Leo najipongeza, nitakula ulabu mpaka kucheee..

Leo najipongeza, nitakula ulabu mpaka kucheee..

Kashaijabutege

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2010
Posts
2,696
Reaction score
740
Ndugu wana JF

Niwashirikishe furaha yangu ya kuwa leo nimeweza kulipa karo za wanangu sita. Kwa furaha hii, nimepanga kidogo kilichobaki nikalambe ulabu (ndovu baridiiii) na nibakize sadaka kwa ajili ya kumshukuru Mungu Jumapili. Nawaombea ambao bado hawajatimiza jukumu hili muhimu, Mungu akazibariki kazi zao halali ili nao wakamilishe jukumu hili.

Nasema :welcome:katika kijiwe changu hapa Kabuteigi tule vitu.
I wish you an enjoyable week-end while drinking responsibly. I love you all.
 
Ndugu wana JF
Kwa furaha hii, nimepanga kidogo kilichobaki nikalambe ulabu (ndovu baridiiii)

Sio Kwamba hicho kidogo ukifungulie Fixed Account ili kila mwezi uongezee, ili mwaka kesho usipate hizi tabu tena zilizokupata mwaka huu???
 
Ndo tatizo la Wazazi wetu kama hawa hawana PLAN hata hawazi kesho itakuwaje!!
Anachowaza ni ULABU 2,Vipi hapo home m2 akiugua ghafula ume2nza chochote??!!

Sio Kwamba hicho kidogo ukifungulie Fixed Account ili kila mwezi uongezee, ili mwaka kesho usipate hizi tabu tena zilizokupata mwaka huu???
 
Sio Kwamba hicho kidogo ukifungulie Fixed Account ili kila mwezi uongezee, ili mwaka kesho usipate hizi tabu tena zilizokupata mwaka huu???

Kuwashirikisha furaha yangu haina maana kuwa nimepata shida sana kupata karo za wanangu. Nia ni kupeana moyo na wengine ambao wana jukumu kama hili. Naichukulia JF kama familia moja ingawa hatufahamiani au hatukai sehemu moja. That was the only reason. Kwa taarifa, kidogo ninachokisema ni kile nilichowithdraw (leo) kutoka benki na si kwamba akaunti haikubaki na kitu kabisa. I am liquid enough.

Hata hivyo nakushukuru kwa ushauri ingawa benki haziruhusu kudeposit pesa kila mwezi katika FDR. As a new invention, thanks for your advice.
 
Hongera sana mkuu wetu..
Umefanya vizuri sana kuweka kipaumbele kwa hawa kizazi kinachoendelea.
Nakupa goahead hapo kajinunulie Tusker kadha, bili kwangu.
 
Ndugu wana JF
nimepanga kidogo kilichobaki nikalambe ulabu (ndovu baridiiii) na nibakize sadaka kwa ajili ya kumshukuru Mungu Jumapili.

Kuwashirikisha furaha yangu haina maana kuwa nimepata shida sana kupata karo za wanangu.
kidogo ninachokisema ni kile nilichowithdraw (leo) kutoka benki na si kwamba akaunti haikubaki na kitu kabisa. I am liquid enough.

Hata hivyo nakushukuru kwa ushauri ingawa benki haziruhusu kudeposit pesa kila mwezi katika FDR. As a new invention, thanks for your advice.

Samahani ndugu kwa kutokukuelewa mimi ulivyosema kilichobaki nilidhani ni KILICHOBAKI... pili hapo kwenye BOLD am sure kuna Accounts kama vile Nyota Children Account angalia hapo chini:- Nyota Childrens Plan : Exim Bank, An Edge Above The Rest

Nyota


This Children's account is designed to help parents, to meet financial constraints such as rising cost in education and the basic necessities. To beat the inflation costs, parents need to save money and invest wisely.
  • Monthly saving - Invest/deposit a fixed, small amount* every month in the name of your children. *(Minimum balance - T.Shs. 10,000)
  • Specific term - You can make deposits for a period of 3 / 5 / 7 years.
  • End of term benefits - a healthy accumulated sum with interest.
  • Gifts - These deposits units can be gifted to only child relative.
  • Age Group criteria - Below 18years.
 
Hongera kwa kukamilisha malengo! ila kama ukiweza achana na mipombe haina issue. Utaishia kujuta tu asubuhi baada ya ulabu kuisha kichwani.

Tena na ninyi wahaya mnapokunywa pombe yote inahamia chini kwenye utu uzima ( i am sure unanielewa)
 
Hongera kwa kukamilisha malengo! ila kama ukiweza achana na mipombe haina issue. Utaishia kujuta tu asubuhi baada ya ulabu kuisha kichwani.

Tena na ninyi wahaya mnapokunywa pombe yote inahamia chini kwenye utu uzima ( i am sure unanielewa)

Ahsante ndugu yangu. Mie pombe inaishia kichwani. Mimi nikinywa nakuwa 'bright' na 'creative'. Kama hunywi, basi jaribu moja leo nitakulipia.
 
Ndugu wana JF

Niwashirikishe furaha yangu ya kuwa leo nimeweza kulipa karo za wanangu sita. Kwa furaha hii, nimepanga kidogo kilichobaki nikalambe ulabu (ndovu baridiiii) na nibakize sadaka kwa ajili ya kumshukuru Mungu Jumapili. Nawaombea ambao bado hawajatimiza jukumu hili muhimu, Mungu akazibariki kazi zao halali ili nao wakamilishe jukumu hili.

