Leo hii ni Januari 2021, hivi gesi ya Mtwara imefikia wapi?

Leo hii ni Januari 2021, hivi gesi ya Mtwara imefikia wapi?

Gas awamu ya kikwete ilifanya usanii wa kutisha nyie acheni tu! hawakutosheka na Escraw
 
Yaliletwa mashtaka kwetu wadanganyika kuwa gesi si mali yetu tena, ilishachukulia na mabeberu zile dk za mwisho za lele mama, walopopitisha ule mswaada kwa dharula usiku kwa usiku mjengoni.

Ingawa mshtaki alikuwa miongoni mwao, hakuwa na la kufanya zaidi ya kutii agenda za kikundi.

Na kwakweli, tumeamua kwa dhati, maji yanakuwa mbadala, sitigila inakamilika, mwanga bwelele siku zijazo.
Na hio pia dakika za mwisho tutaambiwa imeshatekwa na mabeberu
Mataga ni balaa kama korona
 
Ni miaka isiyopungua tisa sasa toka sakata la uchimbaji wa gesi ya Mtwara lilipoibuka hapa Tanzania. Matumaini yalikuwa makubwa, mbwembwe kibao, nguvu ikatumika na watu kupoteza maisha ili gesi itoke Mtwara.

Kuna kitu mpaka sasa nimeshindwa kukielewa kuhusu gesi ya Mtwara, nacho ni Ukimya. Ukimya ni mkubwa na hakuna kiongozi yoyote wa serikali iliyopo madaraka na iliyopita inayejitokeza kulizungumzia. Na hakuna chombo chochote cha habari kinachotupa updates au kumbukumbu ya gesi ya Mtwara.

Nini kinaendelea kuhusu gesi ya Mtwara?
Wapinzani hasa CHADEMA walikua wanakwamisha mchakato mzima wa gesi ndio maana tumewaengua ili kukamilisha mchakato huo
 
Wewe tulia umesikia kama cabodelgado kumechafuka sasa hio gesi tusiifanyie haraka wacha mambo yakitulia tutaanza kuipulizia tena kwenye mapaipu,mazuri hayataki kishindo.
 
Tayari makampuni ya uwekezaji yalijiandaa kuwekeza dola bilioni 30 kwenye mradi wa ujenzi wa LNG. Huu ungekuwa mradi mkubwa wa uwekezaji ambao haujawahi kuwepo katika kanda ya Afrika.

Alipoingia Kivuruge, kama kawaida, miradi yote iliyosainiwa na watangulizi wake, akasimamisha kwa madai kuna ufisadi. Kama alivyofanya kwenye SGR. Wenzake walisaini ungejengwa kwa dola dola bilioni 11, yeye mpaka Singida tayari ni bilioni 9. Kufika Mwanza utajengwa kwa dola bilioni ngapi? Na bado anawadanganya wajinga kuwa anapiga vita ufisadi. Wachina aliowakataa, sasa anawapigia magoti.

Wawekezaji wa gas waliamua kuondoka na kwenda kuwekeza Mozambique. Huko wanajenga LNG, ni uwekezaji wa dola bilioni 28, na ni uwekezaji wa pili kwa ukubwa Duniani kwenye sekta ya gas kwa mwaka 2020/2021.

Wameombwa sana kurudi lakini wamekataa. Muda wa karibu kabisa kuweza kufikiria kuwekeza tena Tanzania, wanasema ni baada ya miaka 5.

Kwa hiyo uchumi wa gas umeyeyuka. Nchi tajiri kabisa Duniani kwa kuzingatia wastani wa mapato ni Qatar. Kinachosababisha wawe matajiri hivyo, ni gas. Sheria yetu ya gas kabla ya 2016, ilikuwa ni copy and paste ya Qatar na Norway. Lakini jamaa akasema ni ya kifisadi. Kama Qatar na Norway, sheria hiyo hiyo imewatajirisha, inakuwaje ya kifisadi kwetu?

Kutafuta umaarufu kwa kisiasa kwa mtu mmoja kumeliletea hasara isiyoelezeka Taifa.

Kiongozi atakayefuata atakuwa na kazi kubwa ya kurekebisha mambo mengi ili kuirudisha nchi kwenye uchumi wa kisasa na kistaarabu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii gesi inapigwa vita sana na makaka wa dunia ndio maana unaona wanamgambo wenye mapanga na marungu wameweza kuteka mradi mzima wa LNG kule msumbiji na hakuna wa kuwatoa
 
Ni miaka isiyopungua tisa sasa toka sakata la uchimbaji wa gesi ya Mtwara lilipoibuka hapa Tanzania. Matumaini yalikuwa makubwa, mbwembwe kibao, nguvu ikatumika na watu kupoteza maisha ili gesi itoke Mtwara.

Kuna kitu mpaka sasa nimeshindwa kukielewa kuhusu gesi ya Mtwara, nacho ni Ukimya. Ukimya ni mkubwa na hakuna kiongozi yoyote wa serikali iliyopo madaraka na iliyopita inayejitokeza kulizungumzia. Na hakuna chombo chochote cha habari kinachotupa updates au kumbukumbu ya gesi ya Mtwara.

