balibabambonahi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2015
- 15,771
- 14,294
Safi Sana,
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu usimuliaji wako huu ni kama kweny LEGEND OF THE SEEKER.Tendelee Eid imepita sasa japo wapo wanao malizia
Basi pale mi nilihama kutokana na mauza uza Yale akuna ambae angeweza kuvumilia niliwaza kwanza awa watu naishi nao hapa ni majini na majini chakula Kikuu ni binadamu sasa ikitokea siku wakakosa uko mi ntageuka kua chakula nikaondoka pale.
Nikatafuta eneo jngne nikaanza maisha tena ila kwa vile sikua na mishe nikawa nasaka hapa na pale sasa kuna rafik angu mmoja Robati alikuja kunishtua palikua na ishu ya ulinzi kampuni ipo hapa Dar jina kapuni ilihitaji watu na wanawapa mafunzo kisha wanangia kazini mi niliona najiweza tayri nishatumia bunduki sio ishu kwangu tulifanya mpango barua za wazamini na paspot saiz tukapeleka maombi aikua tabu walihitaji watu si tukaingia moja kwa moja kwenye mafunzo na tukapata kazi ya ulinzi.
Sasa ulinzi ule ulikua unafanyika sehemu tofautu tofaut makampuni au shule au nyumba binafsi wanapohitaji walinzi kampuni ikipewa tenda inapeleka, mi nilipangwa na mwenzangu mmoja sio yule robati uyu ni mwngne robati alipangwa sehemu nyigne sisi tulipelekwa nyumba ya mtu binafsi alikua ni mama mmoja ivi mfanya biashara tukawa tunalinda pale.
Siku iyo saa 11 alafajiri yule mama anatoka mwenzangu yule akamfungulia geti akaondoka alikua na gari mi nipo pale ndio nilikua na bunduki yule akua na bunduki mim sikua mtu wa kujionesha sababu nipo na bunduki nilikua Mara nyingi najificha lakini kila kinachoendelea naona sababu ukiwa mlinzi upo na silaha majambazi wakivamia popote pale cha kwanza wao tageti yao ni mwenye silaha maana wanaona yule ndio ata waletea shida wanaanza na uyo kwaiyo lazima uwe makini unapokua mlinzi na upo na silaha wewe ndio inabidi uanze kumuona adui na sio adui aanze kukuona wewe.
Iyo mida baada ya yule mama kutoka na palikua na mbwa pale jamaa akawafungia wale mbwa bandani, baada ya dakika chache mbele ile gari ya yule mama ikarudi na kupiga honi pale getini ila honi azikua zile za kawaida jamaa akafungua mi nacheki tu ile gari ikaingia ndani ilipopita pale getini yule jamaa aliona watu wamemteka yule mama wamo ndani ya gari jamaa akashtuka akatoka mbio kuelekea bandani ili afungulie mbwa ile anashika komeo alipigwa risasi tatu mgongoni pale pale akafariki na mbwa wale akufungua mi nikaona hapa nipo na watu wenye silaha nzito ukicheki ya kwangu ni ya kukoki upige alafu useti wao wanazo za kuachia mfululizo ina maana nikiludisha shambulizi sichukui muda na uwawa fasta ikabidi ni bane tu ukicheki nisha survive maeneo kibao uko alafu nife kizembe tu hapa hapana .
Kuna jamaa mwingne nae alikua mlinzi iyo siku wanavamiwa alikua yupo kizembe tu yupo eneo la wazi alafu na kirungu tu jamaa walimpiga tofali kichwani akazimia aliposhtuka akakuta kashapigwa kamba wakampiga virungu vya kichwa vya kutosha alilazwa muhimbili miez mitatu kichwa kina manundu mpaka Leo na ile kazi aliacha na akarudi kwao Dodoma.
Uamuzi nilioamua ni kufanya mawasiliano nikampigia kiongozi wetu ili waje kuongeza nguvu msaada ulikuja kama nusu saa mbele na ile kampuni kubwa ina ambulance za wagonjwa wakaja wakambeba mshikaji wale majambazi walichukua kwa yule mama milioni 30 alafu yule mama wakamfunga kamba, inaonekana mama alikua nazo izo pesa ndani na kuna mtu alichoresha sababu jambazi akurupuki kuvamia kama kibaka
Kibaka ana mvamia mtu ajui labda ana ndizi na pilipli tu lakini jambazi anakua na ramani kabisa kwaiyo anaenda akijua kuna nini.
