Latino na harakati za kuzamia ughaibuni mpaka kutoswa baharini

Oya tupo babaaa dondosha ma epsod apooo. Iyo ya madawa nmeielewa
 
Tuendelee
Baada ya kufika kule kwenye iyo nyumba ambayo ndio ufanyika aya mambo ya kutengeneza madawa na kuyachanganya na kuyapeki wakanitoa kwenye lile pipa alafu walichofanya Mimi nikawa mwonjaji ya yale madawa inamaana majaribio kwangu wananipa nionje ili waone kama kitu kipo sawa au namna gani vipi.
Lakini pia nilikuta kuna wasichana wapo humo wengi wanafanya kazi ya kupakia kwenye mifuko yale madawa ila wapo uchi wa mnyama sababu ni kwamba awatakiwi kuvaa nguo kuepusha wizi yani kwamba kuvaa nguo wanaweza kuficha kwaiyo ndio mana wakuwa wanakaa uchi wanendelea na kazi, ivyo Mimi nikawa muhonjaji akuna kubisha na walikua watu katili awataki masihara kule kuonja ilifika muda nikanyong'onyea sana lakini najitambua
Pia kuna watu walikuemo humo wanafanya ngono sasa hapa nilibahatika tu kuchungulia humo ndani kulikua na watu tofauti na wengne walikua na camera walikua wana rekodi ,
wakati nipo kule akaja yule Dada ambae nilikua nae muda wote bahat nzuri nikapata nafasi ya kukaribiana nae nikamwambia mpaka saiz sijui inakuaje kwangu alafu hii nchi ndio Mara yangu ya kwanza kuja sijawai kuja huku alafu pasipoti yangu wamechukua inamaana sijui natokaje huku nimeshikiliwa yule Dada akaniambia sikiliza Mimi mwenyewe kwa sasa kufanya kazi hapa nishachoka na hata hawa wanawake unao waona hapa wengi mi ndio nimewaleta huku walikua wanajiuza kwenye makasino huko akasema uyu bosi sio mtu mzuri sasa subiri tutaondoka na Mimi kwa kutoroka kwaiyo subiria wakati tunapanga iyo mipango jamaa wakaja wakanichukua na kuniweka tena kwenye pipa walihisi tuna kitu na yule dada

demu nae baadae walimkata kidole cha mwisho cha mkononi.
Wale jamaa wakanichukua nikiwa kwenye pipa tukaenda sehemu ilikua ni usiku ndio wanafanya huo ukatili tukafika uko kunitoa kwenye pipa nakutana na pande la mtu alafu ana midevu sijui ndio muhuaji wao yupo na chepe ana chimba shimo ila alikwenda chini sana ni juu tu ile sehemu ilikua ngumu sana kuchimbika nikiwa nimefungwa kamba wakanishika na kuniweka kwenye shimo lile ina maana nia yao kumbe kunifukia nikiwa mzima kabisa yani nazikwa hai jamaa walikua hatari na ndio inavyokua kwa watu wenye magenge ya madawa ni katili mno mda wowote ana kubadilikia
Nipo shimoni mule wakaanza kufukia ila wanavyolusha mchanga nikawa najichekecha ivi kwaiyo mchanga unashuka chini mi nakua juu waliendelea mpaka ukawa sasa unazidi ila nilijitaidi walau hata pua tu iwe juu nipate hewa na wale jamaa na usiku ule wakaona tayari alafu wamenifunga kamba natokaje pale lazima ningekufa tu wao waliondoka .

