Latino na harakati za kuzamia ughaibuni mpaka kutoswa baharini

Mkuu usimuliaji wako huu ni kama kweny LEGEND OF THE SEEKER.

Yaan ukikamilisha mission Moja Ina ibuka nyingine... ..
 
Hivi hii sio kweli maanake hii story uongo ehh? Isije kuwa chai!!
 
Tuendelee
Baada ya kukutana na yule mama aliniambia niingie kwenye gari ina maana tulitoka pale na kuelekea nyumbani kwake tumefika tukatambulishana vizuri na familia yake safi.
Hapa nilisahau kueleza pesa aliyonipa sikununulia simu aliniambia nisubiri atafanya mpango , kule kwa bi mkubwa sasa yule mama baadae akaja na boksi akalifungua ndani kulikua na Ipodi zile za mziki pamoja na simu za kisasa smartphone nilifurahi sana na nilitamani muda huo niage sababu kule kazini wakawa wananipiigia sana simu nikawa nadanganya foleni kumbe akuna kitu.

Niliwaambia kuna sehemu nilipita sasa narudi ndio foleni na hata kaz yenyewe niliona muda wowote napiga chini sababu zile ni kazi ambazo Mara nyingi watu mipango ikifeli ndio uingia uko
Pale nikapewa chakula tukala fresh stor kidogo ikabidi niage wakanisindikiza tukaachana mi nika elekea nyumbani ile nimefika cha kwanza nikampigia yule mwenzangu aje aniunganishe maana sikua mjuzi wa smartphone akaja akaunga pamoja na Viber fasta nikafanya mchakato nikamcheki yule Dada nikaweka video call sasa tukawa tunaonana mawasiliano yalizidi
kuna siku akaniuliza una paspoti? Mi nikamwambia sina ukicheki siku zote safar zangu za nje magumashi tu.
Akanifanyia tena mpango alituma pesa kwajili ya paspoti ya kusafiria muda huo nshakua mwenyeji kwenye kutoa hela sikusumbuka ila kwenye kupata pasipoti ndio nilimtafuta mtu anisaidie barua na maombi na vitu vingine mwisho nikafika wizara ya uhamiaji pale kukamilisha na siku ilifika nilienda pale uhamiaji nikakuta jina langu nikaonesha risiti nikapewa kwa Mara ya kwanza nashika paspoti ya kusafiria nje ya nchi niliweka mfukoni lakini nilikua muangalifu nayo sana isije kudondoka au kuporwa na kibaka maana wao awana hasara.
Akaja tena akanitumia pesa nyingine hii aliniuliza kama naweza kuendesha gari ki ukweli kwa kipindi hicho ilikua baiskeli tu ndio najua sio gari wala pikpik ivyo iyo pesa alinipa nijifunze gari nilitafuta chuo cha mafunzo ya udereva chuo flani kipo hapa dar nikaanza kupata mafunzo nilikua na wanafunzi wengine Ila binafsi nilikua na bidii sana ya kujifunza gari muda mwingne nipo road naweka gia kama mzoefu mpaka nahacha njia sema yule mwalimu nae alikua vizuri kuni control miezi michache nilimaliza nikapewa uangalizi muda mchache hatimae nikaitimu na kupewa leseni.
Ila nilipiga picha ya paspoti na leseni nikamtumia yule mwanamke akaziona Ila akaniambia sasa inabidi niende kule Denmark.
Yule Dada alintumia maelezo ivi nika scani yani kama njia au vielelezo nitakapo taka anza safari nipeleke ayo maelezo sikua na uzoefu wa izo safari ila sasa nikaanza mipango ya safari changamot ilinikuta nilipokwenda ubalozi wa Denmark Yale maelezo yangu na lile karatasi kama njia vikawa sieleweki nikaambiwa niende ubalozi wa Norway baadae Sweden kilichoonekana sina vigezo maalumu vya kuingia kule kwamba nakwenda kufanya nini na yule Dada akunipanga vizuri kwaiyo maelezo yangu yakawa aya toshelezi na hata lile karatasi lilikua lugha ya kingereza Mimi pia nilikua sielewi mule zaidi kimeandikwa nini .
Lakini baadae wakasema sijui niende Uganda kwenye kambi ya wakimbizi nikapate utambulisho utakao Fanya niende uko na kuonana na uyo mtu au pia kama nataka kuishi nae.
Mimi sikua mkimbizi ikumbukwe ina maana yule mwanamke anaishi kule Denmark lakini yupo chini ya shirika la kusimamia wakimbizi ikabidi niulizie viza nyingne zinapatikanaje wakaniambia zipo za miezi mitatu n.k Ila lazima ulete bank statement uwe na pesa ya kutosha , hotel booking pia zile njia za yule mwanamke zili feli .

