Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Sijakulia wakati wa mwinyi wala Nyerere lakini historia ndo inatuongoza na kutupatia mwanga kwa vijana wengi ambao hatukuwa wakati ule, kulingana na maoni ya watu wengi, mwinyi alikuja kuifungua Tanzania ni vyema sana, lakini huwezi kufungua nchi kwa kuruhusu tu kuingiza kila kitu nchini maana yake kwanza utaua hata kidogo kilichopo, pili utaua thamani ya pesa yako nchini, tatu utajenga taifa tegemezi, yaani watu wataka mkao wa kusubiri/au kuletewa, Nne utaondoa uzalendo ya bidhaa za ndani dhidi ya bizaa za kigeni, madahara yake ni kuwa na Taifa linalowaza sana msaada hata kwa kitu kidogo hapo ni ndoto kuendelea na mataifa makubwa yakiona hivyo hufurahi sana.

Kuna tofauti kubwa sana ya economic reform ya watu wa china na mzee mwinyi, china ilifanana sana kisera na Tanzania, lakini wao walivyofanya reform ilikuwa tofauti kabisa na ya mzee mwinyi, wao waifanya reform ya Kilimo na viwanda + kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi, hivyo wakaanza kutenga maeneo kwa ajiri ya wawekezaji kutoka nje, wakaja kujenga viwanda, wakati huo huo serikali ya china ilijikita zaidi kugawa maeneo kwa wananchi wao ili waweze kulima kilimo cha kisasa, ndo kile kipindi watu wote waliomaliza vyuo kwa course za kilimo walikuwa wanapelekwa vijijini kusimamia kilimo na wakipata mali ghafi zinakwenda moja kwa moja viwandani, hivyo viwanda vikasimama vya wazawa , pia viwanda vikasimama vya wageni waliotoka , wao wakaanza kuuza bidhaa kwa raia wao pia nje ya nchi.
Kuna kitu kimoja pia tunatakiwa tuelewe, toka Enzi za Mao china imekuwa na viwanda, 80% ya viwada vilikuwa vinamilikiwa na serikali ya china kama ilivyokuwa kuwa Tanzania na ufanisi wake ulikuwa sio mdogo, baada ya 1978 walipojifungua hawakuviacha au kuviua viwanda vyao bali walivibinafsisha tu ili kuongeza uzalishaji, serikali ikawa inakusanya mapato, hakuruhusu vitu kuingia nchi kwao kiholela.
Kingine, serikali ilianza kukopa kutoka Bank ya dunia kwa ajiri ya kujenga miundo mbinu ya kisasa kuconnect the whole country na wakasimamia kwa makini, watu wakaanza kufanya biashara nchini bila vikwazo then wakafunguka hadi nje ya nchi. Maendeleo ya china kwa style ile iliwachukua ndani ya miaka 14 tu kila kitu kilikuwa kimeeleweka.

Swali je kufunguka kwa mzee mwinyi ilikuwa ni same same kama watu wa china? Jibu ni NO, je mwinyi alijenga kiwanda au alianzisha mchakato wowote wa kuondoa umasikini kama watu wa china walivyofanya, jibu ni NO, Je kuna barabara zilizojengwa kuunganisha nchi ya Tanzania jibu ni NO,inawezekana kabisa hata sarafu ya Tanzania ilishuka thamani kwa style ile ya ruksa, maana huwezi ruhusu vitu kuja nchini vikaiacha rafu ya nchi salama haitawezekani. Kwa hivyo tutafurahi kuja kwa vitu lakini sio tatizo la kuondoa umasikini au kuleta maendeleo nchini.