Nasema :welcome:katika kijiwe changu hapa Kabuteigi tule vitu.
I wish you an enjoyable week-end while drinking responsibly. I love you all.
tuko pamoja... nimelimss Frijilangu.... ni vyombo mpaka majogooo!!!zikiisha nahamia..
 
Sio Kwamba hicho kidogo ukifungulie Fixed Account ili kila mwezi uongezee, ili mwaka kesho usipate hizi tabu tena zilizokupata mwaka huu???

jamani mwacheni a enjoy maisha kidogo ...
kaiweka familia yake kwanza (hongear sana)
na sasa naye afurahie maisha ....
msileta maisha ya kizungu sana
ndo maana wengi wako wanakuwa na depression ...
live like there is no tomorrow...
ungesema nusu ya hiyo kidogo aiweke bank na nusu aka jipongeze hapo ndo ningekuelewa...
 
jamani mwacheni a enjoy maisha kidogo ...
kaiweka familia yake kwanza (hongear sana)
na sasa naye afurahie maisha ....
msileta maisha ya kizungu sana
ndo maana wengi wako wanakuwa na depression ...
live like there is no tomorrow...
ungesema nusu ya hiyo kidogo aiweke bank na nusu aka jipongeze hapo ndo ningekuelewa...
Nimemuuliza kulingana na alivyosema kwenye wording zake, kidogo kilichobaki kumbe shida ilikuwa kwenye definition ya KILICHOBAKI, kumbe kilibaki katika zile alizodraw na sio kwamba chote kilichobaki benki.... now if the former was true basi ingebidi a-save lakini alivyonielewesha kwamba hizo karo zilikuwa ni vijisenti tu na benki bado ana pesa nyingi basi ndo nikamwambia hakuna noma..... i
 
Nimemuuliza kulingana na alivyosema kwenye wording zake, kidogo kilichobaki kumbe shida ilikuwa kwenye definition ya KILICHOBAKI, kumbe kilibaki katika zile alizodraw na sio kwamba chote kilichobaki benki.... now if the former was true basi ingebidi a-save lakini alivyonielewesha kwamba hizo karo zilikuwa ni vijisenti tu na benki bado ana pesa nyingi basi ndo nikamwambia hakuna noma..... i

haya kama mmeelewana basi..
na mie nafurahi....
 
Ndugu wana JF

Niwashirikishe furaha yangu ya kuwa leo nimeweza kulipa karo za wanangu sita. Kwa furaha hii, nimepanga kidogo kilichobaki nikalambe ulabu (ndovu baridiiii) na nibakize sadaka kwa ajili ya kumshukuru Mungu Jumapili. Nawaombea ambao bado hawajatimiza jukumu hili muhimu, Mungu akazibariki kazi zao halali ili nao wakamilishe jukumu hili.
 
hongera mpendwa kwa kutimiza wajibu muhimu kwa familia yako. nimevutiwa na kitu kimoja kwamba baada ya kulipa (naamini umelipa ada za mwaka mzima na sio nusu) ndio unatumia kilichobaki. ingekuwa kinyume chake ningekukemea kwa ukali sana. pia umekumbuka sadaka na kushauri wengine wanywe responsibly. lakini usipuuze waliyoshauri wengine, mwisho wa kulipa za mwaka huu ndio mwanzo wa kuhifadhi utakazolipa mwaka kesho. it is a circle of responsibilities. enjoy your drinks both responsibly and responsively and God bless you mpenzi
 
Naungana na wewe kukupongeza watoto sita si mchecho na huu mwanzo wa mwaka hongera ,uko mitaa gani nami nijongee
 
Halafu ongezea na Grants tot tatu hivi ili ulale vizuri..! Hongera sana
 
Ndugu wana JF

Niwashirikishe furaha yangu ya kuwa leo nimeweza kulipa karo za wanangu sita. Kwa furaha hii, nimepanga kidogo kilichobaki nikalambe ulabu (ndovu baridiiii) na nibakize sadaka kwa ajili ya kumshukuru Mungu Jumapili. Nawaombea ambao bado hawajatimiza jukumu hili muhimu, Mungu akazibariki kazi zao halali ili nao wakamilishe jukumu hili.

Nasema :welcome:katika kijiwe changu hapa Kabuteigi tule vitu.
I wish you an enjoyable week-end while drinking responsibly. I love you all.

Ndio mzee jipongeze, na mi nakupongeza, karibu chai.
eeh na wakati mwingine sio lazima watu wakupongeze kweli,
mmmmh Raha jipe mwenyewe aisee.
 
Ndugu wana JF

Niwashirikishe furaha yangu ya kuwa leo nimeweza kulipa karo za wanangu sita. Kwa furaha hii, nimepanga kidogo kilichobaki nikalambe ulabu (ndovu baridiiii) na nibakize sadaka kwa ajili ya kumshukuru Mungu Jumapili. Nawaombea ambao bado hawajatimiza jukumu hili muhimu, Mungu akazibariki kazi zao halali ili nao wakamilishe jukumu hili.

Nasema :welcome:katika kijiwe changu hapa Kabuteigi tule vitu.
I wish you an enjoyable week-end while drinking responsibly. I love you all.

Hapo kwenye bold, kama wewe ni mkristo anayeujua Ukristo, sadaka haiwezi kuwa kile ambacho ni masalia ya matumizi yako, ni vema ungetenga kabisa sadaka na sio kusema kitakachobaki ndio sadaka.

Nakupongeza kwa kuweza kulipa karo ya wanao sita, hasa kama ni zile shule ghali(wengine wanatuibia tu), ila kama ni hizi za kata za elfu ishirini ni kawaida tu mkuu huhitaji kupongezwa saaana.
 
Back
Top Bottom