Ikabidi niende kwa washkaji nikawaeleza mkasa mzima kuna mmoja alikua anajua izi ishu akasema kwanni nisimtumie mwaliko wa kuja bongo? Ilo likawa wazo zuri ikabidi nifanye ivyo nilituma mualiko kwake ila kwa kusaidiwa ilikua njia ya email ikiambatana na copy ya paspoti yangu, ule mwaliko ulienda na akaupata akapeleka ubalozi wa Denmark ambao kwa kipindi icho walikua wanatoa viza ya kuja uku alienda ila palikua na maombi mengi yani foleni kwa maelezo yake yeye akaambiwa asubiri kwanza baadae nikapigiwa simu na wizara kuuzlizwa kuhusu yule Dada nikawaeleza hali halisi palikua na maswali mengi ila walicho niambia uyu mtu anakuja uko ila atakua chini yangu sasa kama litampata baya au Mimi gaidi labda ndio nta husika basi nikawauliza anakuja lini wakasema inabidi asubiri sababu pana foleni zingne kabla yake OK.

Sasa yakaanza maajabu kumbe yule mwanamke viza akaipata alafu akuniambia wakati huo yule mama tuna wasiliana sikuelewa kumbe ulifanyika mchezo yule mama alikua ana ndugu uku mdada na mshkaji aka muunganisha wakawa wanawasiliana kwamba anapokuj uku Tanzania astukize ina maana wata ulizia kwangu ki ujanja mpka wafike sababu ya kufanya ivyo ni kwamba alimwambia isije kua ana mwanamke alafu akawa anatuzingua mjanja tu wa mjini.
yule mama pia kwa kipindi icho tayari alisha ondoka muda kurudi Denmark, Uyu Dada wa uku wakapanga sasa na kaka yake atakapokuja mambo yakiwa safi akikamilisha zoezi lake basi wafanye mpango wa ndoa kati ya Mimi na yule mwanamke tufunge ndoa kiserikali ili sasa nikhitaji kwenda kule kwake tayari ntakua na kigezo .
Mwisho wa siku nikawa simpati online kila nikimcheki kumbe tayari yupo kwenye pipa anakuja bongo mi sijui kinacho endelea lakini hapo ndugu zangu niliuza kitanda changu ili nipate bima ya viza niliambiwa ubalozini inabidi niwe nayo yule demu nilimwambia ili swala akasema mambo ayajamkalia vizuri ye ataweka sawa nihangaikie Mimi ilinigharimu karibu laki mbili hapa niliiza kitanda godoro nikaweka chini na kingine tayari aliniambia aya maisha utaondoka nayo lakini palikua na vipengele vingi mpaka nikapigika kuna siku nilimfata rafiki yangu sule kama wadau mnakumbuka nilizamia nae meli akanywa pombe flani ivi yakamtoka manundu mwilini ndio uyo alinisaidia laki moja nikiwa kwenye mazingira ayo.
kumbe uyu ndugu wa yule mama akafanya mpango wa kumtafutia uyu mwanamke mwanaume aisee lakini mazingira ayo yalikua ya kumpiga pesa yule demu pesa ya kitanzania alikua anaijua elfu kumi tu mwisho wa siku alikuja TZ kwa siri ila kilicho nisaidia kuna rafiki yangu alikuaga uko Denmark saizi yupo shinyanga Man P niliwai mtambulisha uyu Dada wakawa wanawasiliana vizuri ila siku iyo alinipigia simu akaniambia Latino yule Shem yupo uko ila umefichwa aliniambia nisikwambie ni siri wanataka wakushtukize kwaiyo jipange.

