Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 22,168
- 39,118
Kwa bahati nzuri Mungu alinijalia kuipenda soka bila mahaba ya timu za Kariakoo. Utashangaa nimewezaje lakini kwangu halikuwa Jambo kubwa kuamua zaidi ya kuupenda mpira wa miguu na kuufuatlia katika Nyanja nyingine ya Uamzi.
Leo ni Tamasha kubwa la timu ya Simba (S. S. C DAY) linaloazimishwa August 8 Kila mwaka Tangu mwaka 2009. Ni Tamasha kubwa linalovuta hisia si Kwa wapenzi na mashabiki wa Simba pekee bali wa vilabu vyote ndani na nje ya Tanzania Kwa jinsi linavyovuta hisia za Soka.
Tarehe 6/08/2022 siku mbili tu zilizopita Yanga walikuwa na Tamasha kubwa kama hili pale pale Uwanja wa Mkapa Temeke Dar es salaam. Mgeni rasmi katika tukio Lao alikuwa Kinana Makamu mwenyekiti wa CCM Taifa. Mbali ya ukubwa wa Tamasha lile na umuhimu wa timu hiyo kama ilivyo Kwa Simba kuhusu soka la nchi hii, Viongozi wote wa juu wa TFF hususan Karia Kwa upekee kabisa hawakufika, hawakuhudhuria.
Leo Simba Wana tukio kubwa na naambiwa mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Patrice Motsepe, Rais wa CAF ambaye yuko njiani kuelekea Arusha kuhudhiria Mkutano wa Mwaka wa CAF unaoanza Jumatano 10/08/2022.
Kuwepo Kwa Motsepe kwenye Tamasha Hilo kunamlazimisha Kwa njia moja au nyingine Karia naye kuwa karibu na bosi wake. Hii itajenga picha gani hasa Kwa mashabiki watafuta sababu? Karia ni Simba ndo maana hakuhudhuria Tamasha la Yanga.
Ukiwa kiongozi huwezi kukosa upande, lakini mara nyingi Karia umekuwa ukichanga vibaya karata zako na naamini ipo siku utalamba Galasa.
Leo ni Tamasha kubwa la timu ya Simba (S. S. C DAY) linaloazimishwa August 8 Kila mwaka Tangu mwaka 2009. Ni Tamasha kubwa linalovuta hisia si Kwa wapenzi na mashabiki wa Simba pekee bali wa vilabu vyote ndani na nje ya Tanzania Kwa jinsi linavyovuta hisia za Soka.
Tarehe 6/08/2022 siku mbili tu zilizopita Yanga walikuwa na Tamasha kubwa kama hili pale pale Uwanja wa Mkapa Temeke Dar es salaam. Mgeni rasmi katika tukio Lao alikuwa Kinana Makamu mwenyekiti wa CCM Taifa. Mbali ya ukubwa wa Tamasha lile na umuhimu wa timu hiyo kama ilivyo Kwa Simba kuhusu soka la nchi hii, Viongozi wote wa juu wa TFF hususan Karia Kwa upekee kabisa hawakufika, hawakuhudhuria.
Leo Simba Wana tukio kubwa na naambiwa mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Patrice Motsepe, Rais wa CAF ambaye yuko njiani kuelekea Arusha kuhudhiria Mkutano wa Mwaka wa CAF unaoanza Jumatano 10/08/2022.
Kuwepo Kwa Motsepe kwenye Tamasha Hilo kunamlazimisha Kwa njia moja au nyingine Karia naye kuwa karibu na bosi wake. Hii itajenga picha gani hasa Kwa mashabiki watafuta sababu? Karia ni Simba ndo maana hakuhudhuria Tamasha la Yanga.
Ukiwa kiongozi huwezi kukosa upande, lakini mara nyingi Karia umekuwa ukichanga vibaya karata zako na naamini ipo siku utalamba Galasa.