LATRA acheni kuhangaika na nauli za Desemba tu

LATRA acheni kuhangaika na nauli za Desemba tu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Binafsi sioni mantiki ya serikali kuhangaika na kupoteza muda na nauli za mabasi kila mwezi wa December ukifika. Huu ni uingiliaji wa kanuni ya biashara inayoitwa "demand and supply in relation to price". LATRA inatia aibu kugeuza kila kitu kuwa siasa na kampeni.

Inajulikana na kufahamika kuwa mabasi yana ratiba zake za kuondoka na kufika ambazo ni fix, ratiba hizi zikikiukwa na wenye magari zinasababisha maredeva na wenye magari kutozwa faini na polisi wa barabarani, mbali na faini za polisi lakini hata wenye mabasi wengine huwa hawaruhusu basi lichelewe kuondoka kwenye muda wake kwasababu ya kugombea abiria ambao ni wachache sana kwenye miezi mingine. Hivyo basi, ratiba za mabasi, faini za traffic, na wamiliki wa mabasi kugombania abiria kituoni inasababisha yafuatayo:

1. Mabasi mengi kuondoka na abiria pungufu (wachache) ambayo ni hasara kwa wenye mabasi.
2. Mabasi kupunguza nauli kama kivutio cha abiria kupanda basi lao, nayo ni hasara
3. Mabasi kufaulisha abiria wao kwenye mabasi mengine na kusitisha safari (hasara) kwa kusosa abiria.

Inapofika December abiria wanakuwa wengi na mabasi machache, na wakati huu bei kubwa ya nauli haisababishi mtu kuacha kusafiri (inelastic) kwakuwa wengi wameshajipanga na kujitayarisha kwa mwaka mzima kuwa desemba lazima aende kwao, no matter how, kiherehere cha LATRA kuzuia bei kupanda na figisu nyingine kwa wenye mabasi ambao sasa wanapata ahueni kwenye biashara yao kinatoka wapi?

Kupanda kwa nauli za mabasi mwezi decemba kuna faida zifuatazo:

1. Wamiliki wa magari wanajaribu kufidia hasara za usafirishaji walizopata wakati wa uhaba wa abiria
2. Kunapunguza ajali za barabarani kwa kuzuia watu wasiokuwa na safari za lazimia kuacha kusafiri wakati huu.
3. Tunatengeneza mabilionea wengi kwenye taifa kwa njia hii
4. Magari mengi yamekopwa, hivyo mikopo kwenye taasisi za fedha inalipwa kipindi hiki.

Binafsi sioni ni kwanini serikali itoe vibari kwa vyombo vya usafiri vingine visivyo na uzoefu wa kusafirisha abiria kwenye njia hizo kusafirisha abiria. Hata TRC haisafirishi abiria miezi mingine kwakuwa hakuna abiria wengi, hivyo wanaogopa kupata hasara na wenyewe. Tuache nguvu za soko ziamue usafiri kwa mwaka mzima, kwani hiyo ndiyo eco-system inavyofanyakazi, survival of the fittest.
 
kampuni gani yenye mabasi mazuri kwa usafiri wa kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza?
 
Latra, polisi, tra, NIDA, ewura, tanesco nk hizi zilizopo ni mzigo kwa taifa.

Si mbaya wakijua hawatakuwapo hivi kwenye serikali zingine zijazo tuzoazoipigania kwa nguvu zote.

Badala ya kuboresha sekta zao wapo busy kwenye kutafuta sababu za mapato zaidi kupitia faini za kubambika.

Mijitu isiyojua kanuni za biashara, kujua biashara au hata kusoma biashara tu, ni ya nini kwenye kusimamia biashara?

Biashara zita flourish vipi penye mizigo ya namna hii?

Bure kabisa.
 
Binafsi sioni mantiki ya serikali kuhangaika na kupoteza muda na nauli za mabasi kila mwezi wa December ukifika. Huu ni uingiliaji wa kanuni ya biashara inayoitwa "demand and supply in relation to price".....
Hao TABOA wana fares ambazo ziko specific for high season and low season? Tumia akili ya kawaida, ukiwa kwenye biashara ambayo iko regulated na macro actors inajulikana., this is the season where one would expect more supply of busses to exploit an increase in passenger number,. when it's rainy season add more containers to fetch water, enjoy reserves and that will help you during dry season.

With regulated businesses just increase your capacity to leverage the opportunities.