Walimchukua jamaa akiwa kafariki tayari apakua na la zaidi Mimi niliomba pale nihamishwe na wakanihamishia sehemu nyingne.
Hapa nilikua na jamaa mwngne nae sio mjuzi sana kwenye ulinzi isipokua ni ujanja ujanja tu sehemu nilio amishiwa ilikua karibu na bahari, siku iyo usiku mnene sana ghafla getini nikamuona bibi kasimama sijui katokea wapi sikumfata kumuuliza nilikaa kumtazama tu pale alikaa karibu masaa manne badae akaondoka mwenyewe kwanni sikumfata uwezi jua labda katumwa chambo ukijitokeza ovyo na kuleta shobo kwake unastukia umepigwa wewe ivyo sikumfata akaondoka mwenyewe
Siku nyingne tena nipo lindo hapo na yule mwenzangu tupo ndani tukasikia mtu anapita taratibu nje kuchungulia alikua na mavaz ya kike anapita anaenda ila alikua na marashi makali ananukia juu kichwani aonekani vizur ila chini unamuona akapotea zake yule mtu.
Siku nyingne ilitokea zarulala yule mwenzangu akaenda sehemu nyingne pale nikabaki peke angu wakati nipo lindo ukanipitia usingizi bana mida kama ya saa Tisa au sa kumi hii tunaita asubuhi ya uongo sababu panakua na muangaza flani ivi kama asubhi kumbe ni usiku hapa ukijichanganya unajua asubuhi kumekucha mi mudawangu ukifika naondoka mi nikaondoka bana mdogo mdogo nimefika sehemu kuna viwanja viwili vya mpira cha kiwanja cha kwanza nikasikia kelele za watu ndio nikajiaminisha kabisa kwamba kumekucha nikawa napita nakaribia ule uwanja ghafla nywele na mwili vikanisisimka sana sasa napita pale uwanjani nikakuta paka wengi sio watu nikajua hawa sio paka ni wanga nikanyosha sikuegeuka .
Nimefika mbele nikakutana na mtu akaniangalia sana sasa nimevaa gwanda zile za ulinzi akutilia Shaka mi nikaenda mpaka nyumbani kitandani nimetulia naona kiza kinazidi kila nikichungulia nje mhm badae nikasikia swalaha swalaha ile alfajir nikajua nimebugi siku ikapita.
Sasa yule jamaa niliepangiwa nae alikua na simu ya smartphone kubwa mi nilkiua nayo ndogo ambayo ina uwezo tu wa kuingia Facebook basi jamaa aliniambia nijiunge Facebook mi nikamwambia fb sitoiweza kutokana na lugha ya mule na Mimi sijasoma akaniambia aina mambo mengi na kipindi icho watu wengi fb ndio wanajiunga kwa wingi akasema unaposhindwa nta kuelekeza kweli akaniunganisha fb fresh akanipiga picha akaweka kwene profile akanielekeza vipengele vichache mi nikaanza kuchati alikua bi mkubwa flani ivi nikaanza chati nae ni mmama mtu mzima mtanzania lakini alikua anaishi Denmark akasema ye yupo kule miaka mingi anafanya shughuli zake na kaolewa uko.
Nika mwambia nahitaji mchumba uko vipi siwezi pata msichana uko akaniambia ngoja, basi nikawa nikipata mb naingia namsalimia fresh siku iyo akanitumia picha ya msichana akaniuliza uyo vipi nikamwambia yupo vizuri akasema ila ana watoto lakini anaishi mwenyewe tu hana mtu mi nikamwambia sawa akuna tatizo mama.
Akaniambia uyo siku za wikiendi anakuaga hapa kwangu kwaiyo nta kuunganisha akaniambia nitumie picha zako ili nimuoneshe du nikalipokea ilo nika mshilikisha yule mshkaji wakati tunatoka lindo akasema mi nakujua kwenye kuvaa sio mzembe cha msingi ukiwa home chagua pamba za maana vaa fresh nikupige picha tutume.
Tukafanikisha lile jambao zile picha nikamtumia yule bi mkubwa akaenda kumuonesha yule Dada zile picha akazikubali alafu yule mama akasema nimpe namba ya simu tulituma na yule jamaa yangu akasema tutume na code namba sababu ni nje ya nchi inahitaji ianze na code namba hii 255 jamaa alikua anani elekeza vitu vingi .
