Leo nimekumbuka namna mpenzi/ mama wa watoto wangu alipoanza kunishinda kipato baada ya kupata kazi kila kitu kikaparaganyika

Leo nimekumbuka namna mpenzi/ mama wa watoto wangu alipoanza kunishinda kipato baada ya kupata kazi kila kitu kikaparaganyika

Glory be to God
Miaka 5 nyuma nilipatwa na hiki kisa, sijui huwa kuna nini kinatokea kwa wenzetu naweza kusema alikuwa mke kabisa maana kwao walinifahamu posa na mahari nilishamaliza na watoto wawili nimemzalisha sasa kipindi chote hicho alikuwa anafanya shughuli ndogondogo tu.

Sasa ikatokea fursa sehemu nikamwambia mama kwa haya maisha tunayoishi itachukua muda kutoboa hapa ebu kamatia iyo fursa ya kazi tusaidizane bwana bwana bwana kumbe ndio nilikuwa namaliza familia yangu wakuu kitendo cha yeye kupata ile kazi tu na vile nilimtumia mtu ninayemjua ilikuwa rahisi sana kwake kutoboa.

Picha linaanza kwanza amepangiwa mkoani akili ikacheza mmh nikiwa nipo kwenye dilema ya maamuzi kwao wakawa wapo karibu nae zaidi na wakamwambia aende huko kwa kuwa watoto bado wadogo waende kwa bibi yao yaani mama yake hadi mambo yatakapokuwa sawa kule then awachukue.

Basi mwezi ukaisha mwezi wa pili mara miezi sita nikaanza kuona mapicha picha kwanza sikuwahi kuona hela yake ingawa alikuwa analipwa mara 4 ya mshahara wangu bado nilitakiwa kutuma pesa ya matumizi kwangu hakuwa shida maana naelewa mwanaume ndio mtunza familia kifedha.

Alifanikiwa kurudi kipindi cha mwanzo mwanzo tu tena akaniletea nyodo hatari stori zake sasa ooh mwaka huu nanunua gari sijui wewe umeshindwa hiki na kile nikitaka tunda anajivutaa nikajisemea hii ngoma ndio imeshavuja hapa. Kwakweli haikufika hata mwaka tukabwagana.

Hakuna kipindi nilikonda kama kipindi kile full mawazo alafu ndugu zake wananichora tu kenge wale!
ilibaki kidogo nidondoke nifeee!

Kuna mama mmoja mtu wa makamo akanifuata na kuniweka chini kisha akanipa ushauri mmoja wa nguvu sana akaniambia kijana wangu usiwe mnyonge hivyo tafuta mwanamke mdogo na mzuri kuliko mkeo then furahia maisha haya maisha ni mafupi sana na utamsahau.

Kwa kweli namshukuru sana yule mama maana from there maisha yalibadilika taratibu nilianza kumsahau yule mwanamke na mambo yake ingawa bado muda mwingine naumia ila ndio maisha isee
tuishi nao kwa akili!

Kwanini nimeleta huu uzi?
Nataka vijana wenzangu hasa hawa wadogo ambao wanajianda kuingia kwenye maisha ya familia wawe makini na kujitaidi wajipende na wao wasijitoe sana kwa ajili ya familia zao things change na maumivu utayopitia sio ya kawaida mm nilikuwa najiona mgumu nilikuwa nashangaa wanaume wanaolalamikia wake zao ila yalivyonikuta nilijishangaa najikaza ila uso na mwili vilijionyesha kuwa nipo kwenye maumivu jamani maumivu ya mahusiano hayaelezeki tena kwa sisi ambao tulishakuwa na familia utashangaa chakula hakipiti wala maji hayashuki.

Kuna bond inayojitengeneza ukishazoea kuwaona watu wako wa karibu kila siku kuitoa hiyo ni ngumu sana yaani kuna muda nilikuwa nikikaa hivi fikra za watoto wangu wapo mbali muda niliopoteza kuwa na mwanamke yule nilikuwa nafamilia ghafla naishi mwenyewe machozi yanatoka yenyewe tu.

