Laptop inashindwa

KyelaBoy

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2008
Posts
206
Reaction score
22
Hi wapendwa,
Ninatatizo na laptop nitumiayo ambayo ni ya kampuni,mtaalamu wa IT wa kampuni amedhibiti hii laptop kwa kufunga code zake kiasi kwamba hata ukitaka kuweka programme yoyote inakataa,yeye yuko NRB nilichofanya nikupeleka kwa fundi aliyejitahidi kufungua hizo code na sasa naweza angalau kuongezea vikorombezo vingine,tatizo linakuja pale ninapotaka kusikiliza muziki kutoka kwenye flash disc,huwa inakuwa inatoa mlio wa kama vile cd imekwama na baadaye hujifunga,na sasa hata nikifungua huchukua muda mrefu.
Je nifanyeje kurekebisha hilo tatizo la kukwama kwa mziki au picha na kuchelewa kufunguka.pia nimesoma kuwa Mitsumi garage ni wataalamu waliobobea je ni kweli.
Na mwisho nawashukuru sana wataalamu wanaotoa mada za ICT hapa jamii,mimi sijui chochote kuhusu ICT lakini kwa kuanza kusoma mada mbalimbali kutoka kwa watu kama Invicible,Shy na wengineo nimeelemiki kiasi kuhusu ICT,kwa mfano kwa sasa kwa kupitia huu mtandao nimeweza ku down load portale App suite.
Huo ndio uzalendo,sio lazima wote tuwe wabunge au wanasiasa ndio tujifanye tunaweza kujenga nchi.
Asante sana na kwa wengine tujitahidi kupitia hii sehemu ya Teknolojia ,tusiishie kusoma mambo ya akina Liyumba ,dowans na vituko vya wakubwa havitusaidii.
Aluta Continua
 
Ndugu kama ni mali ya kampuni ni watu wa kampuni tu ndio wanahusika na mali hiyo mpaka yeye mwenyewe aseme ameshindwa waamue sasa kutafuta msaada wa nje

je unapofanya kazi hapo huwahi kusaini kitu kama mkataba fulani wa utumiaji wa vifaa vya ofisini ?
 
bado ila nafikiri watafanya hivyo kwa baadaye,tatizo ni kuwa siwezi kutumia laptop yangu kwa shughuli za kiofisi kwani hairuhusiwa na kazi zangu ni za kusafiri safiri na siwezi kubeba laptop mbili,asante kwa ushauri itabidi niachane na mambo ya kufanya marekebisho
 
Unaweza kulazimika kuwajibika kama chochote kikitokea kama taarifa kuvuja kuibiwa na vitu vingine hao technical support wa makazini kwenu ni muhimu sana wape chance wafanye kazi zao
 
Well nakushauri usijaribu kuzikwepa hizo security settings utajiingiza kwenye matatizo.

Lakini sidhani kama muziki kukataa kucheza ni moja ya hizo security settings, kama unacheza muziki straight from flash basi jaribu kukopy kwanza kwenye harddrive, pia kama unatumia program ya mziki ambayo ipo kwenye flash jaribu ambayo iko kwenye hard drive. Vinginevyo jaribu kuupdate sound drivers, lakini kwa hili unaweza ukahitaji huyo jamaa wa IT akusaidie, lakini sidhani kama ni tatizo.
 
Get ur own laptop Sir, n leave the company equipment to save the company needs, ulichokifanya kuharibu security settings unatafuta matatizo. Chapa kazi music nunua iPod ziko za kumwaga.
 
Asanteni wote kwa ushauri mzuri,Kang,Shy na N-handsome
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…