Kweli kwa Mara ya kwanza simu yangu ikapokea simu kutoka nje ya nchi ndio alikua yule binti akaniambia uyu mama kanipa namba zako alafu nimeona na picha zako mi pia nikamsifia pale ndio tukawa sasa tunawasiliana ila uyu dada alikua katokea kwenye kambi za wakimbizi uko burundi au Congo aliondika pale kwa msaada wa UN kwaiyo kiswahili alikua ana kiongea vizuri na tayari yeye alikua anatambulika raia wa kule ikawa sasa mida ya usiku wakati katulia akawa anapiga simu kwangu tunaongea.
Baadae akaniuliza utumii Skype au Viber nikamwambia simu yangu ina uwezo mdogo sana aiwezi Fanya ivyo vitu na kipindi kile wasap ilikua bado akasema kupiga simu kwangu anatumia gharama kubwa sana nikamwambia mi nafanya kazi ya ulinzi na hata uwezo wa kununua izo simu sina akaniambia uku kazi za ulinzi zina hela akasema basi ngoja nikufanyie mpango upate simu kubwa nikaona hapa natengenezewa mazingira basi nikasubiri.
Siku kazaa akaniambia nataka nikutumie pesa sasa nikajiuliza uyu pesa anatumaje na tuko mbali ivi mi bana sikua mtaalamu wa aya mambo ya mtandao ye akasema ata nitumia kwa njia ya western Union au money gramu mi ivo sivijui akaniulizia kitambulisho nnacho akasema nitatuma pesa alafu ntaweka majina yako yaliyo kwenye kitambulisho usikosee ata moja maana wata kusumbua kweli siku ya jumatano ilikua pesa iliingia nilipata ujumbe kwenye simu sababu aliweka namba yangu na aliniambia isizdi siku tatu sijachukua pesa inarudi kwa mwenyewe japo siku izi naisi wameongeza siku sjui ni siku saba akanipa namba za siri za kuonesha pale na majina yake fresh pale nikapata muangaza sasa na kutambua .
Nilienda bank nikafanya taratibu zote na kutoa copy kitambulisho na ishu zingine hatimae nikapata ile pesa kutoka nje ya nchi.
Tukawasiliana akaniambia yule bi mkubwa anakuja Tanzania ivyo atampa mzigo wangu aniletee Mimi na yule bi mkubwa siku kazaa akaniambia anakuja Tanzania kapewa mzigo ila akusema kuna nini ,
yule mama alisafiri mpaka uku Tanzania alifika ila sasa nikawa simpati kwenye simu kila nikimtafuta kumbe alikua yupo kweye ishu za kubadilisha laini kupata laini za kwetu uku.
Siku iyo mida ya saa kumi na moja jioni akanicheki tukaongea akasema tuonane mida ya saa mbili usiku maeneo ya Makumbusho ukawa mtihani mida iyo inabidi niwe kibaruani lindo sasa hapa nikapanga nikaombe ruhusa kwamba nimepata zarula lakini nikawaza nikaona watanizingua sababu kule wana ntegemea sikwenda siku iyo nilichofanya nikaenda saloon nikajiweka fresh ili niwe na muonekano wa utanashati alafu nikaenda mpaka pale makunbusho palikua na kama mgahawa pale ndani mi niliwai ili akija anikute nishafika nimekaa pale nikaona sio walau nijibust kuondoa noma akija nichangamke nikapata kinywaji kipo kama zanzi ivi nikapigilia nikapiga na pipi kifua kukata harufu.
Mida nikaona tax inakuja pale mbele yangu alafu ikanimulika taa flani ivi za kunishtua nikajua hapa keshaniona kweli alishuka yule bi mkubwa kwa shangwe nyingi tu yupo na wanawe rangi nyeupe ye aliolewa na mzungu ................................
Tutarejea
Hivi hii sio kweli maanake hii story uongo ehh? Isije kuwa chai!!Naaaamu Turejee sasa
Jamii forum na Hati chafu, za mapenzi ni kweli zinaharibu nyuzi???? Mkaguzi mkuu wa nyuzi JF fdizzle na msaidizi wake TODAYS wata jibu Embu tuone
Inaendea
kile chombo chao au meli walyokuja nayo ilikua na mushkeri kidogo sasa kufika kwao pale ni kwajili ya marekebisho alafu ile meli kumbe waliiteka na watu waliopo mule sikujua waliwaacha wapi nahisi yawezekana waliwatosa majini lakini pia mule mlikua na vitu walivyoteka Mchele, unga, sukari, samaki na vingne vingi kwaiyo kwa ishu ya misosi aikua tabu tena kwangu apo ni mtelezo tu.
Kwaiyo apo sasa yule Sofia ndio alikua mpishi na Mimi mda mwingi ndio nilikua nae kumsaidia kutengeneza samaki na mboga mboga kisha msosi fresh.
