Landlocked umepakana na nchi isiyochangamka kama Tanzania, utafanyaje?

Landlocked umepakana na nchi isiyochangamka kama Tanzania, utafanyaje?

Hadi keshokutwa bado najiuliza kitu gani kinafanya watu wamuone K anafaa kuwa namba 1?

Ni mzuri kwenye kuongea huku amekaza uso, ila hana mikakati ya kiuongozi,

Nikumbushe,ni jambo gani amelisamia ipasavyo na likaleta matokeo chanya toka awe msimamizi..!


Hii nchi inahitaji ama kutawaliwa na Jeshi kamili au Mtu mwenye ujasiri wa kuwa tayari kwa lolote hata kufa alimradi atetee rasilimali na fedha za umma.

Vinginevyo pawe na katiba mpya yenye utawala wa Kiraia unaotokana na umma kwa ajili ya umma .

Katiba iliyopo ni ya kijeshi iliyovikwa vazi la Kiraia chini ya Watu wachache ndani ya CCM .
Kwa sasa tunachaguliwa viongozi watakaolinda mali za dhulima walizo nazo watawala kwenye mifumo yote.

Kuanzia majaji ,wakuu wa vyombo vya usalama , Wastaafu na waliopo kwenye madaraka ya juu . Wote ukiangalia muda wao wa utumishi ni miaka isiyozidi kumi ndani ya nyazifa zao za juu . Lakini wanautajiri wa kutisha na bado wanatumia dola kushinikiza utawala wanaoutaka wao.
Ni kakundi kadogo sana kwa watu. Lakini kana Jesuri kubwa sana kwa sababu ya kuegemea majeshi kuwatisha wananchi.
Sasa tujiulize ni vipi Raia ambaye anaihofia nafisi yake kwa kiwaogopa wezi wa mali za umma na vinaraka wa wazungu akawa Mzalendo.

Kwa Katiba hii ni Bora mwanajeshi awe mtawala mana ni Mzalendo ambaye yupo Tayari kuifia nchi yake. Hawa Raia wanatumia majeshi kutawala lakini wanalinda nafsi zao na mali zao huku wananchi na hata wanaowalinda wakiwa na maisha duni sana.

Kasimu Majaliwa ana uthubutu wa Kukemea wala Rushwa lakini wengine ni wanalinda Nafsi zao. Hata Yule Naibu wake hana Authority ya kukemea Rushwa . Na anajua kuwa hana. Na anajua kwa nini hana na ananua watu tunajua hana.

Ndani ya CCM kwa sasa ni Kasimu na Makonda . Mwingine ambaye wamemdhibiti kihuni ni Polepole.

Vinginevyo tutaenda na Lisu ili waovu wasitamalaki na kujimilikisha hii nchi.


Makampuni yote ya Wageni kama wahindi,waarabu na Wachina yanafanikiwa kutokana na mipango mizuri lakini na usimamizi mzuri wa kuwadhibiti wazi.

Kasimu ana uwezo wa kusimamia mipango ya serikali ambayo ni mizuri tangu Mwalimu Nyerere lakini inakosa wazalendo wa kuisimamia.

Tanganyika imeuzwa kwa wageni wachache wakishirikiana na Watu wachche waliojivika ngozi ya utawala wa kidemokrasia chini ya Katiba ya Kijeshi na Kidikteta .


Katiba iliyopo ikipata kiongozi mzalendo tunapata maendeleo ya haraka sana .
Lakini katiba iliyopo ikipata Mtawala Mbinafsi na Fisadi atachukua mali zote za nchi na kujilimbikizia mali yeye na marafiki zake chini ya mwavuli wa uwekezaji. Kifupi tukizubaa hii nchi itagawanywa bipande vipande kama Kongo kwa sababu ndiyo nchi iliyobaki yenye amani na Rasilimali nyingi amabazo zinaishia mikononi mwa Wachche kwa kasi sana huku Pakiwa na kundi dogo la machawa ,mashoga ,wasagaji , wezi na wauza madawa na magendo wakiwa wanaishi maisha ya anasa na kufurahia kwa dhihaka na ulaghai kazi njema sana ya uumbaji wa Mungu kwa Nchi ya Tanganyika.

Wahuni na wafuasi wao tutawakataa 2025 kwa namna yoyote.
 
