuto wa kisiasa Kyela, pamoja na wafuasi wake wote! Ukikaa karibu sana nao,na wewe utaambukizwa ugonjwa huo wa kukosa mvuto! Utaambukizwa madhambi yao!

(7) Ni vema kumjua mshindani wako! Mwakyembe, utake usitake, ni msomi mzuri kukupita na alipata kura asilimia 93 uchaguzi uliopita. Suala la msingi hapa ni kushusha kukubalika kwa Mwakyembe kufikie angalau asilimia 45 ili bnrother uweze kupeta. Usiendeshe kampeni as if unashindana na mgeni mwenzako kwenye siasa!

( Kumbuka - huwezi kumshinda Mwakyembe kwa hoja za jumla jumla ambazo wananchi wana majibu nazo. Kwa mfano, huwezi kusema hakuna maendeleo ya elimu wakati taarifa za Serikali zinasema: mwaka 2005 kulikuwa na shule nane ( tu za Sekondari za Serikali na sasa ziko shule 23 za Sekondari za Serikali. Shule ya 23 ya Ndobho inamaliziwa!

-Huwezi kumshinda Mwakyembe kwa kuongelea nyumba yake Dar es Salaam wakati wewe unaishi London!

-Huwezi kumshinda Mwakyembe kwa kumlaumu ati ana dereva Mchagga badala ya Mnyakyusa (ingawa Msuya ni Mpare), huo ni ukabila! Kama ni hivyo mbona unawatukuza akina Lowassa na Rostam ambao siyo Wanyakyusa? Mbona akina Mwandosya na Mwakyusa wana madereva wasio Wanyakyusa?

-Huwezi kumshinda Mwakyembe kwa kuongelea daraja moja tu wakati madaraja mapya zaidi ya saba yamejengwa katika kipindi chake, na hilo moja unaloliongelea Mwakalinga, Jeshi lenyewe lilitoa tamko (wewe ukiwa London ukila kuklu kwa mrija) kuwa liliombwa na Mbunge wa Kyela. Ndiyo maana hata Mwakipesile alizuiwa na Jeshi kulifungua!

- Huwezi kumshinda Mwakyembe kwa kusema aligombea ubunge (mwongozo na.13) kwa kumwogopa Mwandosya na Mwakyusa. Hoja hiyo ni ya kitoto na haiingii akilini kwa kuwa kila mtu, anayeishi Tanzania, anajua kuwa marafiki wakubwa wa Mwakyembe ni Mwandosya na Mwakyusa!

- Huwezi kumshinda Mwakyembe kwa kutunga ngonjera kwenye JF za kumtukana. Unapoteza muda, stick to issues man! Ndiyo maana mpaka leo jamaa hajakujibu wala kusema lolote kuhusu wewe. Amekuacha ujimalize mwenyewe!

Safari Njema!
 

Thanks mazee, kumbe ndo Kisa cha Kukimbilia Poland.....mwaga data kachokoza nyuki kwenye mzinga akitegemea mbio.....
 
Fataki,

Ujumbe wako umekaa kimashaka-mashaka.

Mwakalinga alimazia UDSM na utaratibu wa masomo wakati huo ni kuwa ilikuwa inabidi wanafunzi wa kilimo wahamie SUA - Morogoro. Na hapo akahamia SUA kama unavyoona kwenye historia yake na huko ndiko akaacha na kwenda zake Poland.

Hayo maelezo yako hapo juu ni USHAURI mzuri. Ila umetumia Mwongozo alioandika Mwakipesile (nina imani kambi ya Mwakyembe wameubadilisha kidogo ili uwe mtamu kwa wapinzani wa Mwakalinga) na kuutuma hapa. Sasa umeandika MANENO kibaoo wakati hayo Mwakalinga hajaandika wala hajaagiza waandike. Sasa hivi Wapinzani wa Mwakyembe wanajipa kazi ya kumpigia debe Mwakalinga, na hii si kuwa WANAMPENDA, la hasha. Wao wanataka kumuondoa Mwakyembe. Hata kama ungelikuwa wee FATAKI, basi wangelikupigia kura. Hata kama ni Lowassa au RA, bado wangelimpigia debe. Hilo lipo kama umeme unapopita, basi kunatokea Magnetic field. Au gari linapopita kwenye barabara za vumbi, vumbi hutimka.

Kama kweli wataka kumwandikia ushauri, basi soma jumbe zake za zamani, mfahamu ni mtu wa aina gani na hapo sasa muandikie ushauri wako. Kwa leo nakujibu kwa heshima sana msomi wetu.

