Leo ndio nimejua kwanini TANESCO wamegoma kushusha bei ya umeme hata baada ya Bwawa kuanza kazi mwakani

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
38,920
Reaction score
44,970

==========================

Tangu Maharage pale TANESCO alipotoa tamko lisilo na mantiki na linalo-defy all logical reasoning, kwamba eti hata baada ya Megawatt 2100 kuanza kuzalishwa kwenye bwawa la Nyerere na kuingizwa kwenye Gridi bado eti umeme hautashuka bei, nimekuwa nikiwaza sana nisielewe hii itawezekana vipi?!

Ni kwamba Law ya demand vs Supply inagoma kabisa!! Kwamba matumizi yetu hivi sasa ni Megawatt 1,600, na ndizo zinazalishwa kwa sasa, halafu ghafla uingize Megawatt 3,700 kwenye gridi, huo umeme wote atautumia nani kwa ghafla hivyo hadi uishe?

Tulitegemea kwa kuwa umeme hauwezi kutunzwa kwenye betri, kwamba Tanesco washishe bei ili hadi vijijini wapikie majiko ya umeme, kiasi umeme huo sasa utumike wote bila kupotea, vinginevyo itabidi tufungulie maji bwawani yamwagike bire bila kuzalisha umeme.

Sasa leo ndio nimejua mchezo wanaotaka kufanya, ni mwamba hizo Megawatt 2,100 za Bwawa la Nyerere tutazisikia kwenye bomba tu, maana zitaingizwa kwenye gridi ya taifa na kuwa offloaded kwenda Zambia, Malawi, Uganda, Kenya ,Zanzibar, Burundi, Rwanda, Msumbiji, na hata sentano mbuni hatutaiona ya mauzo ya umeme. How? Kwanini nasema hivi?

1.) Umeme huo hautaonekana kwamba umetoka Tanesco, bali kuna dogo mmoja inadaiwa ni mtoto wa mama yetu, yeye kaongozana eti na maafisa wa Wizara ya Nishati ili azalishe umeme wa Solar na kuiuzia Uganda , πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚, kwamba umeme utoke Rufiji, mseme ni umeme jua wa huyo dogo? Halafu malipo yote alipwe yeye?!! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ , ujamja wa kizani sana huu...

2.) Inadaiwa January Makamba anakazana sana kuunganisha gridi ya Tanzania na Gridi za Rwanda kupitia Rusumo, na anafanya mikutano na nchi nyingi zinazotuzunguza hasa malawi, Zambia na wengine eti tuunganishe gridi yetu kwa pamoja ili tuuziane umeme panapokuwa na upungufu. Shida hapa ni kwamba umeme utatoka Rufiji halafu watasema ni umeme wa gesi, hivyo malipo yataenda kwa wenye gesi yao.., sisi tutabaki kulipa mkopo wa Trillion 10 zilizotumika kujenga hiko bwawa, kwa tozo za miamala na kodi za majengo za kwenye umeme zilizopoandishwa.

Hivi mtu mwenye akili timamu unakubali vipi kuambiwa kwamba Megawatt 2,100 ziingizwe kwenye gridi na bado zote zitumike ziishe bila kushusha bei?!!!

We are finished!! Tumekwisha...



I can’t imagine huyo mama abaki hapo hadi 2030, kweli?!! Tanganyika Tutakuwa na hali gani sisi, si tutakuwa tunatembea tunaongea wenyewe kama wehu?!

=========================








Update: 24/04/2024

View: https://www.instagram.com/p/C6HWnolCz_q/?igsh=NGVrbTZmeW5uNmxk
=========================
03/07/2024


View: https://youtu.be/yf2io4O9o2A?si=EUCBr_yO975LU3NV
======================
Sasa yamekuwa, Abdul kuiuzia Tanesco umeme toka Uganda

 
Ujinga ni mzigo kwa hiyo kampuni za kitanzania kwenda kuuza umeme ili kutuletea kipato nayo ni nongwa?

Yaani tayari ni ajenda ya kisiasa sisi masikini kama tunaweza kupata vya kuuza ili tujiingizie kipato ni jambo zuri sio tu kuuza mahindi na maharage.

Kama tunauza na umeme jambo zuri sana hata awe mtoto wa nani binafsi nasupport kampuni za kitanzania kufanya hivyo.

Sio kila siku zinakuwa tu kampuni za kigeni kufanya hivyo napongeza sana kampuni ya tanzania inayofanya hivyo.
 
