Lawrance Mafuru: Dira ya Taifa inataka kila Mtanzania awe na kipato cha Dola 3,000 (Tsh. Milioni 7+) mwaka 2025

Lawrance Mafuru: Dira ya Taifa inataka kila Mtanzania awe na kipato cha Dola 3,000 (Tsh. Milioni 7+) mwaka 2025

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Screenshot_2024-04-05-09-19-40-369_com.instagram.android-edit.jpg

Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango amesema, Dira ya sasa ilikuwa baada ya mchakato wa miaka mitatu kuanzia mwaka 1997- 99, chini ya uongozi wa Rais Benjamin Mkapa. Na walikuwa wamejiwekea malengo kadhaa. Na tumefanikiwa au hatujafanikiwa?

Mwaka 2000 walisema itakapofika mwaka 2025 maisha ya Watanzania yawe yameboreka Watanzania wawe na maisha bora. Ambayo ilikuwa inapimwa kwa vipimo kadhaa mojawapo ni kipimo cha kipato kwamba ikifika mwaka 2025 kila Mtanzania awe na kipato cha Dola Elfu Tatu kwa wastani kwa mwezi.

Hilo lilikuwa lengo. Nchi ambazo watu wana vipato vya hivyo zinaitwa kipato cha kati (uchumi wa kati)"
 
Dira upo kwenye makaratasi hongera kwa kuweka kwenye makaratasi kwa lugha tamu nzuri ya kitaalamu na kuvutia

Swala linakuja kuna chombo gani cha kusimamia utekelezaji wa hiyo Dira independent na kuona kama inaenda sawa kwenye utekelezaji na kutoa ripoti?

Mfano huko kwenye dira waweza kuta kuna kipengele kinaobgelea biasha huria na kuongeza wawekezaji.Haya wanakuja mfano wa viwanda migodi nk na mikataba inasainiwa.Baadye mtu anakurupuka anataka mikataba ipitiwe upya ile ya mwanzo ya kinyonyaji haya mwingine anawekeza kwenye maduka ya pesa za kigeni kesho anakuja mwingine anaanza kuvamia na kupora pesa za kigeni kwenye maduka yao,Haya akipora anatumia zinaisha zikiisha anakuja mwingine tongue na nyie wenye maduka serikali sasa ni rafiki kwenu tunspenda uwekezaji wenu wa maduka ya fedha tumekuja na sera rafiki mwendelee tu.Nini hicho ? Dira inasemaje na utekelezaji unasemaje.Yaani nchi inaenda kama gari bovu tu li dira la maendeleo kiko huko,utekelezaji watu hawaangalii dira na hakuna chombo cha uzimamizi wa kuanxia maamuzi kuwa je yana Comply na dira hiyo tuliyonayo kwenye eneo husika linalofanyiwa maamuzi?
 
Back
Top Bottom