Kumbe bahati nzuri yule Dada alikua anafatilia ule msafara alikuja mpaka pale na pikipk yupo na jamaa wakanichomoa pale shimoni namtazama yule Dada kachakaa ina maana jamaa walishampiga sana.
Sasa pale tuna ondoka kwa usafir wa boti majini na tayari walisha andaa na yule jamaa pale usafir wa hanga isingewezekana paspoti akuna na wale jamaa kama wangerudi na kama wasingenikuta wangeanza kusaka mitahani
Tuliondoka kwa boti izi za wavuvi tulipita vinchi vichache mpaka Angola mji wa Luanda yule Dada pale Angola alikua na jamaa mreno ambae alizaa nae mtoto mmoja ndio tulifikia hapo nilikaa pale kama wiki baadae niliondoka na yule dada alinisindikiza baada ya kutoka hapa nikaingia msumbiji alafu nika elekea Richadbay south Africa.
Lengo nipate taarifa kuhusu yule jamaa yangu ndio nikapata mkasa mzima kwamba jamaa yupo ndani wao walipokwenda kupeleka mahitaji kwa washkaji gerezani msumniji ndio kujua iyo ishu ya mshkaji
wao hutoka south na kwenda msumbiji kupeleka mahitaji kwa jamaa zao walioshikwa
kule nilikaa mda kidogo na nilikuja kubahatika kufanya mawasiliano na jamaa yangu Man P alikua tanzania akaniambia niludi tz kuna ishu ya kusaka vitu vya kale vya mjerumani kuna jamaa anataka ivi vitu vina pesa ndefu kwaiyo njoo tufanye huu mchakato,
Ivyo vitu vya kale kuna lupia izi sarafu ,vikombe pasi majiko kufuli sijui vipo vingi tu vinahitajika akasema niludi tufanye mpango wa kusaka ila kuna msichana wake ana bibi yake anayo sarafu ya kale pia na vitu vingine njoo twende huko.
Nikarudi fresh ila nilimwambia mi sina mda tufanye hii mishe ila mpango wangu ni kurudi tena south Africa basi na jamaa tukapanga tuende kwa uyo msichana na bibi yake ,
nikamuuliza tenaa ivi vitu inasemekana vinakua na ushirikina sana majini mambo ya ajabu inakuaje hapa ? yye akasema endapo mkapata na kumzulumu mtu ndio yanakua ayo lakini azina shida na tayari apo alikua mshikaji mwingine ambae yeye ndio anajua soko lilipo kwa mabosi wenyewe.
Tukatoka na kwenda kwa mzee mmoja ivi alikua na karatasi ambalo ndio lina oroza kubwa ya vile vitu vinavyo hitajika

Jamaa akasema kafanya mawasiliano na yule demu wake na kumwambia ela bibi yake alimpa na kuiweka ndani kwenye nguo aliifunga ile hela ikachana nguo na kutoka kimazingara nje ya nguo mpaka mama yake aliwai muuliza kuhusu ilo swala la nguo kuchanika
akawa sasa kaweka tu sehemu ya wazi na kwa vile ipo ikabid sasa tuende kwa uyu demu
yeye akasema bibi alinipa hii pesa ila alimwambia kama una mwanaume wako itabidi umlete uku ni wakabizi wote ishu ikawa kwenda kukabiziwa tu kwa uyo bibi japo kwa sasa ni marehemu Alisha fariki muda mrefu
inavyo. onekana bibi akua mtu mzuri alikua na ushirikina sasa izi pesa nazo hua na masherti yake .
Tukaenda kwa yule bibi lengo jamaa akabiziwe bibi akasema turudi tena pale baada ya siku 40 kuna mambo ana yakamilisha tukawa na uhakiki alafu na mipango kibao tukijua tunaenda kupata ma milioni ya pesa

wakati tukisubiri kuna kijana anaishi mjini alienda kwa yule bibi kusalimia hua akifika huko anakaa siku kazaa na hua anabeba na vitu kuwa bebea
kule wana ki ukoo yule kijana akafariki ghafla uko uko kijijini na izo siku 40 ndio kwanza siku mbili tayari ilo jambo la msiba linatokea
jamaaa kalala asubuhi aamki kumfata ndani kasha fariki tumepata habari tukaisi labda yule bibi kutoa ile pesa mpaka damu au vipi na je wakiwaza labda Mimi na jamaa tumtoe mmoja inakuaje au labda yule demu kakataa ila wakaamua wamtoe mtu mwingne?.
Zile siku 40 zikafika akatoa ile pesa ila ipo kwenye kitambaa cha sanda sasa sijui ndio sanda aliyo zikiwa marehemu au vipi akampa jamaa ile pesa na yule mwanamke mpaka kwao ile pesa walieweka kitandani siku ya pili asubuhi aipo imepotea ki utata tu ikabidi warudi kwa bibi yule kujua imekuaje na kumpa taarifa
Ajabu yule bibi anajibu pesa isharudi uku kwangu nyie mmeweka kitandani pale sio sehemu safi ni pa chafu airuhusiwi kuwekwa kitandani kwaiyo hapa kuitoa tena mpaka nikamilishe mambo yangu tena.
na yule demu alituambia bibi sio pesa tu anavyo vitu vingine vipo kwenye sanduku kachimbia porin yule jamaa anaejua soko lilipo nae tulikua nae beneti na matumaini kwamba bibi atatoa iyo pesa tusikate tamaa tusubir tena mpaka akamilishe mambo gani sijui anajua Mwenyewe .