Kwaiyo umeme uzwee Bibi zako vijijini waendelee kuwa na macho mekundu na kuumwa vifua sasababu ya Moshi .ujinga mzigo RIP MAGU
Acha ujinga basi mtoa post si kasema wanaenda kuuza wa solar hao watu binfsi.

Ila kwa akili zake na hofu zake tu ndio anadhania utauzwa huu wa umma lakini pia na hata huu wa umma ikitokea mara zote kinachouzwa ni ziada siku zote wapi wamesema kuwa watauza kile kinachohitajika.

Halafu wananchi watakosa tusiwe watu wa ajabu ajabu kwa kuwa bwawa la rufiji tu likikamilika ukiacha hizo solar za watu binafsi linatosha umeme kutumiwa nchi nzima na ziada inabaki.

Achillia mbali vyanzo vingine vya umeme vilivyopo kwa hio hata ukiuzwa nje ni sawa kwa ziada itakuwepo labda tu useme ndani ya muda mfupi kuzaliwe miradi mikubwa mno ya kuhitaji umeme sana kuzidi huo uzalishaji na ndio ktk hili la rufiji Magufuli tutamkumbuka milele ni mradi mkubwa wenye manufaa ndani ya nchi kwa maana ya kupata umeme na nje ya nchi kwa maana ya kuuza.

Huwezi kuutoa bure kwa wananchi wakati kuna madeni na kuna mambo ya kimaendeleo nchi inataka.

Hatuna mjomba wa kutubeba lazima tuiingize kipata kwa hiyo nasupport kampuni binafsi kuzalisha wao na kuuza na pia nasupport kampuni ya umma kuzalisha na kuuza zote tu zinaleta kipato nchini tena fedha za kigeni uchumi ukue.
 
Kwani lengo la mradi lilikuwa ni lipi? Malengo yalikuwa ni kushusha bei ya umeme kwa kuwa umeme wa maji ni wa gharama nafuu na ni mwingi, hivyo kushuka kwa bei kungechagiza ukuajia wa giwamda, kutoa ajira na kupaisba uchumi.., sasa kama wana-deviate kutoka kwenye objectives kwa maslahi yao binafsi n iuonevi kwa wanachi watakaowajibika kulipa hizo trillion 10 za mkopo ambazo zinakamuliwa kwenye tozo za miamala na kodi za majengo kupitia Tanesco
 
Mleta uzi nimemuelewa vizuri shida sio kuuza umeme nje ya nchi ,shida ni mauzo ya umeme kuingia kwenye mfukoni mwa mtu binafsi.
 
Aisee.. Sitaki kujua kinaendelea nini.
Wao ndio wana nchi.. bana!
Hutaki kivipi?! Lengo la mradi wa Rifiji ulikuwa ni kuzalisha umeme mwingi wa bei nafuu ili kuwapa wananchi unafuu wa maisha na kuchagiza ukuaji wa viwanda na unazalisha kwa ajili ya kutoa ajira kwa vijana na kukuza uchumi. Sasa ni kwanini leo hii wantuhujumu kwa makusudi, Megawatt 3700 zinaingizwaje kwenye gridi na bado umeme usishuke , how? Hapo ni kwamba utauzwa na pesa kuingia mfukoni huku tukikamulowa tozo za miamala na kodi za majengo kuulipa mkopo wa trillion 10 tuliokopa kujenga bwawa.., inaumiza sana.
 
Ni muhimu huyo Maharage aeleze vizuri ni kwanini bei ya umeme isishuke baada ya bwawa kukamilika na hizo megawatts kuanza kutumika ???!

Basi kulikuwa na haja gani ya kupoteza pesa nyingi namna ile kama hao walipaji wa hizo pesa hawatanufaika na huo mradi ??!!
 
Mh. Samia simkubali hata kidogo jinsi anavyo endesha nchi lakini kuhusu biashara halali ya kijana anayedaiwa kuwa mtoto wake sioni tatizo lolote.
Kwani mtoto wa raisi siyo binadamu kama wengine? Hana uwezo, akili na haki ya kufanya biashara halali?

Hapa umeleta tuhuma nzito zilizo egemea kwenye hisia zaidi kuliko uhalisia na ukweli.
Acha kuchafua watu.

#MkatabaWaBandari-ni-uhuni-tupu_KataaDPWorld.
 
Mkuu wangu.. Wachache kwenye nchi ndio wenye maamuzi ya mwisho.. Siku kama nchi ikiamuka huenda kukawa na nafuu . ila sasa hivi watu bado wanadanganyika na vitu vidogo sana na kuna wasariti
 
Tatizo Watu wako busy na simba na yanga Diamond mkuu hawa ccm ni zaidi ya upigaji.
 
Mungu anawaona !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…