Seasonal rates/prices are not for all kind of businesses.

Tuache kushabikia uhuni kwa akili za matopeni na ujima.
 
Hao TABOA wana fares ambazo ziko specific for high season and low season? Tumia akili ya kawaida, ukiwa kwenye biashara ambayo iko regulated na macro actors inajulikana., this is the season where one would expect more supply of busses to exploit an increase in passenger number,. when it's rainy season add more containers to fetch water, enjoy reserves and that will help you during dry season.

With regulated businesses just increase your capacity to leverage the opportunities.

Seasonal rates/prices are not for all kind of businesses.

Tuache kushabikia uhuni kwa akili za matopeni na ujima.
Kama ndio wana uchumi wetu wa hivi we are finished. Huwezi kununua ndege nyingi kwaajili ya kusafirisha watu kwenye mwezi mmoja tu high season, baada ya hapo ziko grounded for 11 months waiting for the one month of higher season, nonsense!!! Yaani, nilikuwa mmiliki wa mabasi aongeze mabasi kwaajili ya kubeba abiria mwezi mmoja tu wa december, bangi hiziii. Unapo regulate nauli lazima pia uregulate bei za magari, vipuli, bima, na matengenezo. Lakini lazima pia ufidie pale mfanyabiashara anapopata hasara kwa kusafirisha abiria 20 hadi Moshi kwenye basi la watu 60 kwa miezi 10. Yaani hasara na faida za wafanyabiashara wa usafirisahaji lazima zijulikane na namna ya ku intervene.
 
Kama ndio wana uchumi wetu wa hivi we are finished. Huwezi kununua ndege nyingi kwaajili ya kusafirisha watu kwenye mwezi mmoja tu high season, baada ya hapo ziko grounded for 11 months waiting for the one month of higher season, nonsense!!! Yaani, nilikuwa mmiliki wa mabasi aongeze mabasi kwaajili ya kubeba abiria mwezi mmoja tu wa december, bangi hiziii. Unapo regulate nauli lazima pia uregulate bei za magari, vipuli, bima, na matengenezo. Lakini lazima pia ufidie pale mfanyabiashara anapopata hasara kwa kusafirisha abiria 20 hadi Moshi kwenye basi la watu 60 kwa miezi 10. Yaani hasara na faida za wafanyabiashara wa usafirisahaji lazima zijulikane na namna ya ku intervene.
Huijui biashara tulia tu, zingatia regulated businesses zina kanuni zake unataka baki hutaki achia wengine.

Maisha ni vita Mura
 
Kama ndio wana uchumi wetu wa hivi we are finished. Huwezi kununua ndege nyingi kwaajili ya kusafirisha watu kwenye mwezi mmoja tu high season, baada ya hapo ziko grounded for 11 months waiting for the one month of higher season, nonsense!!! Yaani, nilikuwa mmiliki wa mabasi aongeze mabasi kwaajili ya kubeba abiria mwezi mmoja tu wa december, bangi hiziii. Unapo regulate nauli lazima pia uregulate bei za magari, vipuli, bima, na matengenezo. Lakini lazima pia ufidie pale mfanyabiashara anapopata hasara kwa kusafirisha abiria 20 hadi Moshi kwenye basi la watu 60 kwa miezi 10. Yaani hasara na faida za wafanyabiashara wa usafirisahaji lazima zijulikane na namna ya ku intervene.
Kama wanaweza waombe seasonal permits za kuoperate 24hrs hayo mabasi, wanegotiate na hao latra na mamlaka za juu
 
Kama wanaweza waombe seasonal permits za kuoperate 24hrs hayo mabasi, wanegotiate na hao latra na mamlaka za juu

Tatizo la watanzania ni kudhani wanaowadhani kuwa navyo ndiyo sababu ya umaskini au matatizo Yao.

Urithi wao kutoka kwa mwendazake.

Kwamba ni vita kama vipi achia wengine? Kwa hakika ni ujingani tu.

Hiiiiiiii bagosha!
 
Latra, polisi, tra, NIDA, ewura, tanesco nk hizi zilizopo ni mzigo kwa taifa.

Si mbaya wakijua hawatakuwapo hivi kwenye serikali zingine zijazo tuzoazoipigania kwa nguvu zote.

Badala ya kuboresha sekta zao wapo busy kwenye kutafuta sababu za mapato zaidi kupitia faini za kubambika.