Nini kinaendelea kuhusu gesi ya Mtwara?
Ikiwa kweli unataka kujua kinachoendelea kuhusu gesi ya Mtwara nakushauri ukasome bajeti ya wizara ya nishati ya mwaka huu wa fedha. Kuna shughuli zitafanyika mwaka huu na zimetengewa mabilioni ya pesa.

Bali ikiwa lengo lako ni kupiga siasa tu hapa ninakushauri uendelee kusubiria updates kutoka kwa wanaharakati wa hapa na pale mitandaoni.
 
Mbona mkataba wa madini kama Barick walifurukuta furukuta kuwakabili mabeberu? Jpm mbona kwenye gesi ana act kinyonge hivi?
Mkuu, haja-act kinyonge. Ni ile tu hataki kupiga makelele. Kuna vitu vinaendelea underground. Fanya ukasome bajeti ya wizara ya nishati ya mwaka huu neno kwa neno utaelewa namaanisha nini.
 
Kwa saiv tuiache kwanz iwe pending... Lakin kama ingekuwepo hapa kwetu chato tungefanya jambo
 
Na hakuna chombo chochote cha habari kinachotupa updates au kumbukumbu ya gesi ya Mtwara.
mkuu kwa sasa uzalishaji wa gas unaendelea vizuri kwa PROCESSING PLANT ILIYOPO MADIMBA, na ile iliyopo kisiwa cha songosongo mkoani LINDI. Hiyo gas inasafirishwa hadi pale KINYEREZI ambapo inagawanywa kwenda kwenye plants za kuzalisha umeme za TANESCO (UBUNGO, KINYEREZI n.k) pia gas hiyo imepelekwa katika viwanda binafsi kama dangote cement, goodwil ceramics, rodhia steel n.k na mwisho kwa sasa raia wa kawaida wanaendelea kuunganishiwa katika mikoa ya dsm, mtwara na lindi kwa matumizi ya kupikia.
unaweza kupitia sites za TPDC >>>> www.tpdc.co.tz na instagram check @tpdctz

NB. mimi ni raia tuu niliyeona ni vyema niseme ninachojua kwa uchache.
 
Ikiwa kweli unataka kujua kinachoendelea kuhusu gesi ya Mtwara nakushauri ukasome bajeti ya wizara ya nishati ya mwaka huu wa fedha. Kuna shughuli zitafanyika mwaka huu na zimetengewa mabilioni ya pesa.

Bali ikiwa lengo lako ni kupiga siasa tu hapa ninakushauri uendelee kusubiria updates kutoka kwa wanaharakati wa hapa na pale mitandaoni.
Upload doc yake kama una-acces nayo mkuu.
 
Ni miaka isiyopungua tisa sasa toka sakata la uchimbaji wa gesi ya Mtwara lilipoibuka hapa Tanzania. Matumaini yalikuwa makubwa, mbwembwe kibao, nguvu ikatumika na watu kupoteza maisha ili gesi itoke Mtwara.

Kuna kitu mpaka sasa nimeshindwa kukielewa kuhusu gesi ya Mtwara, nacho ni Ukimya. Ukimya ni mkubwa na hakuna kiongozi yoyote wa serikali iliyopo madaraka na iliyopita inayejitokeza kulizungumzia. Na hakuna chombo chochote cha habari kinachotupa updates au kumbukumbu ya gesi ya Mtwara.

Nini kinaendelea kuhusu gesi ya Mtwara?
Unaleta majungu mzee siyo,hivi kila kiongozi anashughulikia gesi ya mtwara?

Acha uchochezi katembee kwa miguu kutoka lilipoanzia lifute utajua limeishia wapi
 
Ni miaka isiyopungua tisa sasa toka sakata la uchimbaji wa gesi ya Mtwara lilipoibuka hapa Tanzania. Matumaini yalikuwa makubwa, mbwembwe kibao, nguvu ikatumika na watu kupoteza maisha ili gesi itoke Mtwara.

Kuna kitu mpaka sasa nimeshindwa kukielewa kuhusu gesi ya Mtwara, nacho ni Ukimya. Ukimya ni mkubwa na hakuna kiongozi yoyote wa serikali iliyopo madaraka na iliyopita inayejitokeza kulizungumzia. Na hakuna chombo chochote cha habari kinachotupa updates au kumbukumbu ya gesi ya Mtwara.

Nini kinaendelea kuhusu gesi ya Mtwara?
Kwani wewe unadhani hiyo gesi iliyopo Kinyerezi, DSM, ikituzalishia zaidi ya MW 1,000 za umeme inatoka wapi kama si Mtwara?

Mpango mwingine uliopo ni wa kuiuza nje (export) kiasi fulani ya hiyo gesi ya Mtwara ughaibuni ikiwa kwenye LNG form kama wanavyofanya Russia.
 
Mkuu, haja-act kinyonge. Ni ile tu hataki kupiga makelele. Kuna vitu vinaendelea underground. Fanya ukasome bajeti ya wizara ya nishati ya mwaka huu neno kwa neno utaelewa namaanisha nini.
Mkuu, kama hutojali, tuwekee humu. Ukiondoa matatizo yaliyojitokeza, ule mradi uliukuza sana mji wa Mtwara, na kiukweli pamoja na korosho, Mtwara ilitisha na kama ile move ingechukua miaka kama 10 hivi, Mtwara ilikua ni tishio. Tuombe ile miradi irudi tena ili kukuza uchumi
 
Back
Top Bottom