Lafudhi

Lafudhi

we Mphamvu mbona matusi ndio zako!! Shameless

Matusi ni sehamu ya idolect yangu (namna yangu ya pekee ya kusema) na haihisiani na utu wangu wala heshima niliyonayo kwa wengine. Mathalani, kuna walokole wana kauli njema sana kama malaika, lakini wana roho mbaya hakuna mfano, tofauti na watu kama walevi ambao wana kauli chafu lakini ni wepesi kusaidiana kwenye matatizo.
Tizama mfano mwingine kati ya marafiki wanawake (mashosti) na marafiki wa kiume (wana), wadada hutumia kauli nzuri sana wanapozungumza wao kwa wao, lakini wakiachana wanaanza kunyeana tofauti na wanaume marafiki ambao hutukanana matusi ya nguoni, kudhalilishana na kadhalika na bado ni marafiki wa damu na husaidiana kwa tabu na raha.
Sijui wanielewa?
 
Last edited by a moderator:
Lafudhi yako ndo ilonfanya nncheke mkuu! Cheichei mkuu.

Nimemueleza stable woman (ingawa nina shaka na hiyo stability yake) hapo juu kuwa asiwe na shaka na lafudhi yangu na awage na amani tu.
 
Last edited by a moderator:
Nimemueleza stable woman (ingawa nina shaka na hiyo stability yake) hapo juu kuwa asiwe na shaka na lafudhi yangu na awage na amani tu.
Heheeee ! Haya mkuu, kuhusu stability yake huenda jina la kitabu lasadifu yaliyomo. Atakua stable haswaa si umeona lafudhi yake kwenye neno la mwisho mi sikumuelewa alitaka kusema nini. Hivi ni shameless eenh?
 
Last edited by a moderator:
Heheeee ! Haya mkuu, kuhusu stability yake huenda jina la kitabu lasadifu yaliyomo. Atakua stable haswaa si umeona lafudhi yake kwenye neno la mwisho mi sikumuelewa alitaka kusema nini. Hivi ni shameless eenh?

Stability
wapi dada, kashindwa kuvumilia lafudhi yangu vingine ataviweza kweli? Kuhusu maneno wanayotumia mi mwenyewe sielewi, naona wanajitiatia tu...
 

Stability
wapi dada, kashindwa kuvumilia lafudhi yangu vingine ataviweza kweli? Kuhusu maneno wanayotumia mi mwenyewe sielewi, naona wanajitiatia tu...
Abeeee! Kwikwikwi......Ajitiatia.......Mi si mtaalamu sana lakini nadhani shameless halina mantiki kwa jinsi alivyolitumia.
 
Kitaaluma tungesema hivi:

Lafudhi ni matamshi ya msemaji wa lugha fulani ambayo yanatokana na athari za kimazingira. Mazingira hayo yanaweza kuwa eneo atokalo mtu, mahali alikosomea, kiwango chake cha elimu, tabaka lake la kijamii na kadhalika.

Kwa hiyo hapa chanzo kikubwa cha lafudhi ni mazingira alimo huyo mtumiaji lugha, mazingira hayo ni kama yalivyotajwa hapo juu. Lugha mama pia inaweza kuwa chanzo cha lafudhi tofautitofauti, kwa mfano katika kiswahili, hawa watu wakizungumza wazungumzaji wa kiswahili watajua wanatoka mkoa gani au ni kabila gani:


  1. Usiniretee maswara ya ubaguzi wa kikabira hapa
  2. Amemupiga mutoto ya watu juu amemuibia mfaranga makumi mawili
  3. Ukikaa nchale, ukichimama nchale
  4. Wewe unakamuaga mang’ombe tu moja kwa moja
  5. Mbona unakuwa kinganganizi, nilishakwambia sikupendi lakini wewe bado unaningangania tu!
Lafudhi sio kitu kibaya, lakini pia huweza kubadilika kwa kutambua au bila kutambua (hii inaweza kutokea hadi umri wa miaka ishirini na). Lakini chanzo kikubwa cha lafudhi ni mzaingira alimo huyo mzungumzaji.


umechambua vizuri mkuu...ila kwa maono na maarifa kidogo ya lugha. Lafudhi kwa kiasi kikubwa husababishwa na lugha mama, mazingira ni kidogo sana kutokana na sababu za maingiliano. Mchango wa lugha mama katika lafudhi hauna shaka kabisa kwa mtamkaji wa lafudh fulan.
Ila kwa upande mwengne mazingira hufanya mtu kutekwa na kubadilishwa kutoka lafudh yake ya kwanza hadi mpya kutokana na wenyeji wake.
Kwa mfano mim ni mluguru labda, alafu nimezaliwa tanga mathalani sina ninachojua katika kikaguru, kwa bahat mbaya huku nilikozaliwa wazazi wang hawaongei kilugha chochote zaidi ya kiswahili. Unakuta nawakuta watu na lafudhi zao zenye athari za lugha mama lakin mim nitakuwa kati ya mswahili na lafudhi ile husika.
 
umechambua vizuri mkuu...ila kwa maono na maarifa kidogo ya lugha. Lafudhi kwa kiasi kikubwa husababishwa na lugha mama, mazingira ni kidogo sana kutokana na sababu za maingiliano. Mchango wa lugha mama katika lafudhi hauna shaka kabisa kwa mtamkaji wa lafudh fulan.
Ila kwa upande mwengne mazingira hufanya mtu kutekwa na kubadilishwa kutoka lafudh yake ya kwanza hadi mpya kutokana na wenyeji wake.
Kwa mfano mim ni mluguru labda, alafu nimezaliwa tanga mathalani sina ninachojua katika kikaguru, kwa bahat mbaya huku nilikozaliwa wazazi wang hawaongei kilugha chochote zaidi ya kiswahili. Unakuta nawakuta watu na lafudhi zao zenye athari za lugha mama lakin mim nitakuwa kati ya mswahili na lafudhi ile husika.

Nakubaliana na wewe mkuu.
 
Back
Top Bottom