Leo ndio nimejua kwanini wanawake wanajiingiza katika tabia za udangaji

Leo ndio nimejua kwanini wanawake wanajiingiza katika tabia za udangaji

Hapa nilipo nina majonzi, roho imeniuma sana kwa kuzaliwa kwenye familia maskini

Ipo hivi mimi kwetu ndio wa mwisho msichana peke yangu kati ya watoto 6.. Mzee wangu alitangulia mbele za haki hivyo tumebaki na mama tu.. hao ndugu zangu wote hawana maisha ya kueleweka isipokuwa mmoja tu angalau yeye ameajiliwa serikalini ndio kidogo anaibeba familia, yeye ameshaoa ana familia yake

Mimi nimeshahitimu chuo nina kama Miaka miwili nyumbani.. nimepata sehemu ya kujishikiza wananilipa 250000.. Kwetu ni bunju nafanyia kazi magomeni kila siku natumia 5000 yaani 3000 nauli 2000 nakula mchana hapo Ndio najibana mno..

Sasa kwasasa Hivi nyumbani Hakuna mtu nipo peke yangu mama ameenda kijijini kwao bibi anaumwa, mama yangu hana kazi ile ya kumtegemea anauza chupa za maji hivyo siwezi kumsumbua kwa chochote, amesafiri hajaniachia hata shilingi 100.. Hakuna chakula ndani Hakuna chochote, nachofanya nikitoka kazini nashukia kwa brother nakuta wamepika nakula naondoka

Leo nimeumia sana sijaenda kazini Nina siku 2 sina nauli hela niliokuwa nayo akiba imeisha nimemuomba bro kasema yeye hana hela hawezi kuwa anatoa hela mara mbili mbili kwa familia yake na kwangu, Kama niliweza kutafuta kazi basi nijitegemee nauli nikitaka kula nije nyumbani,, nikamuuliza sasa nitatoa wapi na Ndio naanza kazi akanijibu nitajua mwenyewe

Hiyo kauli imeniuma yaani anamaana gani kusema nipambane nitafute nauli yaani naitafutia wapi ..

Leo nimeacha kuwa judge Watu na maisha wanayoishi Kama ndugu yangu wa damu ananiambia maneno haya hao wa nnje watanijibu vipi

Ni hayo tu wakuu
Wewe si una kazi umesema Sasa si uende kazini.?
 
Waheshimu mashoga tafadhari, wako wanaojitambua na wanatumia jasho lao la halali, tena wengine wanahudumia mabasha wao. Kwa kifupi wanalea marioos na viben10.
Hata majambazi, wauzaji nao Wanahudumia ndugu zao na familia zao lakini haihalarishi matendo yao.
 
Me kweli roho mbaya ninayo, hujakosea. Lakini ni watu kama wewe ndo mmenifanya niwe na roho mbaya kwa sababu wengi wenu sio wa kweli. Duniani hapa mmetufundisha ukatili sana. Kwanini mdanganye kwenye maswala serious..?

Nimesema ndugu Kama unaona nimedanganya si uweke hapa taarifa zangu yanini kuandikia mate!!



Yaani ni sawa na kusema wanawake ni mbwa kwa vile umeumizwa na mbwa mmoja

Siko hapa kubishana Kama unahisi nadanganya achana na huu uzi nenda kasome uzi usiodanganya mkuu ni rahisi tu
 
Itakua huongei na watu wakakuambia story zao. Watu wengi ndio walivyoanza maisha, kuna watu walikua wanatembea km 6 kufika kazini na nawahi ili aoge hapo hapo kazini nabadiri nguo zenye jasho, watu wakifika kazini wa amkuta ni msafi kumbe katembea kwenda kazini.

Kuna watu wamepanga vyumba vya 25k huku hana godolo analala chini kwa mwaka mzima akiwa anasave ili anunue godolo.

Hivi ndivyo watu wengi mjini wanavyoanza maisha, kama unahisi kila mtu alipopata kazi mara ya kwanza alikua na ka ist ka kumpeleka job na uhakika wa milo mitatu unajidanganya.

Muhimu ni kukomaa huku ukitunza utu wako.. ukijishusha ukaanza kudanga utakua mtumwa, utafanyiwa mambo ya ajabu ambayo hukuwahi kuota kwamba kuna binadamu wanafanyiwa sababu ya kupenda pesa.. usiwaone hao wanaodanga kuna mengi hawawezi kukusimulia.
 
Sasa usilalamike kusimangwa na kaka yako, na kifuatacho atakufukuza. Hapa wadada wote tutakwambia vumilia ila ukweli na wao wamewapanga masponsor sababu wanawake nature yetu kupokea na sio kutafuta
Aisee..! Nikifika wakati wa kuhitaji kuoa nitaongea na wazee wanitafutie mwali kijijini
 
Sasa usilalamike kusimangwa na kaka yako, na kifuatacho atakufukuza. Hapa wadada wote tutakwambia vumilia ila ukweli na wao wamewapanga masponsor sababu wanawake nature yetu kupokea na sio kutafuta
Vidada vya dizaini hii ndio tunapigianaga pasi za kina gaucho... Eti mwanamke asili yake kupokea sio kutafuta wenzio kibao wanapambana nowadays... Eti ooh tafuta sponsor wa nyoli nyoli... Afu ndio utake haki sawa kwa wote??? Haki na jala yangu umekula... Yaani Itakua kama nachinja kuku
 
Back
Top Bottom