Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

Kwa mawazo yangu wanasiasa wetu wengi wako overqualified na elimu zao haziwasaidii kabisa.
Kwa kuongezea wasomi wengi ndiyo walioangusha taifa hili, bali ya elimu tunatakiwa tuwe na wazalendo hasa wenye nia nzuri na nchi yetu! Wakati mwingine huwa nahoji hawa wasomi wanasiasa mbona ni kama wako kwa ajili ya matumbo yao tu? Mifano unaijua sitaki kujaza thread hapa

Mas
 


Sikonge nilikuwa nakuona wa maana siku zote lakini tangu tuanze kumjadili rafiki yako Mwakalinga a.ka Mtanzania ndio nimegundua kwamba wewe ni *****.

Wanaume wa shoka mnatujua sana, mi nimezaliwa tu nikawa mwanajeshi hata depo la JWTZ sijaenda lakini nina cheo cha kanali, halafu wewe unazungumza utumbo hapa?

Najua hii inatokana na athari za wasomali na wairan mliochangamana nao huko kwenu sikonge, wameshawaharibu akili. Na sina shaka kabisa kwamba hizo mambo za kulegeza sauti ndio zenu wanaume wa kinyamwezi.
 

Balantanda,

Binafsi huwa nasoma posts zako na najua huwa unatoa hoja za maana. Sina tatizo kabisa na maandishi au hoja zako hapa JF hata kama ni kwenye mambo tunayotofautiana.

Hii thread haikuletwa na shabiki wa Mwakalinga, ililetwa na wanaompinga kwa lengo la kumpakazia. Hii imeletwa na Malafyale ambaye ni mtu wa karibu wa Dr. Mwakyembe na yuko maeneo karibu Houston. Huyu mzee hajui lolote kuhusu Kyela maana anaenda kama mtalii. Kuna articles zake nyingi kweli hapa zimejaa wrong information.

Bahati mbaya sisi hatukuwepo na hivyo kufanya habari nyingi za uwongo zisijibiwe on time.

Strategy iliyotumika ilikuwa kuleta watu wao hapa; wajifanye ni wapambe wa Mwakalinga kisha wanaendika habari za kumwangusha Mwakalinga. Ilifanikiwa mwanzoni kwasababu hakukuwa na mtu wa kukanusha.

Mwakalinga hategemei huruma yoyote toka members wa JF na in fact anaamini katika kumkoma nyani Giladi bila kumwangalia usoni. Lakini pia anaamini kwenye hoja zenye data badala ya uzushi.

Mfano ni hiyo ya Malafyale kusema Mwakalinga yuko Kyela anafanya vikao wakati ushahidi wote ukionyesha Mwakalinga wakati huo alikuwa Manyara na Ngorongoro. Au huyo jamaa anasema ametoka kumsindikiza Mwakalinga airport na kwamba alikuwa naye kwenye kampeni Kyela, kumbe ni huyo jamaa wa Yanga ambaye ndiye rafiki wa karibu kuliko wote wa Dr. Bahati nzuri tuliongea naye kwa simu na tukamdanganya kuhusu muda wa kuondoka Dar na yeye akafanya makosa yale yale ya muda. Njia ya mwongo ni fupi kweli kweli.

Nakuhakikishia kwa asilimia 100 kwamba hii thread haikuletwa hapa kumpandisha chati Mwakalinga bali kumshusha. Lakini kama ulivyosema mwenyewe kampeni si hapa JF bali ni kule Kyela na wananchi wa Kyela ndio wataamua.
 
kaaaazi kweli kweli!
FIRST LADY,
Ebu nenda katuwakilishe, maana wenzetu baado mnadai uhuru.

Watu wanaaghaika na kujikomboa na janga hili la umasikini, Mbunge mfalme anataka kutukuzwa kwa kuwa mtukufu kwa kubebwa kana kwamba hayo ndiyo walimchagulia wanakyela.