Wale jamaa walendelea kuwepo pale mpaka maji yalipo pungua kwwnye kile kisiwa kunakua na siku maalumu ya kutoka yale maji sasa ile meli ndio ilikua na tatizo chini kwaiyo maji Yale yalipo pungua ndipo ikawa nafasi ya wao kuweza kurekebisha ile meli.
Walifanya mawasiliano na wenzao wakaja pale wakfanya marekebisho ile meli ikapata afazali sasa hapo ndio wakaniambia twende mbele yani niondoke nao kuelekea uko kwenye uharamia wa kuteka meli baharini humo .
Walitoa begi moja la silaa kisha wakaniambia nichague ipi itakayo nifaa nikachagua silaa moja inaitwa Raifo sina hakika kama nimeandika sahihi wakaniuliza kwann umechagua hii niliipenda tu zile ni Silaa ambazo zilitumiwa na ma sniper kwa juu ilikua na lenzi binafsi nieleze nilishawai kufundshwa kutumia silaa na babu yangu alikua muwindaji wa wanyama pori alikua anatumia izi silaa lakini sio kama ile.
Hii iliboreshwa zaidi na baba yangu nae alikua mtaalamu wa kutumia silaa.
Basi nilichukua ile silaa ili kuwaonesha kwamba na Mimi naweza itumia nikafanya jambo moja wale wabaya wangu nyani ndio nikaona ngoja niende uko Leo nika wanyooshe nikamchukua Sofia tuka elekea kule msituni uzuri nikakutana nao tukiwa na Sofia nikamtandika nyani mmoja na tukarudi kule na Sofia na yule nyani.
Yule nyani pale wale wajamaa walimtafuna vizuri mi ndio nilimtengeneza sasa hapa nikajua jamaa hawa magumashi akuna cha dini wala nini hawa ni maaalamia tu dini wanayao lakini awa izingatii wnabaki tu na kivuli cha dini awana lolote tulikula nyani yule vizuri .
Sasa tukaingia kwenye utekaji katika ishu hii ya utekaji tulishateka teka sana Ila kuna tukio moja lilikua kubwa ambalo tulikutan nalo uko baharin, tulikutana na meli ya wafanya biashara ambayo ilikua na mizigo tuliwateka wale jamaa na tukachukua mzigo wao,
wao tukawaacha na hata meli atukuizamisha sasa kumbe wale jamaa wakafanya mawasiliano na askari wa patrol kutokana na ule uaharamia tuliofanya sisi atuna habari ghafla wakaja wale patrol na boti zao walitumia spika vipaza sauti vile kwamba tunatakiwa tujisalimishe alafu ile meli yetu pale palipotengenezwa palileta itilafu tena kwaiyo ikawa aina spidi sasa mi ndio nilikua na ile silaa ya kulenga mbali nilikua juuu
kwaiyo pale ikabidi nianze akuna kungoja walikua na boti zao mbili nilipiga moja kwenye tenki za mafuta nikapasua wale jamaa fasta wakahamia nyingne nzima ile niliyopiga ikalipuka hapa nafikiri wali elewa kua kuna mdunguaji.
Awakuchukua mda waliondoka pale sie tukaendelea na safari yetu taratibu alafu katika kupora vitu kuna jamaa nilimpora begi ndogo ivi ye nahisi alikua mtu wa kanisa nilivyo fungua nilikuta kuna vitu vya kanisa na pia kulikua na msaba wa dhahabu niliuchukua nikauficha ikitokea uko mbeleni unisaidie kama nikiuza.
kumbe walivyo ondoka wale patrol walienda kujipanga,
sisi atuna habari
Ghafla walifika wale jamaa na boti tatu tena sasa walipofika awakuchelewa wakaanza kurusha risasi kwetu yule masuz na mwingne ally pamoja na mwingne tena kasimu wao wakaanxa kujibu mashambulizi mi nilkua kwa juu kabisa wao wapo chini katika kurushiana zile silaha yule masuz dada ake na Sofia akapigwa risasi kifuani kwenye moyo nyingne begani akazima pale pale.
Sasa kule juu Mimi nikaendelea kulusha zile risasi ila walikua wanatuzunguka awatulii sehem moja baadae Mimi niliipigwa risasi ya kiuno lakini ilinipalaza au kunikwangua aikuingia moja kwa moja nilikua navunjika kiuno hapa lakini sikupata athari kubwa basi nilidondoka toka kule juu mpaka chini kwenye meli nikapoteza fahamu pale pale.
