Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

huyu silencer hana cha kufanya.....kwa hio ina maana mwakalinga na mwakyembe ndio officially wagombea wa kyela?
 
..hivi kila mwana Kyela anayem-challenge Dr.Mwakyembe lazima awe ametumwa na mafisadi?
 
Nimetokea kukuchukia Sikonge....nisamehe bure
 
Wiki jana kulikuwa na taarifa ya Mwakalinga kutangaza nia yake ya kugombea ubunge Kyela kupitia CCM. Dr. Mwakyembe ameingia msituni kujibu mapigo kwa kufuta nyayo za Mwakalinga kila alipopita na jana Dr. alikuwa katika kata ya Ipinda katika kile kinachoonekana kujibu mapigo, juzi alikuwa Kyela mjini na mikutano inaendelea katika kata zingine.

Dalili zinaonyesha patachimbika Kyela 2010 manake wana CCM wanaonekana wanataka mabadiliko lakini wananchi wanaona mbunge wao anastahili kupewa muda zaidi. Wapambe kama kawa wako siti za mbele na wakati wao wa kuvuna ni sasa.
 
Wameamua kuweka Jimbo lao wazi zaidi kwa Watz wote!

Ili iweje?

Maana hapa sioni kama kuna wapiga kura wa hilo Jimbo la Kyela, wengi wetu wanarusha makombora ya kuchafuana kwa sababu zao binafsi. Sasa sioni hata faida ya kuwepo hii thread.

Mambo yaliyoandikwa hapa unaweza kukuta 90% ni uzushi mtupu na hayawasaidii wahusika zaidi ya kuchafuana tu.

Kwa kuwa Mwakalinga ameishajulikana ni nani hapa ukumbini, tunaomba na Mwakyembe nae aweke wazi user ID yake ili tuanze kuchuja michango yao hapa na hoja zao. Vinginevyo hapa naona Mwakalinga anaonewa tu kwa kuwa ameishajulikana ni nani. Na wale chuki zao binafsi wanaweza kuwa wamepata mwanya wa kumpaka matope ili kumchafulia CV yake.
 

Mlalahoi,
Mwakyembe ni SHUJAA wa Taifa. Mwakyembe ni kama Kikwete wa Tanzania. Nchi za nje anafahamika na kupendwa na kuheshimika sana ila Watanzania tunafaidika nini na huo umaarufu wake. Kutusaidia kumuweka Hasheem Thabeet kwenye NBA? Kukutana na Obama kwanza? Kusuluhisha ugmvi wa Kenya na Zimbabwe?

Watanzania wanasota na maisha kila siku iendayo kwa Mungu. akina mama wanajifungulia kwenye makorido. What a mess.

Hivyo ndivyo ilivyo kwa Kyela. Mwakyembe na umaarufu wake kitaifa, Kyela hajafanya kitu cha maana. Wapambe wake wanasema kajenga daraja wakati JWTZ wanataka kuling'oa maana ni lao na Mwakyembe anatambia kuwa ni yeye kalijenga na wala hampi asante Mwamunyange. Kagombanisha au kugombana na watu wengi tu. Hata huyo Mwanjala na kumwita Mjomba, bado kakosana na kijana wake.

Mwakalinga yeye hadi leo hii anafanya vitu vyake. Ana duka, ukumbi wa mkutano, computer centre (mtu wa IT asiwe na hii, ingelikuwa aibu), hotel na takataka nyingine ambazo hadi sasa ziko zinajengwa. Na hivi karibuni atafungua Radio FM. Radio na miradi yote anaiita KYELA na si MWAKALINGA. Hizo zote zinatoa ajira kwa watu kibao kuanzia ujenzi wake hadi watumishi wa ndani.
Mwakalinga si FISADI. Mwakalinga si mfanya biashara. Ni mfanyakazi wa kampuni la HUAWEI huko UK. Mshahara wake sehemu kubwa kila mwezi huwa unaishia Kyela. Kwa uwezo na nyenzo yake ndogo kaweza kufanya hivi vitu na ana imani akipata UBUNGE ataweza kuwa na nguvu zaidi ya kidola ya kuwasaidia Wanakyela.

Wapambe wa Mwakyembe wameyaona mafanikio hayo. Hata Mwakipesile aliyaona na matokeo yake akaanza kuipiga vita Kyela Busness centre akifikiri Mwakalinga afanya hivyo ili agombee ubunge- Mwakalinga hakugombea. Mwakyembe pia aliposhinda, pamoja na kwamba familia ya Mwakalinga walimsaidia kwenye uchaguzi, pia na yeye akaanza kuwapiga vita. Lazarusmtindi alituambia kuwa wale vijana wanne walimpiga kiongozi mwenzao walikuwa wametumwa na Mwakalinga. Ulipofanyika uchunguzi, ikabidi Mwakyembe aombe msamaha kwani ndiye alisababisha huo ugomvi.

