Lavrov: Magharibi inaitumbukiza Asia Magharibi kwenye vita vikubwa

Lavrov: Magharibi inaitumbukiza Asia Magharibi kwenye vita vikubwa

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288

Nov 07, 2023 08:12 UTC

  • Lavrov: Magharibi inaitumbukiza Asia Magharibi kwenye vita vikubwa
Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kwamba serikali za nchi za Magharibi zimeliweka eneo zima la Magharibi mwa Asia kwenye ukingo wa vita vikubwa kwa hatua zao katika nchi kama Iraq, Syria na Palestina inayokaliwa kwa mabavu.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Sputnik, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergey Lavrov amesema: "Kwa sasa tunashuhudia jinsi Anglo-Saxons wanavyoisukuma Asia Magharibi kwenye ukingo wa vita vikubwa. Sera hii imeonekana wazi zaidi katika maeneo mengine, ikiwa ni pamoja na Ukraine."

Sergey Lavrov ameongeza kuwa: "Kuna mifano mingi ya jambo hili, lakini matokeo yake yanafanana: kuangamiza au kudhoofika serikali za nchi, kama zilivyojaribu kufanya huko Iraqi, Libya au Syria."
4c3o6769a4d6dc2co8f_800C450.jpg

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Russia amesema: Matokeo ya sera hizi za nchi za Magharibi ni ongezeko la ugaidi na misimamo mikali, kuporomoka kwa familia na mawimbi ya mamilioni ya wakimbizi.

Hapo awali Lavrov alikuwa amesema kuwa Moscow inalipa kipaumbele cha kwanza suala la usitishaji vita mara moja kati ya pande zinazohusika katika mzozo wa Palestina na Israel.

Russia imewasilisha miswada kadhaa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ikisisitiza udharura wa kusitishwa mashambulizi ya Israel dhidi ya watu wa Gaza, lakini miswada hiyo imepigwa na nchi za Magharibi washirika wa Israel hususan Marekani.
 
Back
Top Bottom