Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

Sijaona waraka wa Mwakipesile, naomba jisaidie link yake maana sikuwepo wiki nne.

Lakini humtendei haki Mwakalinga kwa kuandika ninayosema yanafanana na ya Mwakipesile, kwanini isiwe Mwakipesile ndiye anaimba yale ambayo Mwakalinga anasema ameyafanya.

Moja ya chacteristics za mafisadi ni "denial". Sasa wewe unapo deny kuwa wewe si Geroge Mwakalinga tayari unaingia kwenye kundi la ufisadi hata kabla hujapata huo ubunge.
 
Mwakalinga acha utani, mbona unapitia mle mle .....kupeleka waalimu Kyela, Kuanzisha Open Uni kule ....are you serious? hujauona kwi kwi kwi

Atakwambia kuwa hakuwa hapa kwa wiki nne wakati alikuwa amejaa tele. Kilichochekesha kuliko vyote ni ile ya kuwa mhazini wa Tanzanet na baadaye kuwa mwanzilishi wa JF.

Inaonekana uanzilishi wake wa JF ndiyo hata umefanya hii thread itolewe kwenye jukwaa la siasa.

Ha ha hahaha.
 
ha ha ha ha, inabidi atangaze biashara zake za Kyela. Kama hazifiki bilioni moja basi ajue amekwishney.

Ha ha ha ha , sijawahi kuona pumba za mwanasiasa yoyote kama zile zilitoka kwa kambi ya Mwakalinga hapa jamvini. kuanzia laputopu hadi dola milioni moja?!

FMES alikuwa ameleta nyingine kuwa Mwakalinga anajenga barabara ya lami huko Kyela!

Usipoteze muda na hawa jamaa .......Dec naenda KYELA Xmas nitakuja na habari kamili na picha za vitega uchumi na habari za Mtanzania kule. Nitafikia kijiwe fulani kinaitwa Ipinda ila nitakuwa nalala Kyela town, Half London Guest House kama ni ya Mwakalinga itabidi nisepe...
 
Kilichochekesha kuliko vyote ni ile ya kuwa mhazini wa Tanzanet na baadaye kuwa mwanzilishi wa JF.

Heck...sijui katumia vigezo gani kujiita yeye ni mwanzilishi wa JF....lakini hata mimi ninaweza ku claim uanzilishi wa JF kwani niko hapa tokea izaliwe...so I guess na mimi nikagombee ubunge kwetu Bariadi...
 
Moja ya chacteristics za mafisadi ni "denial". Sasa wewe unapo deny kuwa wewe si Geroge Mwakalinga tayari unaingia kwenye kundi la ufisadi hata kabla hujapata huo ubunge.

Mungu wangu baba wa Mbinguni Msamehe George hajui alitendalo! Omega Psi Phi tuli pamopene !
 
Niwapeni mchapo mwingine, mujue siasa za Kyela zilipofikia.

Kama mnakumbuka kuna katibu wa CCM wa wilaya alipigwa na vijana baada ya kuwatuhumu kwamba wamehongwa pesa na Mwakalinga kupitia kwa diwani Mahenge (diwani wa Kyela mjini).

Kuna kiongozi mmoja wa chama wa wilaya aliongea na Mwakalinga kwa simu na kumtuhumu kuhusika na hizo vurugu. Mwakalinga akasema yeye hahusiki na wala hawajui hao vijana na pia yeye sio mtu wa kuchochea vurugu na badala yake anaheshimu kutofautiana kwa hoja. Wakashindana hapo, nafikiri huyo kiongozi aliendelea kuamini hivyo.

Sasa juzi, Mwakalinga alikuwa anatoka kijijini kwao, kuja mjini. Diwani Mahenge akawa anaenda kijiji hicho kwenda kukutana na wazazi (yeye pia ni mwenyekiti wa jumuia ya wazazi).

Kijana tuliyekuwa naye kwenye gari letu akasema lile pale mbele ni gari la Mahenge. Ikabidi tusimame na Mwakalinga akateremka. Kwenye gari la Mahenge kulikuwa na watu wawili, aliyekuwa anaendesha gari alikuwa amevaa tisheti na mwingine alikuwa amevaa nguo za CCM.

Mwakalinga bila kujua akaenda kumsalimia yule aliyekuwa amevaa nguo za CCM akidhani ndiye diwani Mahenge. Yule jamaa akasema hapana sio mimi na diwani Mahenge ni huyu, akimwonyesha aliyekuwa amevaa tisheti. Ikabidi Mwakalinga aombe msamaha sana kwa makosa hayo. Mahenge akasema hakuna tatizo.

Kumbe Mahenge akawa amefurahi sana; huyo jamaa aliyekuwa naye kumbe alikuwa katika watu waliokuwa wanasema Mahenge amekutana na Mwakalinga kwa siri mwezi March 2009 na kupewa pesa ambazo zimechangwa na mafisadi. Walipoondoka tu yule jamaa akawa wa kwanza kuomba msamaha na kusema Majungu ya Kyela yamenishinda yaani kumbe wewe ulikuwa hufahamiani na Mwakalinga?