Kuna siku nikapigiwa simu niende kwao na yule mama ila kule alikua ndugu wa yule mama nilienda kweli nafika namkuta tayari kumbe ana siku ya saba alikuja na mtoto yule mtoto ananifahamu sababu ya vile tulivyokua tunawasiliana akanikumbatia fresh ila lugha sasa alikua anaongea yule dogo ikawa chenga kwangu, yule demu ndio Mara ya kwanza tunaonana tukapiga story akaingia ndani akaniletea zawadi mojawapo ni cheni alafu alinipa na laptop hii alimletea shemej ake na mdogo angu mimi mambo yakawa ivyo na nikawa sasa nakuja pale na kurudi siku iyo nimeenda nikakuta yule demu kama ana usingizi ivi ile nasogea nikasikia arufu ya pombe kumbe kipindi kile tunachati akuniambia kama anatumia pombe tena Kali alafu mpaka sigara anavuta nilijua mstarabu kumbe alikua muhuni .
Nikamuuliza vipi mbona ivyo pombe akasema hua tunatoka na uyu Dada na ana kaka ake ndio wananipelekaga club hapo alificha kumbe kuna jamaa mwingne ndio alofanyiwa mpango na yule mama .
sasa nikashangaa niliambiwa Mimi ndio ntamtembeza na vitu vingne hii sasa inakuaje ? Wameteuliwa watu wengne nikaona poa ila sasa nikaelewa kitu,
siku iyo tukapanga tutoke ndio nikamuona na uyo mshikaji ana mtembezaga sio muhusika wa kumuoa tukatoka mpaka baa flani ivi pembeni pana hoteli tupo kule tuka muacha jamaa anapiga pombe mi nikawa na yule demu hotelini chumbani nikawa naongea nae akaniambia kwamba yule mama wa kwanza kabisa kuchati nae kamtafutia mchumba mwingne ina maana kumbe usinich ulianza toka kwa yule mama na alimwambia Mimi naonekana muhuni mlugha lugha wa mjini alafu muogo ujanipenda kwa zati
nikauliza huo uongo upi akapayuka kama umenipenda kwa zati badiri dini nikashangaa aya mambo mbona atukuongea mwanzo nikamwambia sikuelewi umekuja upo bize na watu wengne alafu unaleta ishu zingne izi umekuaje mbona unaniletea habar ambazo azipo akasema basi nikupe penzi tu utoe kinyongo alafu baada ya hapo niache niendelee na mambo yangu kwamba tuagane.

Hasa hapa ndugu zangu hisia unapata wapi wakati mawazo yangu yalikua kupitia uyu demu basi ntabadilisha maisha na nikienda uko mbele ntatoboa nikaona uyu anijui alafu Mimi sio mtu wa kutaka sana sex nikamwambia tayari nshapoteza baazi ya vitu alafu hii ishu tayari watu wengi wanaijua niliwapa taarifa Leo nawa ambiaje na kipindi kile mwanzo nilikua na ushamba flani nimepata demu mbele kutangaza sana Leo yanakua aya niliwaza mengi nikienda kule Denmark nifanye bidii nipate leseni kubwa nifanye mengi ki ujumla nikaona ndoto zangu zinapotea tulitoka nje alafu nilikua toafuti sana ila alikua akinituliza lakini sikua vile tena baadae yeye alirudi na yule jamaa mi nililala pale na kile chumba tulilipa alafu maongez ya muda mfupi tu nikaamua nilale pale.
Siku ya pili sasa nimeenda kule kwa demu nika mkuta tena yupo pombe alafu palikua na Dada mwingne sikua na mazoea nae ilibidi nimuulize tu yule Dada.
yule Dada kaka mi nakuonea huruma sana hapa kuna mtu anakujaga mwanaume ndio kafanyiwa mpango amuoe na uyo nae mtu wa pombe sana ivyo na yule demu wana endana ndio mana una mkuta kalewa kila ukija ukicheki mi pombe sinywi ina maana demu nae aliona iyo ishu atuendani.
Alichoniambia yule Dada kaa fikiri sababu mwenyewe una hakili

basi nikawaza kitu kimoja uyu demu nimfanyizie sababu tayari hapo ata ile kaz ya ulinzi nilisha acha ujue kwamba naenda Fanya maisha mengne Leo inakuaje lakini wale viongozi waliniambia kama nikihitaji kurudi muda wowote niende
Nikawaza nimlipoti uongozini uko ili aondoke lakini nikaona aifai nilicho amua siku iyo nikampigia simu nikamwambia mkataba wetu wewe na Mimi umeishia hapa ila kwa sasa jilinde jichunge muda wako ukiisha nenda kwa usalama mim sitaki matatizo na sihitaji lingine toka kwako sababu upo hapa kwajli ya Mimi yule bi mkubwa kumbe akamwmbia siwez Fanya lolote na akutishi kitu uwezi amini yule mama ndio aliongea ayo .
Uamuzi wa mwisho nikamblock rasmi yule mama na yule demu kwote ila nilikuja pata taarifa aliondoka na uyo jamaa kwenda Denmark iyo ilikua nafasi yangu lakini ikachukuliwa na mtu mwingne kiwepesi na ukicheki lile jambo nimelipigania muda mrefu sana ki ukweli sikua sawa kiakili kwa kilichotokea.