Power corrupts. Tukikupa uraisi wa Tanzania leo, kesho hayo yote uliyoyandika hapa utayasahau na kuanza kufisadi kodi zetu.
Halafu kumsomesha mtanzania ukitegemea kwamba atakapo hitimu masomo yake atakuja kuisaidia nchi yake, sahau. Kwa kuwa wakirudi kutoka masomoni kazi yao kubwa ni kufisadi, kujitajirisha yeye na familia yake. Ni kama walienda kusomea ufisadi.


Hapana .
Labda hujui ni kwa nini hawa waliopo Madarakani ni wezi wabinafsi.

Kwanza ni Katiba iliyopo ina mpa mtu mmoja nguvu kubwa sana.
Mtu mmoja akiwa na Nguvu kubwa halafu akakosa uzalendo na kuamua kuteua watu na kuwalinda kwa maslahi yake na kundi analoliteua basi nchi inageuka kuwa kama Vita vya manyani porini . Mwenye nguvu atashiba mufa wote .

Katiba hii iliyopo inahitaji Mtu mwadilifu na mzalendo wana . Lakini aliye tayari kuwakataa hata marafiki na wakwe zake pale wanapokiuka utaratibu na kuharibu mali za umma.

Killa siku sheria mpya zinatungwa na kubadilishwa kutokana na Katiba ambayo haiendani na wakati matokeo yake tunatumia mbilioni kuandaa mavitabu ya sheria na marakebisho yake ambayo hatadumu hata miaka miwili. Fedha zinateketea. No one cares .

Jambo la pili ni Historia ya Wengi waliopo madarakani au waliostaafu.

walisostaafu wengi ni zao la wasomi waliosoma wakati wa Mwalimu Nyerere na kusomeshwa ulaya ,Urusi ,uchina n.k. bila kuwa na usimamizi mzuri matokeo yake wakawa ni wasaliti wa mfumo wa kijamaa kwa kutamani mali za umma ziwe zao binafsi kuanzia mashirika ,nyumba na hata mabenki na viwanda .
Hawa waligeuka kuwa maadui wakubwa wa mwalimu Nyerere ndani ya nafsi zao. Wakaua Viwanda vyote na mashirika ya umma na wakajiingiza kwenye siasa ndani ya Chama cha mapinduzi .

Hivi unawezaje kuua kiwanda cha Viberiti ,tairi, nyaya bora na imara za umeme , viwanda vya mbegu na sasa tunaagiza mbegu kutoka nje kwa manufa ya wachche wanaoshika tenda.

Sasa kizazi hiki kilichopo madarakani kwa asilimia kubwa ni kizazi kilichopata Elimu kwa njia ya wizi wa mitihani na nafasi kimichingo. Hawa hawaamini katika uadilifu.
wengi wmesomea mishahara na sio taaluma kamili.

Kwanza hawana muda wa kuwaza mambo ya kitaifa. Wanajua ukishakuwa MwanaCCM basi huna tena cha kupoteza mana wanaaminiCCM itatawala milele.

Lakini hawa watoto waloko mashuleni hasa Sekondari na Shule ya msingi ni kizazi tofauti sana .
Hawa wamepata Elimu yenye itakayowafanya wapiganie maisha mazuri na usawa kwenye mahitaji muhimu.
Hawana uvumilivu mana hawatawavumilia hata wazazi wao wala kuwaonea huruma watakaowaumiza.

Kama unavyoona watu hawana uvumilivu kwenye mahusiano na familia basi ujue hata watawala hawatavumiliwa na kizazi kinachokua sasa.

Ni vema watawala wakaweka misingi mizuri ya kuwawajibisha Mafisadi mana kizazi kinachokuja hakitawavumilia .

CCM wakikaidi na kuendelea kujenga misingi ya wizi na ufisadi watajenga Taifa baya na lenye watu waovu na wahalifu mana kila mtu anainuka kujitafutia mali kwa halali na kwa dhulma alimradi apate mahitaji yake kama wengine. Uhalifu utakua mkubwa na hata uasi kama Nigeria na Nchi nyingine za Magharibu ,pembe ya Afrika na ya Mbali kama Mashariki kama Afghanistan.
 
Back
Top Bottom