Mijitu isiyojua kanuni za biashara, kujua biashara au hata kusoma biashara tu, ni ya nini kwenye kusimamia biashara?

Biashara zita flourish vipi penye mizigo ya namna hii?

Bure kabisa.
Nchi gani isiyo na faini?
 
Wewe kijana hujui lolote kuhusu issue ya usafirishaji hasa wa abilia.

Kwanza; hakuna basi linapigwa faini kwa kuchelewa hakuna, faini ni ukiwahi tu na hata ukiwahi labda kama una mkono mfupi lazima wakupe cheti au kadi ya clinic.

Pili; hujui bora ujifunze kupitia replies za wadau humu, ukisikia mmilikinwa basi anasema anapata hasara basi ujue kakufunika huyo.

Tatu; Nauli iliyopangwa na serikali 'mfano' bus la kawaida kwenda Arusha ni tshs 32,400/- wamiliki wanajua nauli ni hiyo salange, agent na konda pale stendi wanakwambia 38,000 au 45,000 unadhani mwenye basi anaipata hiyo ziada? NO, inakwenda wapi?.

Nne; Extra buses kwa mwisho wa mwaka si bongo tu hata nchi nyengine huko ukienda wanafanya hivyo, nimefika Botswana mpaka hiece zinapeleka watu mikoa ya mbali as Dar to Mwanza sembuse Dar Moshi!.
 
Binafsi sioni mantiki ya serikali kuhangaika na kupoteza muda na nauli za mabasi kila mwezi wa December ukifika. Huu ni uingiliaji wa kanuni ya biashara inayoitwa "demand and supply in relation to price". LATRA inatia aibu kugeuza kila kitu kuwa siasa na kampeni.

Inajulikana na kufahamika kuwa mabasi yana ratiba zake za kuondoka na kufika ambazo ni fix, ratiba hizi zikikiukwa na wenye magari zinasababisha maredeva na wenye magari kutozwa faini na polisi wa barabarani, mbali na faini za polisi lakini hata wenye mabasi wengine huwa hawaruhusu basi lichelewe kuondoka kwenye muda wake kwasababu ya kugombea abiria ambao ni wachache sana kwenye miezi mingine. Hivyo basi, ratiba za mabasi, faini za traffic, na wamiliki wa mabasi kugombania abiria kituoni inasababisha yafuatayo:

1. Mabasi mengi kuondoka na abiria pungufu (wachache) ambayo ni hasara kwa wenye mabasi.
2. Mabasi kupunguza nauli kama kivutio cha abiria kupanda basi lao, nayo ni hasara
3. Mabasi kufaulisha abiria wao kwenye mabasi mengine na kusitisha safari (hasara) kwa kusosa abiria.

Inapofika December abiria wanakuwa wengi na mabasi machache, na wakati huu bei kubwa ya nauli haisababishi mtu kuacha kusafiri (inelastic) kwakuwa wengi wameshajipanga na kujitayarisha kwa mwaka mzima kuwa desemba lazima aende kwao, no matter how, kiherehere cha LATRA kuzuia bei kupanda na figisu nyingine kwa wenye mabasi ambao sasa wanapata ahueni kwenye biashara yao kinatoka wapi?

Kupanda kwa nauli za mabasi mwezi decemba kuna faida zifuatazo:

1. Wamiliki wa magari wanajaribu kufidia hasara za usafirishaji walizopata wakati wa uhaba wa abiria
2. Kunapunguza ajali za barabarani kwa kuzuia watu wasiokuwa na safari za lazimia kuacha kusafiri wakati huu.
3. Tunatengeneza mabilionea wengi kwenye taifa kwa njia hii
4. Magari mengi yamekopwa, hivyo mikopo kwenye taasisi za fedha inalipwa kipindi hiki.

Binafsi sioni ni kwanini serikali itoe vibari kwa vyombo vya usafiri vingine visivyo na uzoefu wa kusafirisha abiria kwenye njia hizo kusafirisha abiria. Hata TRC haisafirishi abiria miezi mingine kwakuwa hakuna abiria wengi, hivyo wanaogopa kupata hasara na wenyewe. Tuache nguvu za soko ziamue usafiri kwa mwaka mzima, kwani hiyo ndiyo eco-system inavyofanyakazi, survival of the fittest.
Mwaka huu LATRA wameamua kupandisha wenyewe huku EWURA wakishusha bei za mafuta, hutaki hamia Burundi.
 
Back
Top Bottom