Lala salama Hayati Magufuli hukuwahi Kudharaulika na Watendaji wako, Uliogopwa Kiufanisi, nchi ilienda na tulinyooka vilivyo

Lala salama Hayati Magufuli hukuwahi Kudharaulika na Watendaji wako, Uliogopwa Kiufanisi, nchi ilienda na tulinyooka vilivyo

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Wewe Mwenyewe kwa kutaka Sifa kwa tuliokuwa tukikusikiliza na kumuonyesha aliyekuwa Juu yako alikuwa hafai ulisema hutokuwa Mkali na Bandidu na utatudekeza sasa leo unalialia nini kuwa Unadharaulika na Watendaji wako tena uliowateua Mwenyewe?

Wenye Akili Kubwa hapa tunaona unatupigia tu Kelele na kutupotezea muda kwani tulikuambia Waswahili ukitaka uende nao sawa, uwanyooshe na waamke Kiutendaji iga Ubandidu ( Ubabe ) wa akina Hitler, Bokassa na Amin ila hukutusikia.

Na nikusaidie tu kuwa hao Watendaji wako hawaishii tu Kukudharau huko bali hata huku Mitaani tukiwa nao huwa Wanakusema vibaya mno huku wakisema sasa ndiyo Wanakupiga Pesa kuliko hata 2015 hadi 2021 huku wakisema Wewe ni Mvivu wa Kufuatilia Mambo na unapenda kufanyiwa Kazi na Wasanii na Wanafiki wanaokuzunguka.

Yaani GENTAMYCINE niwe Kiongozi halafu sijui Watendaji wangu na Watanzania Wanidharau mbona Moto wangu Watauona na watatafute Wenyewe nchi za kwenda Kuishi.

Namalizia kwa kusema ukijiona Wewe ni Kiongozi halafu Unadharauliwa, Husikilizwi na Watendaji wako wanakuona ni wa Kawaida (Joka la Kibisa) jua hufai au hukufaa kuwa Kiongozi hivyo fanya tu upesi acha hicho Cheo wape Wengine (GENTAMYCINE) nikiwemo kisha tulia uone tutakavyoongoza Kinidhamu na Kimaadili huku Ubabe (Ubandidu) ukiwa mwingi na wa Kutukuka.

Asanteni Watendaji mnaomdharau Mtu.
 
Back
Top Bottom