Lady Jaydee, Mwana Fa, Juma Nature walikosea wapi enzi zao kutotawala Afrika kama Diamond Platnumz?

Lady Jaydee, Mwana Fa, Juma Nature walikosea wapi enzi zao kutotawala Afrika kama Diamond Platnumz?

Siku hizi watu wanateleza wanataka kujidanganya ni uwezo wao! Wanasahau miaka 50 iliyopita pia tulikuwa na wanamuziki wakali lakini na wenyewe walikuwa wanaishia Kenya!

So, upo sahii kabisa! Ni mjinga tu ndie anaweza kupinga mchango mkubwa wa Diamond ktk kuivusha Bongo Flavor nje ya East Africa.
Yap c unajua tena kuna watu naturally wamezaliwa kupinga tu kila kitu, hata kama kitu kinajionyesha dhahiri kwa macho.hapo ndipo tunasema "usimjibu mpumbavu sawa na upumbavu wake, usije ukafanana nae".
 
Watu wanataja habari za media na social networks! Wanachosahau ni kwamba media na social networks zinatengeneza mazingira sawa Afrika mzima!

Kuna wasanii kibao wa South Africa na Nigeria walikuwa wanafahamika Afrika mzima... wao walikuwa wanatumia FB, Instagram? Twitter?! Jibu HAPANA na kwahiyo social networks ni nyenzo tu! Afrika kote tulikuwa tunategemea radio, TV na magazeti lakini bado wasanii wa Naija & SA walikuwa juu!

Timu ya Diamond ipo very strategic. Kwanza walifahamu muziki wa Tanzania ulikuwa unaishia Kenya; PERIOD. Tanzania kama nchi nayo haikuwa maarufu kwa chochote miongoni mwa watu wa kawaida Afrika! Kwahiyo no body paid attention kwa kinachotokea TZ!

So, collabo za Diamond vs Nigeria & South Africa ndizo zimemfanya atambulike Afrika na hatimae kuitambulisha Bongo Flavor nje ya TZ & Kenya.

Kwa nchi kama Tanzania ingekuwa ngumu sana kupenya Nigeria au hata SA bila ya collabo na hit makers wa huko kwa sababu muziki wetu ulikuwa haufahamiki!

Nigeria ndiyo Marekani ya Afrika na SA ni kama UK linapokuja suala la tasnia ya burudani! Nyimbo zako zikishaanza kuchezwa Nigeria hesabu zitachezwa kote kusini mwa Sahara.

AY alifanya kosa la kimkakati! Alianza kutaka kufahamika US wakati hata Botswana alikuwa hafahamiki! US hakuingiliki kirahisi unless USHIRIKISHWE na hit makers wa huko(sio KUSHIRIKISHA)!

So, siri ni collabo! Ni collabo za Diamond ndio zimetambulisha Bongo Flavor nje ya East Africa na wengine hivi sasa wananufaika na hustle zake. Ajabu ni pale hata baadhi ya wasanii wenyewe wanapojaribu kumponda Diamond kwa kufanya collabo!

Hawa wanasahau kama sio hizi hustle za Diamond probably hadi kesho ingekuwa wanaishia Kenya tu hapo... sana sana Rwanda!
Mi nadhani tatizo kubwa ilikuwa ni strategies tu manaake kama ni collabo wapo wasanii walianza collabo mapema ila hazikuleta matokeo chanya.

Kwa mfano AY sio kwamba alianza collabo yake kubwa US moja kwa moja hapana. Kama una kumbukumbu mkuu kati ya mwaka 2007~08 alifanya collabo na P~Square ngoma ilikuwa inaitwa 'Fresh' by that time p~Square ndio walikuwa on fire na walikuwa wamefanikiwa kuliteka soko la Africa vizuri.

So kikubwa nadhani ilikuwa ni mpango mkakati lakini pia tusi~under rate nguvu ya social networks. Collabo ya AY na Sean Kingston wa US ni ya juzi sana mwaka 2012 au 2013 kama sijakosea lakini pia tukumbuke wasanii kama akina Juma Nature, Jide, Babuu (Inspector), akina Solo Thang et al hawakufanikiwa kutusua sababu kubwa pia ikiwa ni wadau wa muziki kuwanyonya.

