Hahaha, muuliza swali umetisha leo!! mwanafunzi yeyote wa chuo ni sio kua na laptop tu, bali access na internet ya kutosha, tatizo la wanafunzi wa Tanzania ndio linakuja hapo, wanachukulia kusoma ka adhabu vile, au kusoma ni ile kwenda shule unamsikiliza mwalimu unafanya mtihani afu imetoka. Kusoma bna ni kuongeza knowledge, lazima upende kujua kitu kwa undani zaidi hata ya mwalimu wako, lazima upende kujua kitu kulingana na dunia inavokwenda na kujaribu ku-make something new ambacho ni bora zaidi ya hapo, ndivyo wanafunzi wa nje wanavyofanya, yani bongo ni wavivuuuuuu ndio maana last year 95% ya form four walienda chaka, unataka uniambie asilimia yote hiyo ni kua hawana access nzuri na elimu? tena katika hiyo 5% asilimia kubwa ni watoto wa maskini na avarage families, kuna softwares mfano iTunes U, sites kama coursera.org na edx.org wanatoa FULL COURSE mbalimbali tena BURE, na hizi lectures ni kutoka vyuo bora duniani eg. Harvard, MIT, Yale etc.. na nikwambie ukweli, hawa jamaa walifikiria Africa hakuna watu safi ndio maana wakaanzisha hii kitu, ila aibu only 3% ya waliyokwenye hii site wanatoka Africa, 97% wanatoka kwingine. Wewe unasoma finance, kichwani unaweka umalize uende uajiriwe ukae uvae tie, unadhani maisha mepec hivo? soma na course nyingine mfano ukichukua CS50 ya Harvard Intro to Comp Science, ukajifunza programming, unaweza ukatengeneza apps zako mwenyewe ndogondogo za finance since utakua umesoma finance, Usikae ukachoka kusoma ati kisa wewe ni finance ukadhani vingine havina maana, kuuliza hivo inaonyesha kabisa hata uwezo wa computer ni mdogo, nani atakuajiri sasa kama computer hujui? Mimi siku wanafunzi wa Tanzania mkubadilisha ideology zenu kuhusu elimu ntawaona watu wa muhimu sana, kwa njia hii.. ndio maana siku hizi graduates wengi wanaishia doro tu mtaani, kubangaizabangaiza tu