Benjamin Mkapa, alichokifaya mkapa katika utawala wake ndo kitu ambacho mwinyi alitakiwa afaye wakati ule, lakini kosa la mkapa ni moja kuua viwanda vya ndani, mkapa alitakiwa afanye ubinafisishaji kwa usawa, unabinafisisha lakini serikali au wananchi wanakuwa na hisa/maamuzi makubwa zaidi, kila shirika unalobinafisisha unahakikisha over 50% za hisa zinakuwa chini ya serikali . Pia alitakiwa aendeleze kulinda viwanda vya ndani, je angelinda viwanda vipi? jibu hakuna, je alitakiwa amlaumu mwinyi kwa kutokuwa na viwanda jibu Hapana, yeye angeanza moja kwa moja kuja na sera ya kilimo na viwanda tukaanzia pale leo hii tungekuwa mbali.
Pia Kuna tatizo katika ubinafisishaji mwanya wa wizi unaongezeka sana hili swala likaibuka na likamshinda Mkapa, kwa nini? hakuwa na sera nzuri ya kupambana rushwa. Lakini kwa upande wa huduma walau alijitahidi, barabara zikajengwa, mashule mengi yakafunguliwa hata ya kata, mikopo vyuoni, na akajenga taasisi japo si imara yaani kwa ufupi mkapa katupeleka western zaidi na kuzika issue za ujamaa.

Swali ni moja tu hapa, je Tanzania itaendelea kwa kutegemea uagizaji wa bidhaa kutoka nje? jibu Haitawezekana na nikupoteza muda kuwaza hivyo.
Kwa maelezo hapo juu, mtajua sasa ni dhama ipi ilikuwa na lengo la kuondoa umasikini Tanzania japo kwa maumivu, pia Tanzania tunatakiwa kujua hatutakuja kuendelea bila kukubali kuumia au kufanya kazi kwa bidii aua kuthamini vitu vyetu vya ndani, tunaweza tukawa na njia za haraka haraka za mikato lakini tujue maendeleo ni kitu kingine hakihitaji comparison ya uislam wala ukristo, ccm wala chadema kina hitaji nidhamu kupanga na kufanya.
 
Dutch disease

The classic economic model describing Dutch Disease was developed by the economists W. Max Corden and J. Peter Neary in 1982. In the model, there is the non-traded good sector (this includes services) and two traded good sectors: the booming sector, and the lagging sector, also called the non-booming tradable sector. The booming sector is usually the extraction of oil or natural gas, but can also be the mining of gold, copper, diamonds or bauxite, or the production of crops, such as coffee or cocoa. The lagging sector generally refers to manufacturing, but can also refer to agriculture.

A resource boom will affect this economy in two ways. In the "resource movement effect", the resource boom will increase the demand for labor, which will cause production to shift toward the booming sector, away from the lagging sector.

This shift in labor from the lagging sector to the booming sector is called direct-deindustrialization. However, this effect can be negligible, since the hydrocarbon and mineral sectors generally employ few people. The "spending effect" occurs as a result of the extra revenue brought in by the resource boom. It increases the demand for labor in the non-tradable, shifting labor away from the lagging sector. This shift from the lagging sector to the non-tradable sector is called indirect-deindustrialization.

As a result of the increased demand for non-traded goods, the price of these goods will increase. However, prices in the traded good sector are set internationally, so they cannot change. This is an increase of the real exchange rate.

In simple trade models, a country ought to specialise in industries that it has a comparative advantage in, so theoretically a country rich in natural resources would be better off specialising in the extraction of natural resources. In reality, however, the shift away from manufacturing can be detrimental.

http://en.wikipedia.org/wiki/Dutch_disease
 
JK na Mkapa na Nyerere hata wafanye nini hawawezi kumfikia Mzee mwinyi hata kwa punje

ukweli ndio huo
 
Kabla ya Mzee watu wali choka vijana walifanya majaribio mara 2 ya kuteka ndege ya ATC na mara moja walifanikiwa kuipeleka UK...na kudai Serikali iondoke imeshindwa..ilikua moja ya aibu kuu kwa Mwalimu. Kwani habari ile na ya mateka wale ilitangazwa dunia nzima na wote wali sypathisize na watekaji...kwani hali ilikua mbaya TZ..
Aisee !! Kweli mmetoka mbali, hii habari ya kuwahi kutekwa ATC sijawahi isikia, unaweza kutupa habari zaidi tujifunze ?
 
Wakuu habar ya majukumu.

Kwanza nitangulize precaution kwamba simtabirii kifo Rais wa awamu ya pili Alhaj Ally Hassan Mwinyi.