NB: Kwa taarifa yako ni kuwa USHINDI wa Mwakyembe ulijumuisha msaada wa Mwakalinga. Mdogo wake Mwakalinga alikuwa na Mwakyembe from day 1 ya kampeni. Zaidi nikuambie kuwa Mwakyembe na Mwakaliga, wanafamiana zaidi ya unavyodhani. Sasa ukisikia Mwakipesile anamsaidia Mwakalinga, aliyesaidia kumtoa kwenye ubunge, INAINGIA AKILINI??
 

- Mkuu ninakusikia sana, ila I am looking forward kuona mijadala yenye masilahi kwa wananchi wa jimbo la Kyela, ninasubiri kusikia vision ya George, maana ya DK ninaifahamu tayari katika miaka kumi ya ubunge wake toka EAC, mpaka huko Kyela hasa zaidi taifa. Ninaiheshimu sana kazi yake kwa taifa letu, lakini lazima niwe mkweli sijui chochote kuhusu kazi yake jimboni, zaidi ya kuwaisikiliza sana hao maluteni wake, wawili.

- George, itafika wakati itabidi aseme kujibu maswali muhimu kwamba ni kwa nini anataka ubunge wa Kyela na sio jimbo lingine?, kwa nini anataka kumtoa mbunge shujaa wa taifa kama DK? kwa nini anafikiri anaweza kuwapelekea Kyela mazuri kuliko mbunge wao wa sasa? Je mbunge wa sasa amefanya mangapi mazuri na mangapi mabaya? Kama mbunge shujaa kama DK ameshindwa yeye atawezaje? Na maswali mengine mengi muhimu kwa taifa pia, ni majibu ya maswali kama haya ndio yatawasadiai wananchi Kyela na sisi wengine, kuliko hizi lows ninaziona humu.

- Kampeni hazijaanza, lakini hii tunaita part gazeti au trailer imeshaanza, na heshima kwa George kwa kuli-freeze taifa na JF for almost a week sasa, saafi sana na ataingia kwenye vitabu vya historia ya taifa kwa ujasiri wa kusimama na kusimamia principles. Ndio maana huko nyuma nilisema kwamba huu uchaguzi utakua wa Century na watakaofaidika ni wananchi wa Kyela hivi vichwa viwili vikitwangana.

- La George kuwa fisadi, bado ninalikataa sijaona sababu ya msingi, kama ni kukutana alianza kukutana na the right hand man wa DK, tena aliyemfuata London, silioni hili likipigiwa kelele hapa, Mwakipesile hamjui George, lakini yes ni adui namba moja wa DK, sheria haimzuii kumshabikia George na hata kumfanyia kampeni on his own ili kushindana na adui wake hilo linaeleweka, kwamba eti George anahusika directly na Mwakipesile au Lowassa, nimewauliza sana wale watu wa DK, ambao binafsi ninawaaminia sana inapokuja masuala ya kampeni za DK na George huko Kyela, infact mmojawao alinihakikishia kuwa George akimshinda mtu wake DK, basi yeye atahamia Malawi na kuomba uraia huko, now that is deep royalty kwa kiongozi, as opposed na hizi blah blah humu,

- Alisema alisikia kuwa George anajenga bara bara ya lami Kyela kwa kusaidiwa na mafisadi, hasa Lowassa lakini alikwenda haraka sana huko na kuhakikisha kwamba sio kweli, na nimamumini sana huyu aliyeniambia haya, sasa hawa wawili wakiniambia kwamba George ameanza kuwa fisadi basi wala sina sababu ya kumuuliza George kama ni kweli au uongo, hawa ni watu tunaheshimiana sana, so far wamesema mengi mazuri na mabaya ya George as a candidate wa jimbo lao, lakini la kushirikiana na mafisadi hawajalisema na ninawaamini sana hasa inapokuja interest ya uongozi wa
DK huko jimboni.

- Ushauri wangu kwa George, ni do not panic maana sasa umeingia siasa za taifa na hasa kwa kumgusa shujaaa wa taifa, haya ya JF ni madogo sana kulinganisha na ya mbele zaidi, hizi za JF ni za kawaida ingawa kuna mengine ni mazuri sana kwake kuyakariri, hasa ule ushauri wa Dilunga kwamba ifike time George ndiye awe the owner wa message yake na awe muangalifu sana na vibaka. Huna sababu yoyote ya kuhangaika kujibu hizi shutuma zisizo na kichwa wala miguu, be yourself watu ni watu tu maana ukiingalia vizuri sana hii thread utajionea mwenyewe some of the so called you "friends" wakivua ngozi zao rasmi, ndio maana hata viongozi wetu huteseka sana na siasa zetu Tanzania maana this is how we are, lakini yasikusumbue yachukulie kama changamoto.