Nilipokuja kuzinduka tuilikua kisiwani yule Sofia alikua akinisaidia kunitibu lile jeraha la kuchunwa na risasi alitumia kisu cha moto kuchoma lile jeraha kuondoa kama kuna unga ule wa silaha ili kuua sumu maana zikibaki huwa zinaleta mazara ata kansa pia akachukua majani flani ivi porini akaniwekea ya dawa.
Jamaa yule kaka ake na Sofia masuz tayari alishafariki ivyo tulifanya namna pale tuakamsitiri jamaa, Dada ake alikua na majonzi sana siku ile ndio ishatokea sasa,
Tulikaa pale kwa siku kazaa baadae tukaondoka pale kisiwani tuka elekea kwao walikotokea wao uko somalia namimi kama jamaa yao tulishaungana pale basi tulienda waote mpaka somalia.
Tulipofika kule baada ya kuwasili Mogadishu niliambatana na Sofia mpaka kwenye makazi yake nilikutana na ndugu zake akanitambulisha fresh na pia akafanya mpango kwenye shughuli za uvuvi kuniunganisha na jamaa flani ivi ambao wao walikua wana vua papa kwa kutumia ndoana flani ivi za shaba ndio zilikua imara kwa kuwanasa wale papa.
Niljiunga na jamaa kufanya ile kazi ila Mimi nilikua upande wa kuchochea makaa ya mawe tulikua kwenye zile meli zinazotumia makaa ya mawe sio mafuta ndio nilikua na chochea ila baadae nilisogea mbele nikaacha kuchochea makaa nikawa kwenye upande wa kuvua.
Kule sasa kwenye kuvua ndio nikajua jamaa wanavua papa kwa kutumia chambo za mahiti ya watoto wachanga wa binadamu jinsi wanavyopata vichanga ni vile labda kama mtu mimba yake imeharibika au mtoto kafia tumboni zile mimba kubwa au kazaliwa kafa au wale wanao toa ujauzito mimba kubwa sasa katika kutupa ndio watu wanatumia iyo fursa ule uchafu unachukuliwa na inawekwa oda kabisa kwenye ma hospital tena ina pesa nzuri tu ambayo ma dokta huwa wanapata kupitia hii ishu mpaka leo.
Lakini ni kwa usiri inafanyika hii biashara sio waz wazi so kupitia chambo hiki papa huwa wanakamatika kilahisi na hata ukimpasua ishu ya kukuta labda sikio la binadamu au kidole nywele viungo vya binadamu kwa ujumla ni kawaida sana
Ni ishu ya kikatili ki binadamu lakini ndio watu na kazi zao ..................... Latino is on
Sio kweli slip way
Ya kahawaHivi hii sio kweli maanake hii story uongo ehh? Isije kuwa chai!!
Ata mimi nime shtuka Sukari ime zidiiiHivi hii sio kweli maanake hii story uongo ehh? Isije kuwa chai!!
Aijaanza Leo cha kufanya ongezea tangawizi tu itazidi utamusasa chai imeanza
.Ata mimi nime shtuka Sukari ime zidiii
Hichi kipande Cha kukosa zari KWA mtoto wakike kimeniuma sanaa....niliwai kumfukuzia dem mmoja hakua mzuri Wala nini....tuli kua Just friends...Tuendelee
Baada ya kukutana na yule mama aliniambia niingie kwenye gari ina maana tulitoka pale na kuelekea nyumbani kwake tumefika tukatambulishana vizuri na familia yake safi.
Hapa nilisahau kueleza pesa aliyonipa sikununulia simu aliniambia nisubiri atafanya mpango , kule kwa bi mkubwa sasa yule mama baadae akaja na boksi akalifungua ndani kulikua na Ipodi zile za mziki pamoja na simu za kisasa smartphone nilifurahi sana na nilitamani muda huo niage sababu kule kazini wakawa wananipiigia sana simu nikawa nadanganya foleni kumbe akuna kitu.
Niliwaambia kuna sehemu nilipita sasa narudi ndio foleni na hata kaz yenyewe niliona muda wowote napiga chini sababu zile ni kazi ambazo Mara nyingi watu mipango ikifeli ndio uingia uko
Pale nikapewa chakula tukala fresh stor kidogo ikabidi niage wakanisindikiza tukaachana mi nika elekea nyumbani ile nimefika cha kwanza nikampigia yule mwenzangu aje aniunganishe maana sikua mjuzi wa smartphone akaja akaunga pamoja na Viber fasta nikafanya mchakato nikamcheki yule Dada nikaweka video call sasa tukawa tunaonana mawasiliano yalizidi
kuna siku akaniuliza una paspoti? Mi nikamwambia sina ukicheki siku zote safar zangu za nje magumashi tu.
