Mkuu nakuunga mkono kabisa sample yangu kuna mjuu wake binti mdogo tu anaitwa Sitti Mwinyi naweza kukapa nidhamu A.Licha ya ucha Mungu pia ni Baba na Babu bora kabisa wa familia yake, watoto na wajukuu zake wengi wananidhamu na ubinadamu kama yeye mwenyewe.
Na sheria alitia yeye sahii...Nyerere kwanza hakupenda vyama vingi kabisaRoho mbaya tu za watu kwa Mwinyi.
Ila umeiweka kichochezi ha ha ha,ety mabanzi mushabaraHalafu kuna njemba ilimkataga mabanzi mubashara hadharani yaani watu wana laana dunia hii.
Na upole ule wa Mzee mwinyi unatoa wapi ujasiri wa kumuadhibu na sucker slap...alinifurahisha alipomsamehe. That's was tottaly humane and humble.
Unatukumbusha mbali sana tena sana, watu tumetoka mbali, Mzee Mwinyi ndie aliyefanya watanzania wengi wajue kama tv. Nchi kabla yake iliongozwa kidikteta hakuna aliyethubutu kusema lolote baya kwa Mwalimu.Hali ilikuwa mbaya kupita maelezo
nchi nzima watu wanavaa katambuga
sabuni za magadi na majani ya mpapai..
mahindi ya msaada kutoka marekani ya njano
yaliitwa mahindi ya Yanga....
ukikutwa na sigara box zima unakamatwa kwa uhujumu uchumi
Tazama hapa uadilifu na ucha mungu wa mzee wetu kipenzi
Tazama maneno yake kwenye barua hii ya kujiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani mwaka 1977
Alli hassan mwinyi.
Sidhani kama anaweza kuja Rais tena mwenye subra na uvumilivu, huruma, mpole na mwenye mahaba ya dhati na watu wake kama Ally Hassan Mwinyi.Alikuwa anamsikiliza Nyerere weeeeee, hambishii, akitoka hapo anafanya anavyoona yeye inafaa!
Enzi zake vijana wakaanza kwenda Dubai kuleta mali
Aliamua makusudi kutokusanya kodi kutoka kwa Makabwela ili kuwajengea watu uwezo wa kifedha, ili baadae wapatikane watu wa kuwatoza kodi..
Alilichinjilia mbali Azimio la Kimasikini lile Azimio la Arusha, Wewe umewahi kuona wapi Azimio linazuia watu kumiliki hata nyumba ya kupangisha eti kisa wewe ni Mwenyekiti wa kijiji.
Wakati anaondoka madarakani almost kila mtu akawa ana TV, watu tumeangalia World Cup mwaka 1994 ITV, tumeangalia Kombe la Mataifa huru ya Afrika yaliyofanyika Tunisia mwaka 1994 Live kila mtu na kideo chake nyumbani!
Pesa ilikuwa inapatikana, Vijana wakaanza kuangusha majumba ya hatari Mbezi, Tabata, Sinza
Aliandikwa vibaya sana na Magazeti kama RAI ya Jenerali Ulimwengu lakini hukusikia anayafungia!
Long live mzee Ruksa, Uko mioyoni mwetu forever!
Umenifurahisha sentensi yako ya kwanzaAlikuwa anamsikiliza Nyerere weeeeee, hambishii, akitoka hapo anafanya anavyoona yeye inafaa!
Enzi zake vijana wakaanza kwenda Dubai kuleta mali
Aliamua makusudi kutokusanya kodi kutoka kwa Makabwela ili kuwajengea watu uwezo wa kifedha, ili baadae wapatikane watu wa kuwatoza kodi..
Alilichinjilia mbali Azimio la Kimasikini lile Azimio la Arusha, Wewe umewahi kuona wapi Azimio linazuia watu kumiliki hata nyumba ya kupangisha eti kisa wewe ni Mwenyekiti wa kijiji.
Wakati anaondoka madarakani almost kila mtu akawa ana TV, watu tumeangalia World Cup mwaka 1994 ITV, tumeangalia Kombe la Mataifa huru ya Afrika yaliyofanyika Tunisia mwaka 1994 Live kila mtu na kideo chake nyumbani!
Pesa ilikuwa inapatikana, Vijana wakaanza kuangusha majumba ya hatari Mbezi, Tabata, Sinza
Aliandikwa vibaya sana na Magazeti kama RAI ya Jenerali Ulimwengu lakini hukusikia anayafungia!
Long live mzee Ruksa, Uko mioyoni mwetu forever!
Hii ni weakness yake.Alikuwa anasikiliza sana ushahuri wa mke wake kuliko baraza la mawaziri
Kabisa mengi kamaliza the Boss. Nakumbuka mwaka 1984 watoto wa shule zote (msingi na sekondari) ambao sare zao zimechanika waliruhusiwa kutumia kitambaa cha madurufu (sanda) kushona sare za shule maana ndio kitambaa pekee kilichopatikana kwa wengi madukani. Mzee Mwinyi alipoingia madarakani akasema "ruksa" kuingia bidhaa nchini.Mkuu kwani hayo ayasemayo THE BOSS kuhusu MZEE RUKSA ni ya uongo??
RUKSA ALIITOA HII NCHI KWENYE TONGOTONGO NA GIZA KALI..
1. ALIFUATA TORATI YA MUSA NA KUWANYONGA WOTE WALIOHUKUMIWA KIFO NA MAHAKAMA KWA MUJIBU WA SHERIA ZA TANZANIA BILA MZAHA WALA UPENDELEO AKIWEMO KANALI MMOJA TOKA TABORA NAMPENDA SANA KWA HILOWakuu habar ya majukumu.