Ikabidi tusubiri sasa hapo tukawa watatu na uyu anae jua soko la kuuza ivi vitu na izo sarafu tukasubiri, ghafla tena yule anae jua soko akafariki ghafla tu na ndio tulikua tuna mtegemea kwenye soko uko

inakuaje tukawaza au yule bibi anafanya aya mambo na usikute yule mwanamke ana zingua atuambii ukweli kama vipi tumkatae hapa kutakua na mipango lazima tuwe makini na bibi anaonekana magumashi mengi ................

Tutarejea
 
[emoji109][emoji109][emoji109]
 
Jamaa alianguka akateguka.......mara mkaanza kuparamia mbususu za maporini 😏
 
Tupo hewani tuendelee kusonga tukamalize mkasa

Kutokana na yale magumashi ikabidi tuachane na yule bibi tukaangalia ishu zingne sasa Mimi nilikwenda kwa mama yangu mzazi ambae alitengana na baba alikua kaolewa sehemu nyingne yule baba ambae alikua kamuoa mama sio baba angu mzazi aliniambia kuna msitu una ivo vitu vya kale ambapo hapo kuna makaburi yapo lakini uendi hivi hivi kuna mauza uza wao waliwai kwenda hapo kufagilia makaburi ilikua saa nne tu asubuhi wakapotea makaburi awakuyaona na eneo ni ilo ilo walirudi siku iyo awakufanya kazi.
tukajipanga ikabidi tufike eno husika kufatilia ivyo vitu tumefika eneo lenyewe sasa ilikua ni kwenye kisima ndio kuna izo Mali ila kisimani akuna maji yalisha kauka muda mrefu wakati tunafika pale kwanza tukakuta fuvu la mtu lipo kwenye miti ivi imefungana alafu pembeni kuna nguo zimechakaa zimeliwaliwa na mchwa sisi tukasonga hapo kwenye kisima kuchungulia kuna Giza kuu kisima kirefu alafu ndani kuna kitu kina ng'aa sana kumuuliza mzee akasema hapo pana nyoka mkubwa na ndio mlinzi wa hizo Mali sasa kinachotakiwa apatikane mtaalamu ili tutoe izo Mali bila ivyo aiwezekani .
mtaalamu tuli mpata alikua ni shehe kaja pale yuko full gado na vitabu vyake kwajili ya kusomea na anajiamini sana kana kwamba tayari alishawahi toa ivo vitu akaanza kusoma wakati yupo pale kisimani
sisi kutokana na uoga tukapanda kwenye miti ye tukamuacha chini akapiga kisomo sana muda mrefu bwana ilitoka mizizi chini kule ikaja juu pale kwa shehe na kumvika alafu inamvutia chini kisimani jamaa yetu mmoja sijui alikua na ujasiri gani akaenda msaidia kumvuta ile miziz ikaachia ikarudi chini na yule shehe kukimbia naona zilikua salamu tu kwamba hana uwezo huo wa kumtoa yule nyoka pale zoez likashindikana tukaondoka patupu izi Mali za wajerumani inasemekana kuna uchawi mkubwa sana upo humo kwaiyo kufanikisha ni kazi ngumu na kuna mitego ipo humo kufa ni swala la dakika tu unapoingia uko. unajitoa mwanga na kuna kodi zao maalumu ambazo wenyewe wanajua.

