Ladies understand your men (Wadada tu, wanaume marufuku)


Ndio maana nimeeleza sana kuwa wadada wanatakiwa kuwa makini na mbayu wayu......

Lazima mtu awe na vigezo vyake na njia zake za kumwezesha kupima kama abiria wake anashuka kituo kinachofuata au ni mtu wa masafa marefu. Vinginevyo simulizi kama hiyo ya mjukuu wangu Kokutona zitakuwa kama bongo flava!!
 
mpendwa nilifikiri namba yako ni ile ile kumbe umebadili maana nilikupigia sijakupata! Ndio nini kubadili badili namba? Nitumie hiyo mpya. Halafu post yako ya mwanzo kama umesikitika vile. Hebu funguka kidogo.

Ni ile ile mpendwa wangu labda network ilikuwa inazingua! Mengi yameshaongelewa, na ulichokiandika hapo ni kweli kabisa!!! Kuna watu wanasema mapenzi hayana fomulae(fine).........ila mapenzi yasimfanye mtu kuwa mpumbavu au mzembe kiasi cha kushindwa kusoma hata alama za nyakati ilihali dalili zote zinaonekana kabisa! Kwa mdada makini na mwenye determination na future yake lazima awe makini na achukue tahadhali sio kila siku ni kutoa tunda alafu mwenzako anapotea.....then anarudi tena kwa ajili ya tunda, sasa hapo utahesabu una mtarajiwa kweli??? Mpenzi anakutishia kukuacha kwa sababu hujampa tunda, basi kwa kutofikiri nawe unatoa eti unahofia kukimbiwa.......does it make sense kweli??? Kila siku unayoenda kumtembelea wewe ni wakupelekwa gest tu au kwenye geto la wenzake, jiulize huko kwake kunani??? Lol......uandishi wangu wa mwanzo usikustue sana, ni kweli......today am not feeling well my dear!!
 
Ni kweli hakuna recipe ambayo inaweza kuwagusa watu wote...Ila zipo ambazo zinawagusa wengi...Kama una idea ya kitu kinaitwa normal distribution, basi utakubaliana nami kwamba mawazo ya Hus yanawagusa wengi....Pia soma ushuhuda wa Kokutona!!

babu unanidai kikombe cha kahawa. Lol.
 

Mkuu,

Michango mingi kwenye uzi huu haikubaliani na wewe.....Mwanamume ni donor .....kama huwezi kutoa mafweza na mazawadi basi pole sana....Kwa hapa MMU, sample size yako itakuwa kama vile haipo!!
 
pole bila ushauri?mwambie Rejao akupe desa!

ooh! Nilikosea, namshauri kokutona atakapotaka kuanza mahusiano mapya amsome kwanza mwenza wake kwa vigezo vyake binafsi na hivyo nilivyomuongezea. Kama anaanzisha mahusiano ya kupeana mautamu tu haina haja ya kufatilia chochote. Una la ziada?
 
ngoja nitafute dikshenare.
 
Na huku upo
naona mabinti wanashauriana mambo yao
hapa nikichangia ntaharibu hali ya hewa tu
sababu haya mambo bwana hayanaga fomula
we mwaga tu sera bana,au ushakaa kaunta dragon? Nakuja ngoja nimuage Husn.
 

kwanza pole kipipi. Tutaongea mengineyo pembeni. Pili ni kweli uliyosema, hakuna anayeishi kwa formular kwamba jana iwe sawa na leo na kesho. Hapo kwenye kushindwa kusoma alama za nyakati ndo huwa nawashangaa wadada! Unakuta mdada kuna kila dalili anaoneshwa kuwa haitajiki lakini anataka hadi atamkiwe. Khaaaa!
 
Mkuu,

Michango mingi kwenye uzi huu haikubaliani na wewe.....Mwanamume ni donor .....kama huwezi kutoa mafweza na mazawadi basi pole sana....Kwa hapa MMU, sample size yako itakuwa kama vile haipo!!

Ni kweli kabisa unachosema. Na sidhani kama hata kuna ambao wameelewa nilichoandika. Licha ya hivyo, ndoa ni partnership. Inahusisha watu wawili katika hali na mazingira yote - shida na raha, milima na mabonde, road bumps, na kadhalika.

Ni imani yangu kuwa ushirikiano unaimarisha ndoa (mahusiano). Ushirikiano unaifanya ndoa iwe na upendo. Kwa hiyo hii dhana ya kwamba mwanaume ndiyo mtoaji na mwanamke ndiyo mpokeaji mimi naikataa kabisa. Imepitwa na wakati.

Lakini kwa vile ndoa huhusisha watu wawili (yeah, wakati mwingine zaidi ya wawili), I am all for couples defining their own roles in their own marriage/ relationship. Imposing my values on others is just not my shtick.

Au wewe unaonaje kaka? Nimepotoka?
 

Koku pole sana. I have a very simple question for u.....umetoka ukakutana na jamaa mkazimikiana(sort of)mkabadilishan no za cm mkaanza mawasiliano. Siku ya siku jamaa akakwambia anakutamani toka alipokuona siku ya kwanza na angependa mkale tunda lkn baada ya hapo no strings attached! Je,ww Koku utakubali??? Tatizo letu kubwa wanawake(sio wote) tukiambiwa UKWELI inatusumbua sanaaa na hatutaki kuukubali,ndo mana wanaume nao wanaona bora watudanganye tu.
 
Mie umeniwekea "speed governor":

"Thread hii ni maalum kwa wadada hasa waliopo kwenye mahusiano ila bado hawajaolewa..."

Nilipita kusalimia tu, lakini nipo nawachungulia tu, mambo mazito haya mie yamenizidi kimo.
FaizaFoxy,naomba tuwe marafiki!
 

Hus,

Mwakani utafute nafasi pia, uwashauri wajukuu zangu ambao wameshusha thamani matunda yao na kuyatumia kukamatia kila kitu hadi kunguru!!
 
which begs a question Koku,huwezi kuwa rafiki na mtu mpaka mvalishane pete?

Inawezekana Bishanga, but inategemea na makubaliano yenu ya awali i mean alikuahidi nini na alikupa matumaini gani kuhusu ndoa. Hata hvyo nimejifunza, ndoa kwangu siyo ishu tena. Natafuta chapaa i mean pesa. Kwenye moyo wangu haku nafasi tena kwa kiumbe ME. wAMENITENDA
 
Hus,

Mwakani utafute nafasi pia, uwashauri wajukuu zangu ambao wameshusha thamani matunda yao na kuyatumia kukamatia kila kitu hadi kunguru!!

hahahahahaha! Ombi la babu liheshimiwe. Nitafanya hiyo kazi. Matunda lazma yatunzwe. Au sio?
 

Kweli mkuu,

Ila hapa watu wanaongelea kipindi cha kutamanishana hadi mtu akaribia kupelekwa ICU kwa sababu ya hamu!!

Hata hivyo, wakishakuwa kwenye game yenyewe...duu mambo ni tofauti kabisa.....Ma theory yote yanakufa na baada ya muda si mrefu watu wanaanza kuziona rangi halisi za rainbow badala kuona pink tu na mawenge wenge mengine.

Kwa watafutaji....wanayoyasema yako sawa kwa asilimia nyingi sana...!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…