Miwsho I am looking forward kuiona na binafsi kushiriki mijadala serious kwa ajili ya wananchi wa Kyela, pindi tu hizi blah blah zikiisha, zitaisha tu karibuni si unajua sisi wabongo na kipya kinyemi, soon tuta get down to serious business, otherwise ninamtakia safari njema kurudi "nyumbani" na pia ninamuombea sana kwa Mungu DK, amsalimishe na majaribu ya waovu wasiomtakia mema na ninawaombea sana wananchi wa Kyela kuwa waangalifu katika kutafakari hii situation, ambayo kama hawako makini itawaletea kimbembe sana, maana this thing is for real.

Mjadala mwema wananchi wenzangu wa JF, ila hapa ninaweka kalamu chini na huu mjadala. Na JF idumu where we dare! nafikiri hata George atajionea mwenyewe humu nyani alivyopigwa giladi, tena bila kumuangalia usoni ikiwa mchana kweupeee! I love JF!

Respect.

FMEs!
 
Thanks mazee, kumbe ndo Kisa cha Kukimbilia Poland.....mwaga data kachokoza nyuki kwenye mzinga akitegemea mbio....

Masa
Mwakalinga alisoma agricultural engineering..tafuta utaratibu wakati huo ilkuwaje,alimaliza UDSM na akaenda sokoine badaye akatimkia Poland
 
Ufisadi unaanza na fikra halafu vitendo. Ila huwezi kukataa kwamba wewe sio fisadi wakati tayari umesha anza kutumia fedha za kifisadi, na kama fedha hizo ndizo zinakupeleka dodoma then hilo ni zao la kifisadi linakwenda kutimiza wajibu wa mafisadi na kutetea mafisadi kusafisha mafisadi na kushiriki ufisadi. Tusitegemee mtoto wa chatu atakuwa kondoo.

Ukiangalia washiriki, washauri, na wale wote wapambe wa karibu wa huyu mmbunge wenu mtarajiwa ni wale mapapa wa ufisadi. Je kwenye ile pay back debt collection iliyoanzishwa uingereza kwa kufungua makampuni hewa yakijifanya yanaidai tanzania na kuiibia nchi fedha nyingi za kigeni watu wakishirikiana na kundi la mafisadi waliopo nchini ni wangapi walishiriki wakiwa ndani na nje ya nchi. Kweli ndoa hii yaweza kuvunjwa hasa pale wanapotaka kujenga kibanda???????????????

Ama kweli mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, basi na masikini aibiwe ila si mpaka kumvunjia kibanda chake .......
 
USHAURI WA BURE KWA MWAKALINGA:
Ndiyo maana mpaka leo jamaa hajakujibu wala kusema lolote kuhusu wewe. Amekuacha ujimalize mwenyewe!
Safari Njema
!

- Ahsante sana mkuu FATAKI, loud and clear kwa wenye masikio na macho kama mimi, duh Fataki bwana baabu kubwa!

Respect.

FMES!
 
kalengamab said:
6. Huko nyuma alipoona wana Kyela wanahangaika kwenye mikopo aliweza kuwashawishi PRIDE kutoka Tukuyu ili waje Kyela. Na mpaka leo PRIDE wanashukuru maana wamegundua soko la Kyela ni kubwa.
Sometimes the Best Man for the job is a Woman! Loh! jamani jamani, kalengamab kwa hoja hapo juu unanadisha, unauza au unamsiliba George aonekane mshirika wa makupe na wanyonyaji?!
 
Naomba mwongozo, hivi ni kweli Mwakalinga alienda Arusha-Munduli kukutana na Lowassa, na kama ni kweli je yeye ndiye kundi la hao ambao walimtuma?

Mimi si-kwamba nataka kumchafua Mwakalinga ila nachotaka ni kuweka mambo sawa na ku-vet mtu ambaye anafaa kwa ajili ya Tanzania na watanzania ambao tmekuwa tukilia na kuliwa urithi wetu na kundi dogo.

Ni ukweli kwamba kundi la mafisadi wamepanga kuingiza mamluki wao bungeni kwa ajili ya mambo yao.

sasa Mwakalinga tayari yupo karibu sana na hao mafisadi, ndio wanaomsaidia na ndio washauri wake. Kinachoniuma zaidi sote tumekuwa tukipiga kelele kuhusu hawa mafisadi na tukitaka wasulubiwe.

Sasa mizizi ya ufisadi imeota na imetapakaa kweli kweli. Ni lazima tuelezane ukweli mapema kwani tusipokata kizazi fisadi jitihada zetu zitakuwa za bure.

Mwakalinga njoo weka uhusiano wako na akina Lowasa na nini mlikubaliana Uingereza na huko Arusha. Je nia yao na yako nini, ni vingapi tayari mmeshirikiana kuliangamiza taifa la watu masikini, je fedha unazotumia kwenye kampeni sizo rasmi zimetoka wapi? Kumbuka ufisadi ni utashi na kama unao kwishnei.
 

