Kyerwa, Kagera: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa agoma kufungua ofisi ya TANESCO kutokana na gharama kutoendana na ujenzi uliofanyika

Lakini tulishakubaliana Mama alete pesa mtaani kwa njia yoyote ile! Subiri na posho za Watumishi walio safiri na Mama kutoka US wakirudi nazo zitamwagikaa mtaani!!

Tushiriki tuu kwenye ku enjoy nchi kila mmoja,
 
Pesa kama hiyo imejenga jengo kubwa kabisa la akina mama hospitali ya wilaya Nachingwea. Ikiwa na facilities

hapa TANESCO wamechemka

kwa mfano kile kibanda cha mlinzi kusema ni milon 7 hapana

au jengo la stoo milion 50 hapana kwa kweli.

tujaribu kuwa na uchungu kidogo na umaskini wa nchi yetu.
 
Alafu ujenzi wa serikali una formalities ngumu zonazoongeza cost. Hapo alitafutwa Mkandarasi, mchoro ulitolewa kwa zabuni, viongozi kukagua kila hatua au consultant n.k
Wao wana telezaa na force account, lkn sasa bado materials ni bei ghali.

Hao wanao shangaa huenda ikawa hawafuatilii ujenzi wa sasa.

Ukianza kuangalia bati za icho kibanda not less than 2.5 M.

Ujija ktk rangi izo not less than 900K.

Ukija ktk mbao not less than 2M.

Njoo ktk cement sasa hapo ndipo utasaga meno na kilio ,njoo ktk finishing izo dirisha alluminium not less than 3 M binafsi nakubaliana na izo gharama za 7 M kwa icho kibanda frankly speaking vifaa vya ujenzi gharama zime shoot sanaa
 
Yaani ukiona gharama za kununua umeme ukiongezeka jua ni upigaji umeongezeka sio maendeleo...
Nawapongeza sana hao waliohusika hapo!

Kama kina Ruge wamefisadi mabilioni lakini wanachiwa na watu tunashangilia kwamba walionewa, kwanini wengine wasifisadi?

Mtu yeyote mwenye nafasi kula sepa.
 
Wao wana telezaa na force account, lkn sasa bado materials ni bei ghalii. Hao wanao shangaa huenda ikawa hawafuatilii ujenzi wa sasa...
Bati za hiko kibanda ni mil 2.5?? Acha hizo aisee. Alaf bati za migongo mipana ni 38000 kwa gage 30, na gage 28 ni 42000
Kwa gage 28 hiyo mil 2.5 ni sawa na bati 60.

Sasa mkuu kweli hiko kibanda kimechukua bati 60?? Hiko kibanda kimechukua bati 8 tu, sawa na 336000 tu, Watanzania tuna shida Sana, mtu anajaribu kutetea wizi wa wazi kabisa.
 
Binafsi naweza nikasema ni sawa kwa kile kibanda cha M7 kwa sababu
Gharama za ujenzi sass ivi zipo juu mnoo
Kama una experience ya ujenzi wa sasa utaelewa tub
Acha uongo na ujinga. Mimi ni mkandarasi niliyeshindikana.

Nimefanya kazi nyingi za kujenga shule za serikali na hata sasa nafanya.

Hiko kibanda tukiweka pamoja na Cha juu tunaweka mil 3.5. Hii ni kwa Sasa, hapo kabla vitu havijapanda tuliweka mil 2.5.

Hapo ni pamoja na Cha juu kwa wale viherehere.
 
Gharama za kawaida sana, nashangaa wanaoona eti gharama ni kubwa, hao wanaoona gaharam nu kubwa wao wanajengewa na sio wanajenga wenyewe kwa fedha zao.
Hebu twende taratibu kwenye hili. Mimi ni contractor na bado hadi sasa nafanya kazi za kujenga shule.
Hizo gharama ni kubwa, hiyo pesa iliyotajwa hapo ndio huwa tunalipwa kujenga zahanati ya kisasa yenye miundombinu yote. Jengo la ward, maabara, mortuary, corridors, ukuta n.k
 
Mchanganuo wa gharama zilizotumika kujenga ofisi ya TANESCO Wilaya ya Kyerwa, Kagera (TZS):

1. Chumba cha walinzi: Milioni 7 (PICHANI)

2. Uzio: Milioni 94.2

3. Jengo la ofisi: Milioni 253.8

4. Stoo: Milioni 51.55.
 
Usanii huu tena wa hali ya juu. Hadi hii leo hajasema chochote kuhusu ripoti ya CAG Kichere iliyojaa wizi, ufisadi na ubadhirifu wa trillions lakini kaamua kufanya usanii kwa milioni!!!!

Hii ndio nchi yetu ambayo inajali wananchi na kuwasogezea huduma. Hili ni jengo la Tanesco lenye thamani ya
 
Mkurugenzi wa Tanesco ndiye shida na siyo vinginevya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…