Pre GE2025 Lema: Tukiruhusiwa tutatumia mfumo wa sarafu za kidijitali (cryptocurrency) ili kuweza kukusanya michango ya mkakati wa Tone Tone

Pre GE2025 Lema: Tukiruhusiwa tutatumia mfumo wa sarafu za kidijitali (cryptocurrency) ili kuweza kukusanya michango ya mkakati wa Tone Tone

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mwenyekiti wa Kamati ndogo ye fedha ya CHADEMA CHADEMA ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Godbless Lema amesema wapo tayari kutumia mfumo wa sarafu za kidijitali (cryptocurrency) ili kuweza kukusanya michango ya kwenye mkakati wa Tone Tone.

Soma Pia: Godbless Lema: Mkakati wa Tone Tone ni mpango wa kuchangia fedha kwa chama kwa kutumia mifumo ya kidigitali

Lema amesema hayo wakati wa uzinduzi wa mkakati huo na kueleza kuwa endapo taratibu za kisheria za nchi zikiwaruhusu watatangaza sarafu ya kidijitali ya CHADEMA ambayo itaitwa CDM Coin au CHADEMA Coin.

 
Na yeye amesema kama Sheria zitaruhusu!
Kwa kauli hiyo inaonesha kuwa ndugu Lema HAJUI hata utaratibu wa CRYPTOCURRENCY hapa nchini...

Sheria ilitungwa mwaka 2015....miaka 10 yote hii hajui kama ipo, ha ha ha ha Lema kweli "tabura rasa" !!
 
Tuachane na regulatory risks, Liquidity ya hiyo coin itakuaje ? Wataalamu watusaidie feasibility ya hii kitu naona kama kuna ukakasi hapa
Wapo watanzania wengi duniani wenye nia njema wanaweza kuvunja tu wakarusha madafu! Sio big deal
 
*The National Payments System Act of 2015"... unlicenced digital payments....
Ok weka kipengele kinachocontrol kulipwa kwa crypto tuende sawa! Sio lisheria ya kucopy na kupaste la mwigulu ambaye hata yeye mwenyewe halijui
 
Ok weka kipengele kinachocontrol kulipwa kwa crypto tuende sawa! Sio lisheria ya kucopy na kupaste la mwigulu ambaye hata yeye mwenyewe halijui
....hata VPN haziruhusiwi na sheria yetu lakini watu wanazitumia katika simu zao....fahamu kuvunja sheria tuko palepale...

Kwa hili REGULATORY BODIES zije na "approaches" dhidi ya hawa wavunja sheria hadharani....
 
Mwenyekiti wa Kamati ndogo ye fedha ya CHADEMA CHADEMA ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Godbless Lema amesema wapo tayari kutumia mfumo wa sarafu za kidijitali (cryptocurrency) ili kuweza kukusanya michango ya kwenye mkakati wa Tone Tone.

Soma Pia: Godbless Lema: Mkakati wa Tone Tone ni mpango wa kuchangia fedha kwa chama kwa kutumia mifumo ya kidigitali

Lema amesema hayo wakati wa uzinduzi wa mkakati huo na kueleza kuwa endapo taratibu za kisheria za nchi zikiwaruhusu watatangaza sarafu ya kidijitali ya CHADEMA ambayo itaitwa CDM Coin au CHADEMA Coin.

awe muwazi tu kwamba wapo tayari kutapeli wananchi kidigitali na kujaribu kufanya money laundring kisayansi,

nadhani wakienda kufanyia Burundi itapendeza zaidi ikiwa wataruhusiwa 🐒
 
.....kwa hiyo amesahau alichoshauri huko nyuma ?!!

Well....sheria inakataza matumizi ya CRYPTOCURRENCY.....kwa hiyo hiyo michango yenu isubiri mabadiliko ya sheria hiyo ya BOT ?!!
Hiyo ni alternative! Siyo kwamba michango haiwezi kupatikana kwa njia nyingine.
 
Back
Top Bottom