Wasanii kwa mfano walifanya kazi kubwa na nzuri infact nyingi zenye kuelimisha ila waliokuwa wanajiita ma~promoter waliwanyonya sana wasanii na kuwakatisha tamaa baadhi ya wasanii wenyewe.

Lakini pia sumu kubwa iliyowadumaza wasanii wetu wengi nadhani ni ulimbukeni na kuiga starehe za kijinga baada ya kufanikiwa kupata vijisenti vyao kidogo. Kwa mfano baada ya msanii kutoa hit song akapata pesa badala ya kujipanga kuendelea kutoa ngoma juu ya ngoma wengi walikimbilia starehe, anasa na kuishia kuwa mateja.

Angalia watu kama akina Ferooz album ya yake ya safari na hit songs kama boss, au starehe zilimfanya akapiga hela ndefu hadi kufikia kupewa zawadi ya gari (jeep) lakini badala ya kujipanga na ku~focus kwenye kuwekeza kwenye muziki starehe zikamponza akapotea, akina Q chillah, Chiddy Benz, Daz Baba akina T.I.D, Ray C etc etc wote walikimbilia unga hadi wengine tumewapoteza na vipaji vyao akina Langa na Ngwair (R.I.P) to them.

Kimsingi nadhani kikubwa walifanya mziki usiokuwa na mkakati endelevu.
 
mimi navyoamini diamond kilichomtoa ukiacha melody zake ni kucheza pia... anacheza na madancer wake kila nyimbo ina style yake kiasi hata ukipiga nyumbani ngololo.. unakuta mtoto anajua inachezwaje.. ukibadili wimbo ukapiga sankoro mtoto anaacha style ya ngololo fasta anahamia style ya sankoro.. nyimbo za diamond zina utambulisho mkubwa wa muziki wake..

pili ni number 1 yenyewe ilikuwa tamu na davido alivyoingia mule akainogesha sana kwa video..

diamond anakwambia video ya number one remix waliifanya studio tu lagos siku moja tu, alikuwa lagos kwenye show aliitwa na davido ndipo wakaungia kuifanya video.. watu hawakuajiandaa kabisa.. wengi wa waliocheza kwenye video ni washkaji wa mwenye studio na wengine ni washkaji wa davido.. walikuwa kama wanazingua ndio maana ikatoka bonge la video africa huku hawakutumia gharama wala u serious kama video zingine... kuna watu wanakata mauno hata hawaelewi wanakata nini ni wanazingua tu
 
Mi nadhani tatizo kubwa ilikuwa ni strategies tu manaake kama ni collabo wapo wasanii walianza collabo mapema ila hazikuleta matokeo chanya.

Kwa mfano AY sio kwamba alianza collabo yake kubwa US moja kwa moja hapana. Kama una kumbukumbu mkuu kati ya mwaka 2007~08 alifanya collabo na P~Square ngoma ilikuwa inaitwa 'Fresh' by that time p~Square ndio walikuwa on fire na walikuwa wamefanikiwa kuliteka soko la Africa vizuri.

So kikubwa nadhani ilikuwa ni mpango mkakati lakini pia tusi~under rate nguvu ya social networks. Collabo ya AY na Sean Kingston wa US ni ya juzi sana mwaka 2012 au 2013 kama sijakosea lakini pia tukumbuke wasanii kama akina Juma Nature, Jide, Babuu (Inspector), akina Solo Thang et al hawakufanikiwa kutusua sababu kubwa pia ikiwa ni wadau wa muziki kuwanyonya.

Wasanii kwa mfano walifanya kazi kubwa na nzuri infact nyingi zenye kuelimisha ila waliokuwa wanajiita ma~promoter waliwanyonya sana wasanii na kuwakatisha tamaa baadhi ya wasanii wenyewe.

Lakini pia sumu kubwa iliyowadumaza wasanii wetu wengi nadhani ni ulimbukeni na kuiga starehe za kijinga baada ya kufanikiwa kupata vijisenti vyao kidogo. Kwa mfano baada ya msanii kutoa hit song akapata pesa badala ya kujipanga kuendelea kutoa ngoma juu ya ngoma wengi walikimbilia starehe, anasa na kuishia kuwa mateja.

Angalia watu kama akina Ferooz album ya yake ya safari na hit songs kama boss, au starehe zilimfanya akapiga hela ndefu hadi kufikia kupewa zawadi ya gari (jeep) lakini badala ya kujipanga na ku~focus kwenye kuwekeza kwenye muziki starehe zikamponza akapotea, akina Q chillah, Chiddy Benz, Daz Baba akina T.I.D, Ray C etc etc wote walikimbilia unga hadi wengine tumewapoteza na vipaji vyao akina Langa na Ngwair (R.I.P) to them.