ilibidi nirudi kwanza shamba kwa mzee wangu kisarawe kule wakati huo yupo kwenye uhai wake kule kijiini nikamuomba anipe shamba nimlimie ili nikiondoka niwe nimemwekea mazingira mazuri ni kama nilijipa azabu tu .
Nililima kwa mzee kule Ila ilikua muda mwingne zinakuja zile hisia za lile jambo kwamba sasa ivi nisingekuepo hapa lakini niliona aikua bahati yangu,
kuna siku nilikua na noa panga na tupa sasa Yale mawazo kichwani lile panga likanikata kidoleni kuwaza sana .
ilichukua miezi sita pale kwa mzee mpka kumaliza kilimo na hatimae nikaondoka na kurudi tena mjini nije kufanya harakati zingne ....................
Tutarejea

Kile kipigo cha madiba kule bondeni du ila aina noma ndio mpira Leo tumepatikana
 
Hichi kipande Cha kukosa zari KWA mtoto wakike kimeniuma sanaa....niliwai kumfukuzia dem mmoja hakua mzuri Wala nini....tuli kua Just friends...
Ila kilicho kuja kutokea nilipo mu approach alinitosa
nilijichunguza sanaa badae sanaa nilikuja kugundua alinikataa kwa sababu yeye alikua mtu wa tungi na bangi alaf mm ni good behaved...
 
Du hatari mzee
 
Hivi hii ni stori ile ile ya latino au imebadilika?
 
Tuendelee
Baada ya kutoka kijijini kwa mzee nikarudi tena mjini na akili mpya kabisa kumbuka nilibaki na godoro tu kwa hasira nalo nikauza alafu ishu ya kulala aikua tabu nikawa na lala kwa ndugu ila nikafanya harakati upya na mshkaji wangu mmoja ivi kwajili ya kurejea SOUTH AFRICA.
Uyo mshkaji alikuja bongo ila katokea south Africa lakini mtanzania ndio ishu zake anapiga uko jamaa aliniambia tunaenda Afrika kusini ila tukiwa na mzigo yaani madawa au unga cocaine mpaka sasa yupo huko na yeye alikua mtu wa kupaa sana na mwewe ndege kwenda nchi toafauti tofauti kama Brazil , ureno sometimes uturuki n.k
Mi nikamuuliza huo mzigo tunaluka nao vipi akasema atuondoki na ndege isipokua ni gari tutapita Zambia uko mpaka maeneo alafu mi ntajua tutafanya nini kuvuka

Tulichofanya tukaingia dukani tukachukua raba alishauri viatu vyenye soli ndefu air Jordan rebook au puma mi nikachukua air Jordan mnyama yule kilichofanyika ile soli ikatolewa alafu ikachimbwa kule chini ikawekwa mzigo alafu ikarudishwa kwenye kiatu nikavaa chuma kipo on kimesimma nikaona hapa Fresh, mzigo mwingne tukapakia kwenye laptop hapa watu watajiuliza kwenye laptop unawekaje ipo ivi betri zinatolewa alafu ile sehemu panawekwa unga ina maana laptop aziwaki hapo hatari sana mbinu zinazaliwa kila siku.

Mzigo mwingne tukaweka ndani ya mpira wa miguu ule mpira mpya unatolewa kigozi sehemu moja tunapakia kisha kinaludisshwa kwa ustadi sana alafu tunaweka kwenye nyavu yake unaonekana mpya kabisa .
Wote tumepakia mzigo safi alafu nikatinga traki kuonesha ni mwana mazoez alafu nipo na mpira vile kiroo safi na mwana tukaondoka Tz mpaka Zambia mpakani tulikua jioni ivi tukakamilisha ishu za boda pale tukavuka mpaka na hatimae south Africa cape town kwa madiba
((( pale tulipo pokea kipigo cha mbwa koko kutoka kwa kaizer kitaeleweka kwa mkapa baazi tumeelewana)))

