The Icebreaker
JF-Expert Member
- Feb 11, 2018
- 22,278
- 65,817
Robert Nesta Marley maarufu zaidi kwa jina la Bob marley,alifariki siku kama ya leo 11-may-1981
Bob marley alizaliwa Jamaica tarehe 6-2-1945 kwa mama mjamaica Cedella malcolm booker,na baba yake ni mzungu Norval marley mwenye asili ya Uingereza,
Bob marley alipata umaarufu na mafanikio zaidi kupitia nyimbo zake za One love,Zion train,Iron lion zion,No woman no cry,Buffalo soldier,Zimbabwe,Africa unite,Three little birds,Waiting in vain,Is this love,Get up stand up,Positive vibration,Wake up and live,Redemption song,Exodus na nyinginezo nyingi,
Bob aliacha watoto 11 wawili wakiwa wakuasiliwa,Sharon na Stephanie ambao Rita aliwazaa na wanaume wengine,
Watoto wake wengine wa Bob ni;Cedella,David "ziggy",Stephen,Robert "robbie",Rohan,Karen,
Julian,Ky-mani na Damian,
Siku za mwisho akiwa kitandani hospitalini,rasta zake zilinyolewa kutokana na hali aliyokua nayo kiafya,
Bob alifariki akiwa na miaka 36 tu mjini Miami USA may 11-1981 kwa ugonjwa wa melanoma (skin cancer) leo ni miaka 37 toka kifo chake,
Bob marley alizikwa tarehe 21 may 1981 katika kijiji cha Nine mile nchi Jamaica,kijiji ambacho ndipo alizaliwa tarehe 6-2-1945.
Habari zaidi, soma=>CIA walimuua Bob Marley?
Historia na kumbukumbu ya kifo cha Bob Marley
Bob Marley aliamini Mungu kweli?