Kweli Wanakyela poleni sana, mmelamba grasha, huyo sio Mbunge ila ni kimeo hicho.
kgwamaka
 
Mkulima,

Walau umejibu kwa uwezo wako!



Sidhani kama Masters tatu zinakuwa equivalent na PhD hapa labda nipate msaada!

Kila laheri Mwakalinga

Masa
.

Mkuu mkulima,
Tatizo la Masanio ni ujinga alio nao.
Ana wivu wa kike na ujinga wa kitoto.wee mtu na elimu yake yote hiyo na uzoefu baado anawaambia wajinga wenzake eti George ana cv feki.

masanio,hakuna ataye kuunga ujinga wako.Sisi ni Mwakalinga tu.

Hongera sana mwakalinga na kila la kheri
 
Balantanda,
Kwa mara ya kwanza nimeona umejenga hoja nzuri na umenikumbusha mbali sana. kura ni Bujonde, Kilasilo, Nkuyu n.k na sio JF.

Na kama kuhitimisha mjadala basi wewe ume-winding up.

Tatizo humu wamemwanga hata watu ambao kwa mara ya kwanza wanaandika kwenye computer kisa Kumpaka matope Mwakalinga, lakini imekuwa kinyume na matarajio yao.
Ubunge wa Kyela utamuliwa na Wanakyela kwa merit za mtu, na sio vinginevyo. Nani kafanya hiki na nani anastahili kuwa mbunge wao na kwa sababu gani?
Tutapima matokeo ya mtu anayetaka ubunge na the best one's win.

Tatizo Wapambe wa Mwakyembe hawana hoja ya kuwaeleza wanaKyela mbunge wao miaka 4 hii amewafanyia nini wanakyela. Kama wapo hapa semeni. Watoto wanakosa madarasa ya kusomea, mbunge anajirebesha kwa maandamano huku akiwacheka wapiga kura wake, huyo kweli ana nia nzuri na Kyela? Lazima tumpige chini 2010

Sasa hivi wanajikanyaga kujaribu kujinusuru kwa kutumia neno fisadi wakati hata yeye Mwakyembe amewafisadi wanakyela kwa kubeba pesa za KDF na michango mabalimbali kwa manufaa yake binafsi, huku akianzisha mradi wa umeme Singida kwa pesa za walala hoi alizochukua kwa kuwadanganya.

Yana mwisho Rashid alisema (Kitabu cha KULI), 2010 hukumu yaje na atakuwa na mengi ya kujibu.
kgwamaka
 

Masanio,
Hapo tuko wote.
Kumbuka kuwa swala la kuongelea Elimu ulileta wewe na majibu yake ndiyo hayo hapo.

Asante Masanio na kumbuka kuwa ugomvi ambao ameuleta mwakyembe ki wilaya,ki mkoa na kitaifa unarudisha maendeleo nyuma.Hatumtaki.George Hoyee
 
Duh! Hatimaye Joji aka Mtanzania katinga tena ukumbini. Even Iddi Amin and Adolf Hitler had their supporters in thousands if not millions.
 

NYEPESI NYEPESI.

Wana ukumbi, leo nilipata kuongea na jamaa yake Mwakyembe, ndg Elias Mwanjala ambaye alikuwa mpiga kampeni mkubwa sana 2005 na alitumia pesa zake nyingi kumsaidia Mwakyembe kupata kiti hicho.

Elias anasema kuwa Mwakyembe amemfanyia mambo mabaya sana na baado anaendelea kumnyanyasa.

Anasema alipata nyumba ya National Housing Mikocheni na ndiko anakoishi, basi Mwakyembe alikwenda kumwambia Sitta ili wamnyang'anye ile nyumba.

Anasema naye Sitta akakubali azimio hilo na jamaa ameletewa notice ya kuondoka ile nyumba haraka kwa sababu hasizozijua, na alipofuatilia sana akapata habari kuwa hiyo nyumba anatakiwa kuhamia Sitta.

Anasema Mwakyembe amemwambia kuwa amesikia tetesi kuwa anamuunga mkono Mwakalinga na atamuonyesha lasivyo awaambie wapambe wake wampe kura yeye.