Tuendelee utani kidogo
tukaingia south pale cap town mountain table
kuna mlima juu upo kama meza ivi tukaelekea western London kuna bichi moja inaitwa kids bich tukatulia hapo na kufanya ishu za kuondoa ile mizigo na kuifikisha eneo husika ila kila kitu maswala ya pesa alikua ana shughulikia yule mwana na hata mzigo ulipowasilishwa pesa akapokea yeye.
Hapo tukaanza maandalizi ya safari nyingne kuelekea ureno kufata unga tena kupitia Angola ila sasa kwa ndege tulitoka south mpaka Angola alafu tukaingia Meli pale Angola sio safari za kimagumshi yani hapo ni halali tiketi safi sio kuzamia tulikwenda tukapita siela leone , alafu Morocco kuna tu miji pale tulipita mji wa safi alafu Casablanca badae aljadina sijui ile na mpaka Rabat na hatimae Ureno kwa njia ya maji.

pale ureno palikua na mabosi wakubwa ambapo mwana ndio alikua anafanya nao kazi ina mana tuchukue mzigo kisha turudi south ila sasa kwa ndege tulikutana na watu wengne ambao wapo kwenye harakati izo pia alikua demu mmoja ivi katokea Rabati mzaliwa wa Morocco ndio akawa ana nionesha mitaa kunitembeza uku tukisubiri mzigo ambao ulikua unatokea Brazil .
Mzigo ukawasili baadae na mshkaji akaandaliwa safari ila sasa jamaa aliniambia Mimi inabidi nibaki pale yeye anaondoka sikujua lengo ni nini na pale nipo tu nakula bata nikaona poa aliniambia yeye akai ndani ya wiki anarudi anapeleka mzigo na kugeuka mi nikabaki pale na ile kampani na yule demu fresh kumbe ule mzigo alio ondoka nao mshkaji ni Mali kauli ivyo Mimi nilibaki kama bondi nipo chini ya uangalizi na muangalizi ndio alikua uyo demu lakini sikutambua chochote kwa muda huo maana niliona nipo safi tu kila kitu kinaenda sawa.
Ila kama ikitokea mshkaji kaharibu katika huo mzigo au kaenda mazima asirudi basi wao watanishikilia Mimi na watakua na maamuzi ya kufanya chochote kwangu ila ndio ivyo sikua naelewa kitu.

Jamaa aliondoka na mzigo ila safari hii alimeza mzigo ulikua tumboni akapanda ndege toka ureno kuitafuta Zambia nieleze kidogo mzigo wa madawa kumeza tumboni ili ushtukiwe Mara nyingi ni njia ya kuhisi sio zile mashine za kuscan zile kuona ni ishu mzigo ukiwa tumboni,, ndio mana ukihisiwa tu unapelekwa chooni au kulazimishwa kunywa chai ya moto
Pia kwa mbebaji hata matumizi ya simu yanapungua sababu pale kwenye viwanja vya ndege kuna watu wapo kwenye vitengo ivyo vya madawa na ni wachunguzi kwa kuhisi yani kwa kumwangalia tu mtu ivi wanahisi uyu labda ana wasi wasi ivyo wanamtilia mashaka mfano sana watu wanaotoka America ya kusini maana ndio chimbo la madawa uko ...................