Kimsingi nadhani kikubwa walifanya mziki usiokuwa na mkakati endelevu.
Tuanze na hilo la collabo ya AY na P Square. Kwenye post yangu moja nimetumia msisitizo maneno "KUSHIRIKISHWA" na sio "KUSHIRIKISHA".

Kwavile muziki wetu ulikuwa haujavuka mipaka; KUWASHIRIKISHA watu kama P-Square au 2Face ilikuwa ni kujifurahisha tu ingawaje wao walikuwa TOP in Africa. Ukiwashirikisha; wimbo unakuwa ni wako mwenyewe na sio wa P-Square. Na kv ni wako mwenyewe, P-Square au 2Face hawataipigania ngoma yako ichezwe kule kwao unless kuwe na makubaliano ya pembeni! Na kama mwenyewe hauna connection na media za nje basi ngoma yako itaishia kupigwa East Africa kama nyimbo zingine kwavile ndio ngome yako ingawaje umemshirikisha msanii mkubwa! Ni kutokana na hilo ndio maana collabo za aina hiyo huwa hazifanyi vizuri nje!

Kinyume chake, UKISHIRIKISHWA, tunafahamu ngoma ni ya yule aliyekushirikisha! So, kama ni Mnigeria; it's obvious ngoma itaenda kupigwa Nigeria. Na kama ulishirikishwa na wakali kama P-Square; ina maana sauti yako ita-trend sana pande hizo!

Tukirudi kwa Diamond, pamoja na yote vile vile alikuwa na zari moja! Collabo ya kwanza kabisa nje ya EA, ikafanya vizuri na kuzoa Channel O.

Zile Channel O hazikumvimbisha kichwa na badala yake kwake alizichukulia ni exposure. Akaanza kufanya collabo kwa fujo huku pia akishirikishwa kwa fujo. Ikawa akienda Coke Studio; yeye ni collabo.

Hii ikamfanya hata wale ambao hawakuipenda Number One Remix na Davido, si ajabu wakaja kuangukia kwenye Nanaa na Flavor, au Coco Baby na Yemi, au Bum bum na Iyanya, au Love Boat na kcee; n.k.

Kwahiyo ilikuwa ni ngumu sana kwa Wanaija kutomsikia Diamond kwa sababu alikuwa amekaba kila kona!

Kinyume chake; wakati bado artist ni Unknown, muziki wenu unknown; kwa mazingira kama hayo ni ngumu sana kutoboa na ngoma moja hususani kama umeshirikisha na sio kushirikishwa!

Hayo masuala ya kunyonywa, mapromota n.k yanaingia sana kwenye suala la maslahi na sio kuutoa muziki nje ya EA. Hata US; wasanii wananyonywa sana na ndio maana baada ya kushituka wakaanza kuanzisha label zao na makampuni makubwa yakitaka kufanya kazi na wao; inakuwa ni mkataba kati ya kampuni kubwa na label na sio kampuni na msanii! Lakini pamoja na yote hayo; hiyo haikuwahi kuwazuia kutusua nje ya US!

Social networks; sipuuzi mchango wake lakini tusisahau hata hao Wanaija waliokuwa wanatisha Africa yote enzi hizo; na wao hawakuwa na social networks lakini hiyo haikuwazuia muziki wao kuchezwa kila kona ya Africa. In short, level of playground ipo the same. Zaman sote hatukuwa na social networks na hivi sasa sote tunazo social networks na kwahiyo system inabaki in equilibrium.
 
Kosa kubwa lilikuwa ni kuwa chini ya Clouds. Muone Kiba anapewa sifa za hovyo huku mifuko mikavu.

Kuna wehu ambao ni mamluki kila akishauriwa vizuri Kiba utawasikia Kiba hana makuu. Hao ndio plots wa Mawingo jf kuhakikisha Kiba hainuki na kujitegemea kama Mondi.

Kuhusu Jaydee, Mwana FA na Nature waliwekewa vikwazo vizito ili waendelee kuwa watumwa. Kosa walilolifanya kwa Mondi ni kumu under rate.
 
Back
Top Bottom