Elias amekimbilia Mahakamani kupinga hiyo notice ambayo haina sababu yoyote ya msingi zaidi ni uonevu tu.

Haya huyo ndiye mpinga ufisadi, haya ni zaidi ya ufisadi.

Kgwamaka
 

Hatimaye nimekupata mzee😀😀😀😀Asante kwa kuniondoa kwenye mataa. Nilikuwa gizani😀 Hata nilipouona mwanga nilikuwa nimebaki kizani. Sasa naona😀
 

Kwa hiyo Mwakyembe ndio aliiona nyumba kwanza halafu akaenda kumshtua Sitta "eeh bwana e, kuna nyumba hapa ya mjinga mmoja njoo tumtoe uhamie"? Ridiculous.

Shutuma za juu juu kama hizo ni weak mno kuaminiwa na baadhi yetu hapa JF. Huwezi kusema kwa kugusia gusia kwamba jamaa kapewa notice ya kionevu bila kusema kilichomo kwenye notice. Na huwezi kuanza kipande cha hadithi ya mahusiano mazuri kwenye campaign ghafla ukarukia kwamba Mwakyembe hampendi tena. Walifanyana nini hapo katikati, husemi. Mwakalinga kaja juzi tu kwenye picha. (Na sijui kama atakuwepo, kwa jinsi alivyo mishandle debut yake.)

Sitta anajengewa nyumba ya serikali as we speak, sio hiyo ya National Housing.

Mwakyembe na Sitta wana serious character issues na mapungufu ya kiuongozi lakini hii stori ni whacky.
 
..mpambano kati ya Mwakyembe vs Mwakalinga ungekuwa mzuri kama washabiki wange-stick to hoja na masuala yanayowaathiri wana Kyela.

..badala yake naona muda mwingi unatumika kushambuliana kwa mambo madogo-madogo yasiyo na maslahi kwa mwananchi wa kawaida wa Kyela.

..binafsi napenda kujua zaidi ya mpunga, Kyela kuna nini? kwasababu ipo siku huu mpunga wa Kyela unaweza kupata mshindani[rejea kuanguka kwa zao la karafuu] na hali ya kipato na maisha ikabadilika Kyela.

..napenda kujua wana Kyela wamefanya nini kuhakikisha kwamba wanaendelea kuwa "nambari one" ktk kilimo cha mpunga, kwa kuongeza uzalishaji per acre na vilevile kudhibiti ubora na viwango.

..pia wana Kyela, wakitumia rasilimali yao ya mpunga wamefanya nini kujiletea maendeleo ktk nyanja kama za ELIMU na AFYA?

..kuna masuala ya ukimwi ambayo yameathiri taifa zima kwa kiwango kikubwa kabisa. je, masuala ya elimu ya kujikinga na janga hili yakoje ktk wilaya ya Kyela?

..suala la mwisho ni UMOJA na MAELEWANO jimboni. je, wana Kyela wameridhika na jinsi hali ilivyo jimboni kwao? kwasababu bila mambo hayo mawili ni vigumu sana kwa eneo lolote lile kupiga hatua ya maendeleo.


..mjadala huu uwe-confined kuhusu nani kati ya Mwakyembe na Mwakalinga, kwa kushirikiana na wana Kyela wote, yuko ktk nafasi nzuri zaidi kuchochea maendeleo na kuboresha maisha ya wana Kyela.
 
..mjadala huu uwe-confined kuhusu nani kati ya Mwakyembe na Mwakalinga, kwa kushirikiana na wana Kyela wote, yuko ktk nafasi nzuri zaidi kuchochea maendeleo na kuboresha maisha ya wana Kyela.

Haya ni mawazo ya kinadharia kuliko hali halisi kisiasa. Uchaguzi haushindiki na kushindwa kwa misingi ya nani ana sifa bora zaidi pekee.