Wakuu Tutaendelea siko vizuri ki afya
 
Tuendelee
Tuje kwenye watu wa jamii ya Asia hawa Mara nyingi mizigo ya madawa ya kulevya awamezi hawa huwa wanaweka kwa njia ya aja kubwa mtu anainama au ana lala ivi alafu mzigo unachomekwa kwenye tundu la aja kubwa karibu kilo ya mzigo inaingia kwenye mfuko unapangwa vizuri,
Kwenye li mfuko alafu wanavaa ma pajama yale ule mzigo unakua na kikamba flani kinabaki nyuma
akifika anainama alafu mtu anavuta lile li mfuko mzigo unatoka tunduni kibongo bongo uku tunasema hawana marinda ayo yote katika harakati za kutafuta pesa.
Pia upande wa wanawake hawa nao wanaweza wasimeze mzigo wenyewe muda mwingne wanatumia sehemu ya aja ndogo kuweka ila anaweka pale anapokua muhezini alafu anavaa ile ped apo safi na zile mashine kitu kilicho zungukwa na damu sio laisi kung'amua ukiacha chuma apo mzigo unafika.
Izi njia hupendelewa sana sababu kumeza watu wanaona athari yake ni kubwa ndio wanatumia njia izi za kupakia kwenye matundu ya aja ndogo na kubwa na kwa mwanamke sometimes mpaka maji hua yanachuruzika kutoka hukeni humu pembeni ya mapaja ivyo yale mapajama yanasaidia kuto onekana.
Ipo pia njia nyingine ambayo linachukuliwa begi sehemu zile za nyama mule kwenye begi zinatolewa alafu unapkiwa mzigo alafu linachukuliwa karatasi lile la xray ambazo hutumika hospital inawekwa juu pale ya mzigo inachukuliwa mashine ya ku scan inapima kama mzigo unaonekana izi mashine ambazo zipo airpot au kwenye viwanja vya ndege watu wanazo ndani wanatumia niliiyona hii ureno
Ipo njia ya samaki, pia matunda mfano tikiti maji wengne njia ya mipira hii ya kuchezea zipo nyingi ndio mana vita ya madawa ya kulevya kuimaliza ni ngumu sana wale jamaa kila siku wanabuni njia mpya pia wana pesa wanaenda na technologia na hutumia akili sana kuwazidi serikali husika .
Tuludi kwa waweka mzigo kwenye njia ya aja kubwa ishu ya msosi watu watajiuliza wakitaka kujisaidia hapo vipi ipo ivi mtu anaechukua mzigo kwa njia ya aja kubwa atumii vyakula vigumu yeye ata tumia vya kula vyepesi ambavyo vitamfanya

mpaka afike eneo husika bila kujiskia aja.
Mdau ishia kusoma na kujua hapa tu usijidanganye kwenda huko sikuizi teknlojia imekua kubambwa nje nje unakwenda kuozea jela.

Tuendelee na yule mshikaji wangu ambae aliondoka na mzigo na mmi kubaki pale kama bondi bila kujua ikumbukwe baazi ubeba mizigo na hutumia wengne awatumii ivyo kuna ambao wao huvuta ule unga pia kukata haja kubwa wakimeza unga ndio kama mshkaji wakati yupo
Kwenye ndege anavuta kidogo ile hali ikiisha anavuta tena wakati ndege inakwenda inaonekana jamaa katika kuvuta aliongeza dozi alizdisha na ikamzidi Akapoteza fahamu .
Ikatolewa taarifa na wale watu wa huduma walipiga simu airport kwamba ndege sio mda mrefu inatua msumbiji ila ndani kuna mgonjwa
apo msumbiji ndio angetoka na kuitafuta Zambia.
kwa taarifa ya wale jamaa aliamka baada ya siku tatu sijui taarifa walipata vipi sijui nao wana watu wao ambao wanawapa taarifa ndio kazinduka baada ya siku tatu tayari unga ushatolewa tumboni upo mezani, pemben kuna askari alafu ana pingu mkononi.

Kule ureno nilikua na yule Dada tupo maeneo kama kawaida tunazunguka jamaa mmoja akaja wakaongea wakanichukua pale tulitoka ndio wakaja kuniambia kwamba jamaa kazingua kashikwa sasa kwao hasara ni kubwa na wakaniambia kubaki kwangu pale ni bondi jamaa aliniweka sasa nikajua kilicho fanyika wakanipeleka kwenye pipa wakanitumbukiza humo alafu wakafunika tayari nilishapiga pombe kidogo nikapitiwa na usingizi asubuhi nashtuka lile pipa lina nyanyuliwa linaingizwa kwenye gari mi nipo ndani safari mpaka sehemu flani ipo kama jangwa wao ndio wanatumia uko kama mtu akiwazingua, kafanya upuuzi ndio wana enda nae huko na huko palikua na kijumba ndio kama maabara yao ivi yani kuchanganya madawa na unga ndio vinafanyika huko kupanga unga grade one mpaka ya mwisho yani mtu mwenye pesa atapata unga wa daraja juu wenzangu na Mimi pesa ndogo ndio daraja la chini unga ambao unakua na sumu sumu ndio mateja wa mtaani uku wanakula mabaki ya mwisho zinakua na athari sana ndio ile unakuta mtu akikosa ana harisha au ana legea ovyo ishu ka izo kifupi nchi maskini mizigo mingi inakua ya ovyo grade one ndio inakwenda mbele uko kwa madoni wenyewe*******"" ************************
Tutarejea wakuu sijui mpo kweli maana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…