Leo ni siku ya aibu sana kwa Utawala wa Hayati Magufuli baada ya Sabaya kukiri alikuwa akitumwa kutekeleza uovu

Tafsiri yako hiyo inaamanisha 'Ujamaa' sio 'demokrasia'
Demokrasia ni uhuru usio na udhibiti kila mmoja anachokiwaza kufanya ni ruksa lakini ujamaa unazingatia maadili na anayekiuka huchuliwa hatua kali kwa mjibu wa sheria.
Demokrasia ni maisha yanayofuata utaratibu na siyo kuishi kiholela.
 
Hata wasemeje hakuna hata mmoja atafuta mazuri ya JPM kwenye ufahamu wangu, alafu ni aibu sana kundi kubwa sana la watu wanatumia nguvu kubwa kujaribu kumchafua maiti asiye na uwezo wa kuamka kujibu lolote, Jpm kama alikuwa muovu kiasi hicho basi uovu wake tulikuwa tuna uhitaji watanzania wengi sana. RETURN IF POSSIBLE FATHER
 
Weka majina ya watanzania waliokufa na njaa kwa sababu ya bei!! Otherwise ni mihemuko tu na kukariri maneno kama kasuku!

Mbona wewe mwenyewe hujafa njaa
Kwa hiyo vipi mnavyosema magufuli aliua watu wengi mbona wewe hujauliwa? ni sawa na mfano uliotoa hapo juu tunazidi kuyatunza maneno yenu wanafiki wa hii nchi!!!!!!!
 
Kwa hiyo vipi mnavyosema magufuli aliua watu wengi mbona wewe hujauliwa? ni sawa na mfano uliotoa hapo juu tunazidi kuyatunza maneno yenu wanafiki wa hii nchi!!!!!!!
Kama Magufuli angeendelea kuwa hai, pengine kufika leo angekuwa kisha muua baba yako, sidhani kama ungeandika pumba hizo
 

Umeongea Ukweli mchungu kwa maneno mepesi sana.
 
Ndiyo maana Magufuli aliitwa DIKTETA UCHWARA kwa vile allikuwa anapoua ana acha traces. Alikuwa hana akili ya ku deal na opposition au critiques, aliamini katika kutumia vyombo vya dola kushinikiza. Akasahau vyombo vya dola siyo mali yake.

Na cha moto akakipata mwenyewe Machi 17, 2021
 
Kwa nchi hii UDIKTETA ni Muhimu Sana Kutokana Aina ya kizazi kilichopo.

Hivi jaribu kutafakari mtu amepewa dhamana anaruhusu kuingizwa Kwa Sumu au DAWA zilizokwisha muda wake na zinawaua Wananchi wasio na hatia unadhani huyu anastahili adhabu gani? Haya tuseme akamatwe apelekwe Mahakamani na afungwe jela. INAWEZEKANA??

KUNA MAUAJI NA UDIKTETA MKUBWA UNAFANYIKA UKIWA UMEMEFICHWA KWENYE KOTI LA DEMOKRASIA NA HAKI ZA BINADAMU LAKI KWA UPANDE MWINGINE NI NAFUU KABISA HATA WALE WANAOFYEKWA HADHARANI KWA RISASI.

HAWA MAFISADI,WASIMAMIZI WA HIKI NA WATOA HUDUMA MBALIMBALI ZA UMMA WANAOPINDISHA HAKI KWA MASLAHI YAO BINAFSI UNADHANI WANASTAHILI ADHABU GANI?
 
Alikua anafanya ugaidi au alikua anadili na magaidi na fisadi kwenye kikosi maalum? Kutumwa na rais kwa kazi maalum mbona kawaida tu na sio kinyume cha katiba. Fisadi mliyoshughulikiwa ndio muda wenu sasa chini ya msaliti samia.
 
Alikua anafanya ugaidi au alikua anadili na magaidi na fisadi kwenye kikosi maalum? Kutumwa na rais kwa kazi maalum mbona kawaida tu na sio kinyume cha katiba. Fisadi mliyoshughulikiwa ndio muda wenu sasa chini ya msaliti samia.
Vibaka zama zenu zimekwisha, hata choo hamjajenga, mmeishia kukaririshwa propaganda
 
Hata Kama Ni Wewe Utashindwa Kumsingizia Marehemu ili Uachiwe..
Hakuna cha kusingiziwa kwanza Sabaya alionewa sana kwa sababu watu wa kariba yake walibaki uraiani wakitamba mfano:-Makonda,Mnyeti,Musiba,Bashir Ally,Polepole,Gambo,Kihongosi,Homera,Heri James nk.
 
Alikua anafanya ugaidi au alikua anadili na magaidi na fisadi kwenye kikosi maalum? Kutumwa na rais kwa kazi maalum mbona kawaida tu na sio kinyume cha katiba. Fisadi mliyoshughulikiwa ndio muda wenu sasa chini ya msaliti samia.
Jibu baya kuwahi kutokea,ni aibu mtu kushabikia mauaji.
 
Kwani utawala wa sheria dhana yake ni nini? Huo UDIKTETA unaotaka kuutetea hapa una mapungufu sana. Kwa kuwa mtu mmoja huendesha nchi kadri ya hisia zake zinavyomtuma. Unaona mambo aliyokuwa anafanya Magufuli? Kama kusitisha mikataba ya madini kwa vile tu amejisikia. Sasa hivi kuna mashauri kama 3 huko ICSD. Hata kama Demokrasia ina mianya lakini ndiyo utawala wa kistaarabu
 
Uhalifu unaofanywa na awamu ya sita ni mbaya zaidi kuliko kipindi cha sabaya maana kwa sasa wtz wengi wanakufa kwa njaa inayotokana na kupandisha bei ya vyakula hovyohovyo akisaidiwa ba chawa wake
mbona we uko hai unajijambia hapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…