Akanifanyia tena mpango alituma pesa kwajili ya paspoti ya kusafiria muda huo nshakua mwenyeji kwenye kutoa hela sikusumbuka ila kwenye kupata pasipoti ndio nilimtafuta mtu anisaidie barua na maombi na vitu vingine mwisho nikafika wizara ya uhamiaji pale kukamilisha na siku ilifika nilienda pale uhamiaji nikakuta jina langu nikaonesha risiti nikapewa kwa Mara ya kwanza nashika paspoti ya kusafiria nje ya nchi niliweka mfukoni lakini nilikua muangalifu nayo sana isije kudondoka au kuporwa na kibaka maana wao awana hasara.
Akaja tena akanitumia pesa nyingine hii aliniuliza kama naweza kuendesha gari ki ukweli kwa kipindi hicho ilikua baiskeli tu ndio najua sio gari wala pikpik ivyo iyo pesa alinipa nijifunze gari nilitafuta chuo cha mafunzo ya udereva chuo flani kipo hapa dar nikaanza kupata mafunzo nilikua na wanafunzi wengine Ila binafsi nilikua na bidii sana ya kujifunza gari muda mwingne nipo road naweka gia kama mzoefu mpaka nahacha njia sema yule mwalimu nae alikua vizuri kuni control miezi michache nilimaliza nikapewa uangalizi muda mchache hatimae nikaitimu na kupewa leseni.
Ila nilipiga picha ya paspoti na leseni nikamtumia yule mwanamke akaziona Ila akaniambia sasa inabidi niende kule Denmark.
Yule Dada alintumia maelezo ivi nika scani yani kama njia au vielelezo nitakapo taka anza safari nipeleke ayo maelezo sikua na uzoefu wa izo safari ila sasa nikaanza mipango ya safari changamot ilinikuta nilipokwenda ubalozi wa Denmark Yale maelezo yangu na lile karatasi kama njia vikawa sieleweki nikaambiwa niende ubalozi wa Norway baadae Sweden kilichoonekana sina vigezo maalumu vya kuingia kule kwamba nakwenda kufanya nini na yule Dada akunipanga vizuri kwaiyo maelezo yangu yakawa aya toshelezi na hata lile karatasi lilikua lugha ya kingereza Mimi pia nilikua sielewi mule zaidi kimeandikwa nini .
Lakini baadae wakasema sijui niende Uganda kwenye kambi ya wakimbizi nikapate utambulisho utakao Fanya niende uko na kuonana na uyo mtu au pia kama nataka kuishi nae.
Mimi sikua mkimbizi ikumbukwe ina maana yule mwanamke anaishi kule Denmark lakini yupo chini ya shirika la kusimamia wakimbizi ikabidi niulizie viza nyingne zinapatikanaje wakaniambia zipo za miezi mitatu n.k Ila lazima ulete bank statement uwe na pesa ya kutosha , hotel booking pia zile njia za yule mwanamke zili feli .
Ikabidi niende kwa washkaji nikawaeleza mkasa mzima kuna mmoja alikua anajua izi ishu akasema kwanni nisimtumie mwaliko wa kuja bongo? Ilo likawa wazo zuri ikabidi nifanye ivyo nilituma mualiko kwake ila kwa kusaidiwa ilikua njia ya email ikiambatana na copy ya paspoti yangu, ule mwaliko ulienda na akaupata akapeleka ubalozi wa Denmark ambao kwa kipindi icho walikua wanatoa viza ya kuja uku alienda ila palikua na maombi mengi yani foleni kwa maelezo yake yeye akaambiwa asubiri kwanza baadae nikapigiwa simu na wizara kuuzlizwa kuhusu yule Dada nikawaeleza hali halisi palikua na maswali mengi ila walicho niambia uyu mtu anakuja uko ila atakua chini yangu sasa kama litampata baya au Mimi gaidi labda ndio nta husika basi nikawauliza anakuja lini wakasema inabidi asubiri sababu pana foleni zingne kabla yake OK.