Baadaye hata kiongozi wa CCM ambaye huko nyuma alimtuhumu Mwakalinga akatupigia simu na kuomba msamaha pia. Mwakalinga akamwambia akitaka aangalia hata passport maana Mwakalinga alikuwa TZ mara ya mwisho January 2008.

Hiyo habari ilienea Kyela kwa muda mfupi sana, watu wakaanza kusema wameumbuka kwa uzushi.
 
Heck...sijui katumia vigezo gani kujiita yeye ni mwanzilishi wa JF....lakini hata mimi ninaweza ku claim uanzilishi wa JF kwani niko hapa tokea izaliwe...so I guess na mimi nikagombee ubunge kwetu Bariadi...

Toa vitega uchumi vyako kule!
 
...so I guess na mimi nikagombee ubunge kwetu Bariadi...

Hehehe wewe komredi utawapelekea nini wananchi wa kule majembe ya ng'ombe au? Maana laptop huwezi gawa kule akina Ngosha hawatakuelewa.
 
Hehehe wewe komredi utawapelekea nini wananchi wa kule majembe ya ng'ombe au? Maana laptop huwezi gawa kule akina Ngosha hawatakuelewa.

Labda nitapeleka magirigita (matrekta) ya John Deere au Massey Ferguson...Lol
 
Atakwambia kuwa hakuwa hapa kwa wiki nne wakati alikuwa amejaa tele. Kilichochekesha kuliko vyote ni ile ya kuwa mhazini wa Tanzanet na baadaye kuwa mwanzilishi wa JF.

Inaonekana uanzilishi wake wa JF ndiyo hata umefanya hii thread itolewe kwenye jukwaa la siasa.

Ha ha hahaha.

Mwafrika,

Humtendei haki Mwakalinga maana unarudia jambo lile lile ambalo mimi kwa niaba yake nimelitolea maelezo huko nyuma.

Mwakalinga hakusema ni mwanzilishi wa JF na hata context ambayo JF ilitajwa ilikuwa tofauti kabisa.

Msiwe mnapotosha watu bila sababu zozote.
 
Mwakalinga alikuwa anatoka kijijini kwao, kuja mjini. Diwani Mahenge akawa anaenda kijiji hicho kwenda kukutana na wazazi (yeye pia ni mwenyekiti wa jumuia ya wazazi).

Kijana tuliyekuwa naye kwenye gari letu akasema lile pale mbele ni gari la Mahenge. Ikabidi tusimame na Mwakalinga akateremka. Kwenye gari la Mahenge kulikuwa na watu wawili, aliyekuwa anaendesha gari alikuwa amevaa tisheti na mwingine alikuwa amevaa nguo za CCM.

Utwa pamusi Mwakalinga?
 
Mwafrika,

Humtendei haki Mwakalinga maana unarudia jambo lile lile ambalo mimi kwa niaba yake nimelitolea maelezo huko nyuma.

Mwakalinga hakusema ni mwanzilishi wa JF na hata context ambayo JF ilitajwa ilikuwa tofauti kabisa.

Msiwe mnapotosha watu bila sababu zozote.

Mtanzania,

mpaka Mwakalinga mwenyewe aje hapa kukanusha hizi habari (maana wewe umekataa kuwa sio Mwakalinga), basi utetezi wako utachukuliwa kama habari original inavyochukuliwa.

Kwa sasa wewe hauna credibility zaidi ya aliyesema kuwa Mwakalinga ni mwanzilishi wa JF (kama kweli wewe sio Mwakalinga mwenyewe).
 
Komredi umenipa wazo zuri sana....stay tuned! Naenda kum challenge fisadi Chenge....

Hahahaha komredi hapo umelamba dume lakini kumbuka yeye alichinja ng'ombe juzi kati karibia kila kijiji alicho simama.
 
Hahahaha komredi hapo umelamba dume lakini kumbuka yeye alichinja ng'ombe juzi kati karibia kila kijiji alicho simama.

Mimi nitaenda juu zaidi na kuchinja ng'ombe na beberu kila kijiji....
 
MWAKALINGA AFUATWA NA PCCB KYELA:

Basi wenzenu tulitumiwa mpaka na PCCB kwamba eti tumeanza kampeni mapema na tunahonga wananchi. Wakatusimamisha njiani, kagua gari, wakakuta tu Mwakalinga na Diary yake ikiwa imeandikwa tunataka maendeleo zaidi sio maandamano zaidi.

Wakasema walipewa habari kwamba sisi tunahonga wananchi na tumejaza pesa kwenye gari letu na kwamba ilibidi wachukue hatua maana ndio kazi yao.
 
Back
Top Bottom