Lazaro Nyalandu: Nitapeleka muswada binafsi kurudisha mchakato wa katiba ya Warioba ili tupate katiba mpya

Kweli wakiongozwa na Elibariki
 
Bunge la katiba lilishaipitisha huwezi rudisha mchakato nyuma tena kinachosubiriwa ni kura ya maoni Ya wananchi wa bara na visiwani kupiga kura Kama hiyo katiba ambayo iliridhiwa Na bunge la katiba lenye wawakilishi wa wananchi wanaitaka au la. Tume ya warioba ilikuwa kazi kukusanya maoni tu na kuyapeleka kwa wawakilishi wa wananchi yaani wabunge waiangalie wajadili na waje na rasimu ya bunge wakiipitisha raisi aipeleke kupigiwa kura na wananchi wote waseme yafaa au la. Wengi hawaelewi kazi ya tume ya warioba ilikuwa Nini. Ilikuwa kukusanya maoni tu ambayo si lazima bunge likubaliane nayo. Na hilo si mara ya kwanza bunge kupiga chini maoni ya tume au kuyarekebisha. Mfano iliundwa tume ya kukusanya maoni ya wananchi Kama wanataka kuingia mfumo wa vyama vingi au la wabaki na chama kimoja Asilimia 80 walikataa kuwa hawataki vyama vingi bunge lilipopelekewa likakubali maoni ya wachache waliotaka mfumo wa vyama vingi likatunga sheria ya kuruhusu vyama vingi. Tume ya maoni sio Final!!!! Ya tume ya warioba yalishapita!!! Hiyo hoja hata ikipelekwa itaenda tupwa shimo la choo cha bunge
 
Bendera fuata upepo kila alie ccm anaewapa maneno matamu masikioni mwenu anajitambua,pamoja na kujitambua kote huko mmefaidika vipi na kujitambua kwao
 
Mku huyu anawaonyesha Watanzania njia salama ya kuilinda amani yetu. Ee Mwenyezi Mungu naomba uilinde nchi yangu Tanzania. Amen
 
Huu ni muwasho kutoka singida, yetu macho, huu mchezo hautaki hasira.
 

Sawa naunga mkono hoja
 
Katika hii Dunia kuna v2 havijawahi kujificha, na v2 hivyo ni;
1.Jua
2.Mwezi
3.Ukweli
Ktka issue ya 'ukweli/kweli,anayeificha hyo 'kweli' ndy anayeiweka bayana muda ukiwadia...,sasa naona Nyalandu ameamua kuiweka kweli hadharani baada ya kushindwa kuificha, soon watafuatia na wengine muda ukiwadia.
Kumbukeni habar za Sauli/Paulo kutoka katka Biblia Takatifu,kumbukeni habar za mke wa Uria na Mfalme,kumbukeni habar za Daudi na mke wa Mfalme
You can hide a lot of money,but you can not hide the openly truth
Ccm...,Qumaniner!
 
Ila leo ACT wengi waliohamia makinikia wanatoka Singida pia
 
Hataweza. Watamtimua
 
Hii ndio kazi ya mbunge,kuwakilisha wananchi.wananchi wanataka katiba. Serikali ifanye yake na mbunge afanye yake.... Sio jitu linakuwa halijulikani kama ni waziri au mbunge
 
[HASHTAG]#Nyalandu[/HASHTAG] for president!.Go! go!

Katiba ya Warioba ni tunda la wananchi wao wenyewe!

Hongera sana Brother Nyalandu, tunahitaji wabunge wenye kusimamia issue za msingi kama hizi!!
 
Dar es Salaam. Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu amesema anakusudia kuwasilisha hoja mswada binafsi kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai utakaoweka sharti la kurejea upya mjadala wa Katiba mpya.
Nyalandu ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii katika Serikali ya awamu ya nne , ameeleza hayo katika akaunti zake mitandao ya kijamii ya Instagram, Twitter na Facebook huku akisema mswada huo atauwasilisha kwenye kikao kijacho cha Bunge.
Katika akaunti hizo Nyalandu ameandika: “Nakusudia kuwasilisha kwa Spika wa Bunge , Mheshimiwa Job Ndugai, azma yangu ya kuleta muswada binafsi wa sheria katika kikao kijacho cha Bunge itakayoweka sharti la kurejea upya mjadala wa Katiba Mpya ya Tanzania, kwa kuzingatia Rasimu ya Katiba ilivyowasilishwa na Tume ya Jaji Warioba,” .
 
looser is always are Looser''
Ana chochote Uyu
anatafuta Kick
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…