Jamaa flani ivi vijana wakapata taarifa kuhusu lile eneo ni wa huko kijijini wakaona sisi tumekurukupuka na vile tumetoka mjini awajui kitu ngoja twende sisi wakajikoki vizuri ili wakafnye ilo zoezi na wakatafuta mganga awakutak shehe sababu ana soma dua wao waliamini dua ni mpaka mungu aipokee ivyo kwa haraka ni mganga itakua sahihi kwao basi
Yule mganga aka waambia walete kuku wao walikua wa tatu na mganga wa nne wakaenda eneo husika wamefika mganga akaanza manyanga yake piga tambiko mwisho aka waambia uyu kuku tuna muacha hapa tunakaa siku tatu tunakuja kuangalia asipo kuepo ina maana sadaka imekubaliwa na kinachobaki ni Mali kuchukua basi na tukimkuta kuku bado yupo sadaka aijakubaliwa yule kuku akaachwa pale wao wakaondoka kusubiri zile siku ,

Zile siku tatu zikatimia wakarudi pale yule kuku yupo ina maana sadaka aijakubaliwa mganga aka waambia wasubiri tena siku tatu wakasubiri kurudi yupo ambae alitoa yule kuku nyumbani kwake akaamua jambo moja amchukue kuku wake wenzake walimkataza walimwabia uyu kuku keshafanyiwa dawa muache jamaa aligoma na akasema mganga muongo akamtoa pale wakati wana ondoka yule nyoka kule chini alitoka na kuanza kuwafukuza ila walifanikiwa kurudi nyumbani japo msitu upo mbali sana na kijiji ila kuku jamaa alimpoteza msituni wawili walikua wa kijiji kimoja mwingne kjiji kingne wale wawili kwao walipoulizwa akuna walicho kisema baadae mmoja akaumwa akafariki akafata mwingne nae akafariki yule mwenye kuku alie mtoa alibaki mzima mpka sasa ivi yupo lakini ni chizi ilibidi mganga afwatwe kuulizia imekuaje ndio katika kuagua akaona tukio ambalo liliwakuta na waljchofanya hapo ndio taarifa zikasambaa.
uyo aliebaki hua anarudi kule kwenye Mali lile joka linapo jigeuza kuna baazi ya Mali zinatoka sasa jamaa anapkwenda anzikuta anachukua na kuna sehemu anaenda kuuza alafu anaingia kwenye pombe akuna kingne anachofanya zaidi ya kunywea zile hela mpaka zinaisha na kule anako uza huwa wana mkadiria tu akija nazo ndio watu wanamuona yupo na mzigo wa ela anaishia kunywa tu.
Na icho kjiji ni njia ya kuelekea mzaramoni unapita ufulu unaeleka malumbo alafu kuna kijiji kinaitwa paraka alafu unaingia kidugalo cha kanga ni njia ya kuelekea Mzenga hapa katikati kuna vijiji ambako mzee wangu uyo ambae alimuoa mama baada ya kuachana na baba yangu mzazi ndio asili yake hapo na saizi kuna mji kule unaitwa parisi kwa upande wangu Mimi nipo dar hapa nafanya shughuli zangu nyingine za kujipatia kipato nashukuruni nyote.
MWISHO.

Ndugu zanguni Latino mkasa kaumaliza hapa Mimi pia nashukuru kwa kumuwakilisha hapa kwa kuweka mkasa wake na ndugu zangu wa humu ambao amkupata kusikia basi muusome japo palikua na changamoto nyingi za baazi ya member ambao walikosa ustarabu nashukuru kwa kumaliza mkasa
asanteni.

Latino ni uyo mkono wa kulia iyo ni moja ya interview akismulia mkasa wake na mr davista .
 
Wazee wa mali za mjerumani nadhani wamekusikia sasa washindwe wenyewe
 
Ahsante sana kwa kujitolea nimeburudika sana.
Latino ametukamata kweli kweli ana FIX balaa Ila nimeenda nae huko huko.

Nipe address nikutumie doge coin ukanywe soda.
 
Asante sana mkuu, msalimie sana Latino mwamba... Stori ni nzuri sana.

Mtu kama Latino akipata mchongo kushughulikia wauza unga... Hawachomoki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…