Hii thread tangu ianze, tumekuwa tukijibu mapigo tu bila ya kushambulia mtu. Ila nakuahidi kitu kimoja, kuna siku itafika hapo mwakani, na sisi tutaanza kushambulia. Leo hii ni zamu yenu. Pakeni na msilibe saana. Ohh, jamaa fisadi, ohh hajafanya kitu, ohhh hiki ohh kile. Dawa yatokota jikoni na ukifika muda tutaipakua na kuwawekea mezani. Tutawakumbusha watu nini Mwakyembe aliahidi na nini kafanya. Na tutaangalia Mwakalinga, nini ALIWAAHIDI na nini kafanya. Hapo wana Kyela wataamua na kutenganisha Pumba na Mchele. Vinginevyo hapa tunafurahisha genge maana wengi wao humu si wapiga kura.
 
Hili nalo ni neno mkuu!
 
Mwenye shati la Njano ni Masanilo aka Shalom ambaye nisecretary wa Engineer

Yaaaah shalom wa texas, na wazungu naleta msiwe na wasi wasi kabisa nilikuwa nasubiri pastor John Hagee Amalize series yake ya 7 gates of Jerusalem ili nimwombe aje kutusaidia na kyela maana naona ni wilaya inayoongoza kwa wajane!
 
Kuna kupigana kwa kisu ulichoenda nacho vitani lakini kisu chako mwenyewe kikakuondolea kichwa chako mwenyewe.

Iddi Amini alisemekana kuwa na silaha nzito na sophiscated zaidi ya zile wabongo walizoenda nazo, lakini kwa kukosa skills za wapiganaji wake wakajikuta wanaziacha silaha kwenye uwanja wa vita na wabongo wakaingia darasani kuzijua silaha zile na zikatumika kwa mafanikio kuwarudi wenye nazo. Penye miti mingi wajenzi ni wachache sana.

Kwa mfumo wa chaguzi za Bongo, kampeni ndio zimeshaanza, kipindi cha mavuno kwa walala hoi. Nyama choma na chupa fupi brown zitakuwa njenje. Mwenye mkono wenye asali atalambwa. lakini mwenye blabla ataishia kuangalia ze komedi origino. Kama hakuna mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi, walio nacho wataendelea kula kama wanajua kula na vipofu, lakini wadandiaji tutawasikiliza kama tunavyomsikia Bichuka bila kuathiri chochote.

Wapiga kura wa kweli wanataka kujua umejituma kwa kiasi gani kuwaonyesha wewe unawajali kwa vitendo, sio kuwaimbia utawafanyia watakapokuchagua. Fanya leo tukuone ili tukupe kiti ukikalie kwa raha zako. Kumtoa aliyekaa kwenye kiti sio rahisi vile, labda kiwekwe kipindi maalum cha kukalia kiti chochote cha siasa hata Ubunge. Watu husema zimwi likujualo halikuli likakwisha. Nitatupaje mbachao kwa msaala upitao? Bila shaka utawajibika kumpenda zaidi mkeo kuliko mimba yake, maana mkeo wamjua ati, mimba si mtatafuta nyingine? Kama kuokoa okoa mkeo basi sio kuua mkeo ili uiokoe mimba yake.

Leka.
 
malafyale tunajua umo kwenye timu ya kampeni ya mwakalinga ninyi nyote lazima muangukie pua tu nimeona mkutano wa mwakyembe hapo kyela juzi sio siri yeye ni moto mkali kwa mafisadi kama wewe na mwakalinga watu bado wana imani na mwakyembe hata akigombea kupitia chadema atashinda tu we need a smsrt person like him
 


Nahene Sezaye! Kila la heri katika mapambano haya,and all the best kwa Mwakalinga!
 

Hafai kuwa mbunge maana hatakuwa karibu na wananchi sababu ya ubusy wa shughuli zake hizo, aendelee kusaidia na kutoa ajira bila ya kuwa Mbunge!
 
Usibishane na Mpumbavu, maana watu hawataona TOFAUTI.
 
Point Masa!

Wazee wa texas


Mkuu sisi wazee wa COW BOYS huku Texas tutaendeleza mapambano hadi tone la mwisho mpiganaji Mwakyembe asiangushwe na Mafisadi! Ule mradi Tshirt na Kanga unaendelea vizuri...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…