Mkuu Sikonge,

asante kwa maelezo mazuri na asante kwa kunikaribisha. Nitakubali kutofautiana nawe kuwa lugha kama hiyo uliyotumia hapo ambayo kwa namna moja au nyingine unaengelea gender ya mtu kwa namna ya udhalilishaji (kikwapa cha msichana) sidhani kama inalingana na maandishi yanayosomeka kwenye moja ya threads hapo juu zilizo-stick.

Huwezi kuwa kwa upande mmoja unaomba watu kulichukulia jamvi hili siriasi lakini kwa wakati huo huo wewe ukiwa mmoja wa wale wanaolidhalilisha. Kama hiyo ndiyo njia mpya ya kuchangia hapa JF, basi nitaungana nawe kuendeleza jokes na utani na matusi muda mwingine ili kufurahisha baraza. Lakini kama nia ni kujenga forum yenye nguvu, basi lugha za udhalilishaji kama hizi sioni kama zinafaa kuendelezwa.

Nakubaliana kutofautiana nawe kwenye hili.
 

Hii Mkuu Sikonge,

Inabidi hapa nikubali kuwa unamfahamu sana huyu Mwakalinga. Nilikuwa naona kama unatania kwa kujitaja kuwa wewe ndiye Mwakalinga ila baada ya kusoma haya, imebidi nikubali kuwa mwenzangu unamfahamu vilivyo sana huyu ndugu. Ni vizuri sana kustick na mwenzako ambaye yaonekana unakila linalohitajika kwa ufahamu wa maisha yake ya shule na kikazi.
 
Fataki,
Mkuu shukran sana tena basi inabidi Mwakalinga akusome na akuelewe kwamba unamtakia mema na sii kinyume.. Kwa wanao kusoma vinginevyo ndio tunarudi kule kuleeeee - sisi Miafrika Ndivyo Tulivyo.
 
point tupu........
 
He he he.
Kweli wewe ni fataki.

Hayo madaraja saba ulijenga wewe?
 
MWAKYEMBE KUCHINJA NG'OMBE KILA KATA.

Mbunge wa Kyela Harison Mwakyembe kwa kushirikiana na jamaa zake wenye ufinyu wa mawazo Ally Kinanasi (Shemeji wa wilaya) na Emmanuel Mwamulinge (Kinundu) watapita kila kata huku wakichinja ng'ombe na kula na wananchi kwa lengo la kuubadili upepo mkali unaomkabili

Habari zilizotapatikana sasa hivi hapa mjini kyela zinasema, upepo sio mzuri tena kwa mheshimiwa huyo baada ya kukimbiwa na madiwani na watendaji wa kata karibia wote wakimtuhumu kwa tabia yake ya kusabisha migongano ndani ya chama na wilaya nzima ya kyela na hivyo maendeleo ya wilaya ya kyela kuzidi kushuka.

Mwakyembe kwa kushirikiana na Ally Kinanasi na Emanuel kinundu,watakuwa wanapita kila kata na kuchinja ng'ombe na huku mwakyembe akisimikwa upya kama chief wa kinyakyusa kwa kisingizio cha kwamba watu wanampa pole na ajali

Habari zinasema mwakyembe ameona upepo sio mzuri kwake na ameona aitumie nafsi ya ajali aliyopata kama kisingizio cha kusafisha jina lake.

Wapambe wa mwakyembe wamekuwa wakikutana kila siku usiku na kukaa kwa muda mrefu huku wakijipanga jinsi ya kununua hizo ngo'mbe kila kata.

Katika mkutano mkuu wa Halmashauri ya ccm wilayani kyela uliofanyika mapema mwaka huu kujadili vurugu, zilizopelekea kupigwa kwa Katibu wa ccm wilaya, Mwakyembe aliambiwa wazi wazi na madiwani kuwa hawamtaki na kama kunauwezakano ajuzuru. Ni mbunge wa kwanza kuambiwa na madiwani kwa kipindi kidogo alichoongoza.

Mwakyembe ana jina kubwa sana kitaifa, lakini hapa wilayani kapoteza dira na mwelekeo. Kikubwa sana ni ile tabia yake ya dharau na kusababisha migongano mingi sana ndani ya jamii ya kyela.
 
He he he.
Kweli wewe ni fataki.

Hayo amdaraja saba ulijenga wewe?

Yalijengwa Mwakyembe kwa kushirikiana na JWTZ(Gen. Mwamunyange)

Na ndio sababu ya Mwakipesile kususia kwenda kwenye ufunguzi wa madaraja hayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…