Kwanza nitangulize precaution kwamba simtabirii kifo Rais wa awamu ya pili Alhaj Ally Hassan Mwinyi.
Nimekuja hapa kutaka kujuzwa kuhusu Mwinyi kabla hajafa ili tumpe hongera zake akiwa hai. Kumekuwa na kasumba katika nchi yetu ya kumwagia sifa nyingi kiongozi mara tu anapofariki, wakati akiwa amekufa sifa zake humwagwa hata zile ambazo wengine hatukuwahi kuzijua, sijui kwa nini hali hii inasubiri mpaka afe.
Leo nimefikiria kuhusu Mzee Mwinyi simaanishi kumtabiria kifo lakini kwa mwanadamu yeyote anaeamini uwepo wa Mungu anaamini kuna siku atakufa. kwa kulitambua hilo mimi kama kijana ambae wakati Mzee mwinyi anaongoza (1985-1995) nilikua sijapevuka kuweza kupambanua mambo na kwa bahatu mbaya sana watanzania hatuna tabia ya kuweka kumbukumbu zetu kwenye maandishi imeniwea vigumu sana kufahamu uimara na udhaifu wa mzee Mwinyi wakati wa utawala wake.
Hivyo nimekuja humu kuwaomba wajuzi wa mambo ambao wao pengine walikuwa na ufahamu wa kutosha kipindi cha Mwinyi watujuze strength na weakness za utawala wake ili apatiwe haki yake akiwa hai tusisubiri Mzee amefariki tuanze kujaza nyuzi humu kila mtu akijifanya kunfahamu Mzee. Nimejifunza hili kwenye msiba wa Mzee Sitta tukiambiwa mambo mengi ambayo hata hatukuwahi kuyafahamu.
tabia hii tuache watanzania, leo nimeona nianze na hili tuambieni kuhusu Mzee Mwinyi.
Nawasilisha
Propaganda hii aliianzisha Nyerere baada mawazo yake hayafuatwi.Hii ni weakness yake.
Hiyo ni mbingu na ardhi!!! Mzee Mwinyi hakuwa mtu wa visasi, alikua mtu anaeshaurika na kuchukua hatua baada ya tafakuri ya kutosha, alitamani wananchi wake waishi kama malaika hakupenda watu wawe maskini aliruhusu mijadala ya kumkosoa ndio maana alisema "dereva mzuri haachi usukani ili kumpiga mbu anaemn'gata"Kifupi ni kwamba rais wetu WA Sasa aige mengi kutoka Kwa MWINYI
Ahsante sana mkuu1. ALIFUATA TORATI YA MUSA NA KUWANYONGA WOTE WALIOHUKUMIWA KIFO NA MAHAKAMA KWA MUJIBU WA SHERIA ZA TANZANIA BILA MZAHA WALA UPENDELEO AKIWEMO KANALI MMOJA TOKA TABORA NAMPENDA SANA KWA HILO
2. ALIWABEBA SANA WAFANYABIASHARA KIASI KWAMBA AJIRA IKAONEKANA NI UPUUZI NA WENGI WALIACHA KAZI SERIKALINI KWAKUWA MISHAHARA ILIKUWA HAIPATIKANI MPAKA WAFANYABIASHARA WAPELEKE FEDHA BANK NDIPO MFANYAKAZI APATE MSHAHARA NI KATIKA KIPINDI CHAKE ALINISABABISHIA NIACHA KUSOMA BAADA YA KUONA KUAJIRIWA HAKULIPI KAMA KUFANYA BIASHARA
3. ALIMDEKEZA SANA WAZIRI WA FEDHA MAREHEMU PROF. KIGHOMA ALI MALIMA AKAJENGA MSIKITI WIZARA YA FEDHA.
4. NI KATIKA KIPINDI WAISLAM WALITAKA TANZANIA IONGOZWE KIDINI NA MKAKATI HUO ULIONGOZWA NA MAREHEMU SHEIKH YAHYA HUSSEIN KWA KUANZISHA BALKUTA NA KUANZA KUVUNJA MABUCHA YA NGURUWE NA NI KIPINDI HICHO NYAMA YA NGURUWE ILIITWA KWA UTANI "YAHYA" AU MBUZI KATOLIKI
5. NI KATIKA UTAWALA WA MWINYI SERIKALI ILIKUWA HAIKUSANYI KODI NA WAFANYABIASHARA WALIKUWA NA NGUVU YA KUFANYA LOLOTE NA IKULU PALIKUWA PANAINGILIKA KIRAHISI SANA HATA UKIWA NA SHIDA YA ADA YA SHULE ULIRUHUSIWA KUMUONA RAIS NA UKIHITAJI KUCHEZA BAO NA PRESIDAA UNAOMBA NA UNAINGIA KAMA ALIVYOFANYA MWENYEKITI WA YANGA NA MBUNGE WA KILOMBERO MAREHEMU ABBAS GULAMALI. NAISHIA HAPO.
basi jombi ya meishaMkuu mimi nimeanza na huyu nafahamu wapo wengi hata wew unaweza ukaanzisha uzi kwa wengine maana wapo wengi, wapo akina malecela, warioba, salim.. wapo wengi mno
samahani jombi ulimi hauna mfupaAnzisha thread yako tumuhoji mwalimu au karume au mkapa au kikwete au magu..simple Sana