Laptop zina kodi nikiagiza nje?

Kang

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2008
Posts
5,655
Reaction score
2,506
Kuna mwenye ufahamu kuhusu hili, nakumbuka kuna wakati walifuta kodi kwenye kompyuta je iko hivyo kweli?
Kuna wakati niliagiza laptop battery na RAM kutoka amazon nikapigwa kodi je kwa laptop kodi ipo?
Asanteni.
 
Hapa kodi tuu .....[HASHTAG]#hakuna[/HASHTAG] namna..!
 
Kuna mwenye ufahamu kuhusu hili, nakumbuka kuna wakati walifuta kodi kwenye kompyuta je iko hivyo kweli?
Kuna wakati niliagiza laptop battery na RAM kutoka amazon nikapigwa kodi je kwa laptop kodi ipo?
Asanteni.
Haina kodi.
 
Kodi ipo kwa ajili ya laptops kwa ajili ya yoyote anayetaka kuagiza, kuna rafiki tangu amepigwa hela kinoma.
Anasema kama 60% ya thamani ya machine, kuna VAT, Import Duty, Kodi ya Reli etc.
 
Kodi ipo mkuu ila ni ya tofauti na bidhaa zingine kama za luxury goods
 
na jee simu nimeona samsung galaxy s4 inauzwa dola 80 jee nitakatwa kodi?
 
Brother wasiwasi wangu ukiagiza kutoka nchi kama china,ujiandae na lugha kwa chochote utakachotaka kufanya na hiyo laptop..
 
China unaagiza laptop hizi ndogo ndogo freshi tu, nimenunua Chuwi Hi10 pro $230 , 10inch, 4GB ram, 64GB storage, windows10/Android tablet na keyboard dock yake, iko freshi sana kwa portability. AliExpress, wachina wajanja wanafoji bei posta inapita bila kodi lol.

Sema nataka gaming laptop hizi china ngumu kupata ya uhakika.
 
Nijuavyo stationary material material haina kodi,nimeshawah agiza laptop uk 2 yrs ago sikuchajiwa kodi,labda Kama imedilishwa hivi karibuni.
 
sio laptop tu mkuu, hata ukiagiza Chupi kodi iko palepale
 
Hiyo sheria imeshafutwa..

Kodi kama kawa.. Mi nilishapigwa kodi, halafu ni kubwa kinyama..
Kiongozi, hebu nipe estimation manake nina shida na iMac lakini kwa bei ya TZ ni pasua kichwa wakati refurb kutoka Apple store, unapata ya maana kabisa kwa USD +1000K.
 
Kiongozi, hebu nipe estimation manake nina shida na iMac lakini kwa bei ya TZ ni pasua kichwa wakati refurb kutoka Apple store, unapata ya maana kabisa kwa USD +1000K.
USD 1000k..?? hivi unakijua hiki ulichokiandika au unachangamsha genge tu.??
Okeii ..1000k = 1,000,000 hapo haujazidisha na 2300 kuiconvert kwa pesa madafu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…