Labda unahitaji kuongeza ujasiri kidogo tu ili upande viwango vya juu zaidi!

Labda unahitaji kuongeza ujasiri kidogo tu ili upande viwango vya juu zaidi!

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Sina uhakika kama Kikwete alikuwa na ndoto ya kuja kuwa Rais wa Tanzania. Mwinyi alipomteua kuwa Mbunge na Waziri, alimfuata na kumwomba amwondolee uwaziri amwachie ubunge. Badala ya Mwinyi kulipokea ombi lake, alimtia moyo kwamba yeye ni kijana mwenye akili hivyo ataimudu hiyo nafasi. Kilichofuatia baada ya miaka kadhaa ni Historia.

Samia alipoitwa Ikulu ya Zanzibar kujulishwa kuwa kateuliwa kuwa Waziri, alishtuka sana. Hakuwa na uhakika wa kuyamudu hayo majukumu.

Kwa nafasi aliyo nayo sasa huhitaji kujiuliza kama aliyaweza majukumu ya uwaziri au la!

Ali Hassan Mwinyi alihudhuria mkutano mkuu wa CCM mwaka 1984 kama wajumbe wengine, lakini alirejea Zanzibar akiwa na "jina" jipya, Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar.

Vipi akina Lusinde na Msukuma? Japo wana Elimu ndogo, lakini wameweza kuwashawishi wananchi wao kuwachagua kuwa wawakilishi wao bungeni.

Unajifunza nini kwa hiyo mifano? Unaowaona wapo juu wanaweza wakawa hawajakuzidi akili, na huenda, hata majukumu wanayoyafanya wewe ungeyamudu vizuri zaidi kuwazidi. Kilichowatofautisha wao na wewe ni kitu kimoja tu, ujasiri.

Walithubutu, japo inawezekana ni kwa kujaribu, na wakaishia kuwa hivyo walivyo sasa.

Na wewe unaweza kuthubutu kufanya lile ulitamanilo na likaishia kuwa kweli.

Ongeza ujasiri kidogo tu uone kitakachotokea.
 
wapo wengine walithubutu na kuongeza ujasiri kilichowakuta wengine hawaongei ila ni wazima na wengine hawatikisiki!.. ujasiri uendane na akili.
 
wapo wengine walithubutu na kuongeza ujasiri kilichowakuta wengine hawaongei ila ni wazima na wengine hawatikisiki!.. ujasiri uendane na akili.
Naam, ujasiri uwe katika mambo ambayo mtu ana uelewa nayo.

Si busara dereva wa mabasi kujaribu kuiendesha ndege bila mafunzo. Lakini ni sahihi Mwalimu wa shule ya msi msingi kujitosa kwenye kinyang'anyiro cha ubunge hata kama hajawahi kuwa balozi wa nyumba kumi. Akiwa na ujasiri katika kuwania hiyo nafasi, atayajua yampasayo mbele ya safari.
 
Sina uhakika kama Kikwete alikuwa na ndoto ya kuja kuwa Rais wa Tanzania. Mwinyi alipomteua kuwa Mbunge na Waziri, alimfuata na kumwomba amwondolee uwaziri amwachie ubunge. Badala ya Mwinyi kulipokea ombi lake, alimtia moyo kwamba yeye ni kijana mwenye akili hivyo ataimudu hiyo nafasi. Kilichofuatia baada ya miaka kadhaa ni Historia.

Samia alipoitwa Ikulu ya Zanzibar kujulishwa kuwa kateuliwa kuwa Waziri, alishtuka sana. Hakuwa na uhakika wa kuyamudu hayo majukumu.

Kwa nafasi aliyo nayo sasa huhitaji kujiuliza kama aliyaweza majukumu ya uwaziri au la!

Ali Hassan Mwinyi alihudhuria mkutano mkuu wa CCM mwaka 1984 kama wajumbe wengine, lakini alirejea Zanzibar akiwa na "jina" jipya, Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar.

Vipi akina Lusinde na Msukuma? Japo wana Elimu ndogo, lakini wameweza kuwashawishi wananchi wao kuwachagua kuwa wawakilishi wao bungeni.

Unajifunza nini kwa hiyo mifano? Unaowaona wapo juu wanaweza wakawa hawajakuzidi akili, na huenda, hata majukumu wanayoyafanya wewe ungeyamudu vizuri zaidi kuwazidi. Kilichowatofautisha wao na wewe ni kitu kimoja tu, ujasiri.

Walithubutu, japo inawezekana ni kwa kujaribu, na wakaishia kuwa hivyo walivyo sasa.

Na wewe unaweza kuthubutu kufanya lile ulitamanilo na likaishia kuwa kweli.

Ongeza ujasiri kidogo tu uone kitakachotokea.
Vipi kuhusu magu?....,kama naelewa hv?......ila hata messi......lakin vp kuhusu bob.....ila hata jamaa wa tozo.....eeeh kuna kolomije.....bas ata mi naweza🤔
 
When you talk everday about politics how is gonna going to help you?mr thread writer politics is just a dirty game just leave your life ya NGOSWE MWACHIE NGOSWE WRITTEN BY EDWIN SEMZABA RIP
 
Kuna mapacha wasiofanana...waliongeza ujasiri na kuthubutu...ghafla mama yao akawatoa kwenye uongozi
 
Back
Top Bottom