Sasa yakaanza maajabu kumbe yule mwanamke viza akaipata alafu akuniambia wakati huo yule mama tuna wasiliana sikuelewa kumbe ulifanyika mchezo yule mama alikua ana ndugu uku mdada na mshkaji aka muunganisha wakawa wanawasiliana kwamba anapokuj uku Tanzania astukize ina maana wata ulizia kwangu ki ujanja mpka wafike sababu ya kufanya ivyo ni kwamba alimwambia isije kua ana mwanamke alafu akawa anatuzingua mjanja tu wa mjini.
yule mama pia kwa kipindi icho tayari alisha ondoka muda kurudi Denmark, Uyu Dada wa uku wakapanga sasa na kaka yake atakapokuja mambo yakiwa safi akikamilisha zoezi lake basi wafanye mpango wa ndoa kati ya Mimi na yule mwanamke tufunge ndoa kiserikali ili sasa nikhitaji kwenda kule kwake tayari ntakua na kigezo .
Mwisho wa siku nikawa simpati online kila nikimcheki kumbe tayari yupo kwenye pipa anakuja bongo mi sijui kinacho endelea lakini hapo ndugu zangu niliuza kitanda changu ili nipate bima ya viza niliambiwa ubalozini inabidi niwe nayo yule demu nilimwambia ili swala akasema mambo ayajamkalia vizuri ye ataweka sawa nihangaikie Mimi ilinigharimu karibu laki mbili hapa niliiza kitanda godoro nikaweka chini na kingine tayari aliniambia aya maisha utaondoka nayo lakini palikua na vipengele vingi mpaka nikapigika kuna siku nilimfata rafiki yangu sule kama wadau mnakumbuka nilizamia nae meli akanywa pombe flani ivi yakamtoka manundu mwilini ndio uyo alinisaidia laki moja nikiwa kwenye mazingira ayo.
kumbe uyu ndugu wa yule mama akafanya mpango wa kumtafutia uyu mwanamke mwanaume aisee lakini mazingira ayo yalikua ya kumpiga pesa yule demu pesa ya kitanzania alikua anaijua elfu kumi tu mwisho wa siku alikuja TZ kwa siri ila kilicho nisaidia kuna rafiki yangu alikuaga uko Denmark saizi yupo shinyanga Man P niliwai mtambulisha uyu Dada wakawa wanawasiliana vizuri ila siku iyo alinipigia simu akaniambia Latino yule Shem yupo uko ila umefichwa aliniambia nisikwambie ni siri wanataka wakushtukize kwaiyo jipange.
Kuna siku nikapigiwa simu niende kwao na yule mama ila kule alikua ndugu wa yule mama nilienda kweli nafika namkuta tayari kumbe ana siku ya saba alikuja na mtoto yule mtoto ananifahamu sababu ya vile tulivyokua tunawasiliana akanikumbatia fresh ila lugha sasa alikua anaongea yule dogo ikawa chenga kwangu, yule demu ndio Mara ya kwanza tunaonana tukapiga story akaingia ndani akaniletea zawadi mojawapo ni cheni alafu alinipa na laptop hii alimletea shemej ake na mdogo angu mimi mambo yakawa ivyo na nikawa sasa nakuja pale na kurudi siku iyo nimeenda nikakuta yule demu kama ana usingizi ivi ile nasogea nikasikia arufu ya pombe kumbe kipindi kile tunachati akuniambia kama anatumia pombe tena Kali alafu mpaka sigara anavuta nilijua mstarabu kumbe alikua muhuni .
Nikamuuliza vipi mbona ivyo pombe akasema hua tunatoka na uyu Dada na ana kaka ake ndio wananipelekaga club hapo alificha kumbe kuna jamaa mwingne ndio alofanyiwa mpango na yule mama .
sasa nikashangaa niliambiwa Mimi ndio ntamtembeza na vitu vingne hii sasa inakuaje ? Wameteuliwa watu wengne nikaona poa ila sasa nikaelewa kitu,
siku iyo tukapanga tutoke ndio nikamuona na uyo mshikaji ana mtembezaga sio muhusika wa kumuoa tukatoka mpaka baa flani ivi pembeni pana hoteli tupo kule tuka muacha jamaa anapiga pombe mi nikawa na yule demu hotelini chumbani nikawa naongea nae akaniambia kwamba yule mama wa kwanza kabisa kuchati nae kamtafutia mchumba mwingne ina maana kumbe usinich ulianza toka kwa yule mama na alimwambia Mimi naonekana muhuni mlugha lugha wa mjini alafu muogo ujanipenda kwa zati
nikauliza huo uongo upi akapayuka kama umenipenda kwa zati badiri dini nikashangaa aya mambo mbona atukuongea mwanzo nikamwambia sikuelewi umekuja upo bize na watu wengne alafu unaleta ishu zingne izi umekuaje mbona unaniletea habar ambazo azipo akasema basi nikupe penzi tu utoe kinyongo alafu baada ya hapo niache niendelee na mambo yangu kwamba tuagane.