Nimekuja hapa kutaka kujuzwa kuhusu Mwinyi kabla hajafa ili tumpe hongera zake akiwa hai. Kumekuwa na kasumba katika nchi yetu ya kumwagia sifa nyingi kiongozi mara tu anapofariki, wakati akiwa amekufa sifa zake humwagwa hata zile ambazo wengine hatukuwahi kuzijua, sijui kwa nini hali hii inasubiri mpaka afe.

Leo nimefikiria kuhusu Mzee Mwinyi simaanishi kumtabiria kifo lakini kwa mwanadamu yeyote anaeamini uwepo wa Mungu anaamini kuna siku atakufa. kwa kulitambua hilo mimi kama kijana ambae wakati Mzee mwinyi anaongoza (1985-1995) nilikua sijapevuka kuweza kupambanua mambo na kwa bahatu mbaya sana watanzania hatuna tabia ya kuweka kumbukumbu zetu kwenye maandishi imeniwea vigumu sana kufahamu uimara na udhaifu wa mzee Mwinyi wakati wa utawala wake.

Hivyo nimekuja humu kuwaomba wajuzi wa mambo ambao wao pengine walikuwa na ufahamu wa kutosha kipindi cha Mwinyi watujuze strength na weakness za utawala wake ili apatiwe haki yake akiwa hai tusisubiri Mzee amefariki tuanze kujaza nyuzi humu kila mtu akijifanya kunfahamu Mzee. Nimejifunza hili kwenye msiba wa Mzee Sitta tukiambiwa mambo mengi ambayo hata hatukuwahi kuyafahamu.

tabia hii tuache watanzania, leo nimeona nianze na hili tuambieni kuhusu Mzee Mwinyi.

Nawasilisha
 
Kuelewa mchango wa Mwinyi unapaswa kwanza kuelewa hali ya nchi ilivyokuwa wakati anakuwa Rais...

Nchi ilikuwa na Redio moja tu Redio Tanzania..na magazeti ya chama na serikali...

hakuna kabisa sehemu ya kukosoa wala kueleza matatizo...

na baada ya vita ya Iddi Amin kiuchumi nchi ndo ikayumba kabisa

Sera za Nyerere za ujamaa na kila kitu kufanywa na serikali kuanzia kuuza mikate
hadi nguo n kadhalika ilisha feli....

watu wanapanga foleni kununua sukari na sigara

mtu akienda Kenya mnamuagiza colgate na sabuni za lux...

hali ilikuwa mbaya except kwa wachache waliokuwa na nafasi...

Mwinyi akaapishwa mwaka 1985....by the time anaondoka 1995..

Ilikuwa nchi tofauti kabisa.......magazeti tele..TV na redio...tele
vyama vya upinzani.....hadi uchaguzi wa 1995 kulikuwa na mdahalo kwenye tv

hapo ndo Lipumba akaibukia CUF....

Vitongoji kama Sinza vikawa maarufu wakati wa Nyerere ni kulikuwa na mashamba tu ya mpunga..
magari ikawa ruksa unanunua bila kuomba kibali..

Sasa wapo wanaosema hakufanya lolote...
labda mabadiliko yangekuja tu bila yeye...

but wengi wanaosema hivyo hawakuwepo enzi hizo
 
1.Aliitoa nchi toka mfumo wa kimashariki -ujamaa (socialim) kwenda mfumo wa kimagharibi-ubepari (capitalism) tuliokuwa nao hivi sasa chini ya sera maarufu ya RUKSA
2.Ndie muanzilishi wa mfumo wa vyama vingi uliopo hivi sasa baada ya mara ya kwanza kuondolewa miaka ya 1976-70
3.Hakua mbaguzi wa dini aliamini kila Mtanzania ana haki regardless ya jinsi na jinsia aliyenayo
 
Mungu ndiyo anajua siku zetu za kuishi, kwanini hujasema mniambie mazuri ya Mwingi kabla sijafa?
 
Hivi ni kweli alioa akiwa madarakani ??
 
Back
Top Bottom