#COVID19 Leo ni siku ya Afya ya Akili, Je Watanzania tutumie chanjo ya Corona kama kipimo cha utimamu wetu?. Wapinga chanjo, sio wazima! Je ni vichaa?

Unamkuta mtu anaipinga CHANJO dhidi ya CORONA kwa kigezo kuwa zinatoka ULAYA kwa mabeberu....huku kila siku akimeza TEMBE DHIDI YA VIRUSI VYA UKIMWI....sasa sijui hizo tembe zinatengenezwa Lushoto Tanga?!!! 🀣
Kabla hajapata akili sawa sawa aliingiziwa mwilini chanjo ambazo hazijui vizuri lakini baada ya kupata uelewa anazipinga chanzo hizo!. Ni akili mbovu sana za ubishi na ujuaji ambazo kwa mujibu wa mleta mada ni sawa na kuwa kichaa kuwa nazo kichwani mwako.
 
Sasa mbona na hao mabeberu wanatumia hizo hizo chanjo?
Huenda mpaka sasa unapumua kwa hisani ya mabeberu!
 
kwa wanasiasa na viongozi vichaa ni wale WOTE waliokuwa wanasema chanjo haifai kipindi Dr. Magufuli akiwa hai, lakini baada ya kuwa ameuliwa wanasema chanjo inafaa.

kwa wananchi vichaa ni wale wote waliochanja.
Marehemu akifufuka atakimbia fastaa kupiga chanjo!
 
Mkuu tatizo watu washazoea kufuata maagizo ya waganga na viongozi wao wa dini... Kule hawaruhusiwi kuhoji hoji vitu! Ni Tawire na Amina!
Watasomesha watoto wao shule ghali ghali kusudi wapate elimu lakini hawataheshimu taaluma zao wakianza practice!
 
kwa wanasiasa na viongozi vichaa ni wale WOTE waliokuwa wanasema chanjo haifai kipindi Dr. Magufuli akiwa hai, lakini baada ya kuwa ameuliwa wanasema chanjo inafaa.

kwa wananchi vichaa ni wale wote waliochanja.
Mkuu hata wewe hapa unaviashiria vingi sana vya ukichaa... Pamoja na kwamba unajua kuandika, kusoma na kuvaa
 
Mkuu hiyo mifano uliyoitoa ni viashiria vikubwa sana ya ukichaa. Mitaani huku wengi ni vichaa kisa dini. Wengine ni vichaa kisa Simba, Yanga na zile timu zao za Ulaya wasizozijua vizuri!
Tafuta kwanza maana ya ukichaa utakubaliana na mimi!

Ndio maana nimesema inategemea unautafsiri vipi ukichaa. Na kama ukichaa una tafsiri na maana moja, haiwezekani mtu akawa kichaa kwenye eneo moja lakini sio kichaa kwenye eneo jingine.

Kama umeajiriwa kuna mtu ana kuona hamnazo, na wakati wewe unamshangaa anaebeza kuajiriwa, Je, hapo kuna chembe chembe za ukichaa kuhusika?
Na kama zipo, ni upande upi una ukichaa? Na vigezo vipi vinatumika kuhitimisha huo upande una matatizo ya akili?
 
Ni kigezo gani kimetumika kuichagua chanjo ya Corona? Je kuichagua chanjo ya Corona na kuziacha nyingine sio ukichaaa?
Ni ukichaa! Kuchanja mwilini chanjo isiyo kukinga na ugonjwa kwa 100%, nao ni ukichaa! Kuendesha kampeni za kuchanja, ni ukichaa!
 
Ni ukichaa! Kuchanja mwilini chanjo isiyo kukinga na ugonjwa kwa 100%, nao ni ukichaa! Kuendesha kampeni za kuchanja, ni ukichaa!
Hivi hao jamaa hawaelewi hiyo chanjo ni biashara kubwa! Vichaa ndo nyinyi mnaodai chanjo inasaidia wakati ufanisi wake haueleweki!
 
Nadhani tumuulize Antony Diallo alisema miaka mitano nyuma kuna kiongozi alikua na file mirembe ila akapewa ofisi kubwa tuanzie hapo.
 
Sasa naanzaje kumsaidia Gwajima?
 
Kuna aina kumbi na mbili za ukichaa, ukichaa sio kutembea uchi barabarani wala si kutembea na karabai in a neon dsy light hata kuna vichaa waliondani ya suti kuna vichaa wanaoanzisha hata nyuzi JF. Nsalo jile 12.

Hata kugombea ubunge ukaforce kuchaguliwa na ukapata wakati hufai kuwakilisha wananchi na unajua umeenda kwa egos zako binafsi ni ukichaaa

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Hakika 😍😍
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…