Hasa hapa ndugu zangu hisia unapata wapi wakati mawazo yangu yalikua kupitia uyu demu basi ntabadilisha maisha na nikienda uko mbele ntatoboa nikaona uyu anijui alafu Mimi sio mtu wa kutaka sana sex nikamwambia tayari nshapoteza baazi ya vitu alafu hii ishu tayari watu wengi wanaijua niliwapa taarifa Leo nawa ambiaje na kipindi kile mwanzo nilikua na ushamba flani nimepata demu mbele kutangaza sana Leo yanakua aya niliwaza mengi nikienda kule Denmark nifanye bidii nipate leseni kubwa nifanye mengi ki ujumla nikaona ndoto zangu zinapotea tulitoka nje alafu nilikua toafuti sana ila alikua akinituliza lakini sikua vile tena baadae yeye alirudi na yule jamaa mi nililala pale na kile chumba tulilipa alafu maongez ya muda mfupi tu nikaamua nilale pale.
Siku ya pili sasa nimeenda kule kwa demu nika mkuta tena yupo pombe alafu palikua na Dada mwingne sikua na mazoea nae ilibidi nimuulize tu yule Dada.
yule Dada kaka mi nakuonea huruma sana hapa kuna mtu anakujaga mwanaume ndio kafanyiwa mpango amuoe na uyo nae mtu wa pombe sana ivyo na yule demu wana endana ndio mana una mkuta kalewa kila ukija ukicheki mi pombe sinywi ina maana demu nae aliona iyo ishu atuendani.
Alichoniambia yule Dada kaa fikiri sababu mwenyewe una hakili
basi nikawaza kitu kimoja uyu demu nimfanyizie sababu tayari hapo ata ile kaz ya ulinzi nilisha acha ujue kwamba naenda Fanya maisha mengne Leo inakuaje lakini wale viongozi waliniambia kama nikihitaji kurudi muda wowote niende
Nikawaza nimlipoti uongozini uko ili aondoke lakini nikaona aifai nilicho amua siku iyo nikampigia simu nikamwambia mkataba wetu wewe na Mimi umeishia hapa ila kwa sasa jilinde jichunge muda wako ukiisha nenda kwa usalama mim sitaki matatizo na sihitaji lingine toka kwako sababu upo hapa kwajli ya Mimi yule bi mkubwa kumbe akamwmbia siwez Fanya lolote na akutishi kitu uwezi amini yule mama ndio aliongea ayo .
Uamuzi wa mwisho nikamblock rasmi yule mama na yule demu kwote ila nilikuja pata taarifa aliondoka na uyo jamaa kwenda Denmark iyo ilikua nafasi yangu lakini ikachukuliwa na mtu mwingne kiwepesi na ukicheki lile jambo nimelipigania muda mrefu sana ki ukweli sikua sawa kiakili kwa kilichotokea.
ilibidi nirudi kwanza shamba kwa mzee wangu kisarawe kule wakati huo yupo kwenye uhai wake kule kijiini nikamuomba anipe shamba nimlimie ili nikiondoka niwe nimemwekea mazingira mazuri ni kama nilijipa azabu tu .
Nililima kwa mzee kule Ila ilikua muda mwingne zinakuja zile hisia za lile jambo kwamba sasa ivi nisingekuepo hapa lakini niliona aikua bahati yangu,
kuna siku nilikua na noa panga na tupa sasa Yale mawazo kichwani lile panga likanikata kidoleni kuwaza sana .
ilichukua miezi sita pale kwa mzee mpka kumaliza kilimo na hatimae nikaondoka na kurudi tena mjini nije kufanya harakati zingne ....................
Tutarejea
Kile kipigo cha madiba kule bondeni du ila aina noma ndio mpira Leo tumepatikana
Du hatari mzeeHichi kipande Cha kukosa zari KWA mtoto wakike kimeniuma sanaa....niliwai kumfukuzia dem mmoja hakua mzuri Wala nini....tuli kua Just friends...
Ila kilicho kuja kutokea nilipo mu approach alinitosa
nilijichunguza sanaa badae sanaa nilikuja kugundua alinikataa kwa sababu yeye alikua mtu wa tungi na bangi alaf mm ni good behaved...
BadoImeisha?
Ndio ile ileHivi hii ni stori ile ile ya latino au imebadilika?