Ingekuwa hivyo labda Mwandosya na Salim Salim ndio wangekuwa marais. Lakini kwenye campaign kuna mengi. Salim Salim alipakwa matope na kambi ya Kikwete, akaonekana hafai. Mwandosya alionekana sio "kijana" na CCM stalwart kuliko Kikwete.

Tunapojadili Mwakyembe vs Mwakalinga lazima tuangalie mambo mengine ambayo yanaambatana na kampeni, campaign tactics, na pia jinsi mgombea anakavyojiuza, na kuuzwa na mwenzake, kupakwa matope etc.

Mwakyembe ni campaigner mzuri sana kwa standard za Tanzania, anaweza kuchota watu akili hata akiwa anaongea kwa matusi. Mwakalinga anaweza kuwa bora zaidi lakini Mwakyembe akamwangusha kwa sababu ya u-alwatan na sifa bandia, kambi ya Mwakalinga haiwezi kuyafungia macho haya, yanaweza kutokea. Yatatokea.
 

Dilunga,

..nilichoona mimi hapa ni kwamba mjadala mzima uligeuka kuwa a shouting match.

..Mwakyembe na Mwakalinga wamejitambulisha kama wasomi waliobobea.

..sasa tunaomba basi waendeshe kampeni zao kwa ustaarabu na kujenga hoja zenye maslahi kwa wana Kyela.

..of course mara nyingine kampeni za uchaguzi huingiliwa na matapeli na wajanja-wajanja, lakini hiyo isiwe kusingizio cha kukata tamaa na kuweka pembeni hoja na mambo ya msingi.
 
Hivi kwa nini wanasiasa wetu wanapenda sana ku tout academic credentials zao? Kwani zina uhusiano gani na kazi ya ubunge? Huyo Mwakyembe na PhD yake (kama anayo) amefanya nini huko jimboni mwake ambacho kilikuwa hakijawahi kufanyika? Ametengeneza ajira kwa kushawishi makampuni kwenda kuwekeza huko?
 
Kwi kwi kwi Mwaka 2010 Osama atakuwa Papa wa RC kule Roma, na kule Kyela Mwakalinga atakuwa Mbunge.....

Kwi kwi kwiii, nakubaliana na wewe. Hata Mtupe Paulo mapema alikuwa Malaika SAULI!!!
 
Hoja ya mwakalinga ni nini? anataka ulaji au uwakilishi. je kyela wamekosa maendeleo kwa sababu DR.mwakyembe ameshindwa kuwawakilisha?au kwa sababu CCM imeshindwa kutekeleza ahadi zake huko kyela? kama ni kwasababu DR.mwakyembe ameshindwa kuwawakilisha ili siamini sana.manaake amekuwa mstari wa mbele na wengi wanajua hilo. Kama ccm imeshindwa Kutekeleza ilani zake basi tutakuelewa sana mwakalinga ukijiunga upinzani. Vinginevyo unatumiwa na mafisadi na kwa hivyo na muunga mkono mchangiaji hapo juu, watu wasome nyaraka za kanisa wakukemee mbali.
 

Wee Mwita,
Hilo tusi ulilonitukana kimoyomoyo ***** nasema asante sana. Sijawahi kusifiwa kwa kupewa manyotanyota mengi namna hiyo.

Nilifahamu tangu mwanzo wee kijana wa miondoko ya Mombasa. Sauti lainii na kurembua macho "sasa kaka Mwakalinga, na mimi ntapata LAPUTOPU?". Ehhh Kaza sauti basi, unaongea kama Form one ambaye hajabarehe.
Usivyo na aibu unadhihirisha kabisa wee ni Mombasa line. Haya ya eti "TUNAKUJUA SANA", ebooo, mie simo. Mie namjua mke wangu tu hapa "cheupe dawa wangu, niliyelipa mang'ombe 35".
 

Eti cheupe dawa wako ulimlipia ngomba 35...acha urongo bana
 


Tuambie wewe unayejua, Kwanini Hamna maendeleo hayo uliyotaja huko Kyela?. Kama sio Dr tupe sababu basi mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…