Nashukuru sana gospel music inafariji sana.
 
Haya mambo haya yanapendeza kusimuliwa tu hivi kwa wenzako......usiombe yakukute......ni mazito...............

Mdogo wangu nakumbuka yalipomkuta alikuwa anashinda chooni kutwa kama mende......hata chakula hali anasema hakina ladha.......

Ila mapenzi hayana baunsa......ukiwa hujaingia kwenye kumi na nane unaweza ukaongea mengi sana ya kejeli na dharau........

Baba yangu mdogo alikuwa anaongea sana shombo.....siku aliyokimbiwa na mkewe ndio nikajua haya mambo hayana mwenyeji......

Alikuwa anashinda ukweni anaomba msamaha mpaka usiku analala kibarazani kama mlinzi........dah!!

Haya mambo haya.....huwa yanaanza kama utani vile.....
Yeah haya mambo it's unpredictable kabisa yaani unaweza kutomba nchi nzima na ukawa wala hauna wivu na wanawake ila sasa Ipo siku Moja Moyo wake utacreate bond na Mtu Fulani Halafu inakuja kutokea Huyo mtu anazingua au wewe unazingua Halafu anaondoka na kukuacha hapo sasa ndio utajua What's the meaningful to escaping from sobirbo 🤣🤣🤣
 
Mi zamani nilikuwa nikisikiaga zile story za mwanamke kuchinjwa, sijui kuchomwa visu 60 nk. Nilikuwa nawashangaa wanaofanya matukio ka hayo ila Sasa hivi nasema kama hayajakukuta kaa kimya,, mi na upole wangu huu ,nahisi nitakuja kutrend siku moja
🤣🤣🤣
 
Kuna bond inayojitengeneza ukishazoea kuwaona watu wako wa karibu kila siku kuitoa hiyo ni ngumu sana
mimi nishajiambia kabisa mke wangu atakua mama wa nyumbani yani nitamjengea awetegemezi kwangu kwa kila kitu siku zote ni wapo hai ila nitaandaa mazingira flani hivi ni kifa asiteseke sana maana ukimwezesha mwanamke yani jua ni umempoteza. Mbaya zaidi mimi hiyo bond na mke siitaki naishigi na mke wangu mpaka kuna kipindi ananiambia mbona unaishi na mimi kama unaishi na mtu back ila sijibu chochote zaidi ya kumuuliza kwani wewe hujiamini kuwa ni mke wangu alafu na kaa kimnya..

Hajawai kosa huduma yoyote ile ila nimemfanya amekua tegemezi mpaka anaogopa kunizingua maana anajua akizingua hata taulo ya kujisitiri anaweza akakosa japo siwezi mlipia ubaya kwa ubaya ( kiukweli na mpenda mke wangu ila siwezi muonyesha kamwe) . Kwanini na yafanya haya kwake niliwahi kuwa na wanawake kadha wa kadha na niliwawezesha na kuwaonyesha upendo wa kweli, nikachanganya hadi mahusiano na imani ila mwisho wake ulikua mchungu sana hakika hauelezeki na sitaki kukumbuka maana ilifika mahali nusu nijiangamize siyo kwa kuchwa masikini vile

Nb. Mke wangu anisamehe sana mimi ninaishi kwa kuharibu uchumi wake ili awe tegemezi kwa kila kitu kwangu kwenye maisha haya ila siku nikiwa sipo kuna vitu atakuja kushtuka nilimuwekezea kimnya kimnya maana watoto hawaaminiki wanaweza telekeza mama yao.
 
Naomba kutoa ushuhuda tofauti na huu. Siyo sahihi kusema wanawake wote ni vigeugeu.

Kuna kijana mmoja wakati yupo msingi, mwalimu alikuwa anamchapa mwanafunzi mwingine, kipande cha kiboko kikamchoma jicho moja.

Alipowekewa dawa ya macho AKAPOFUKA.

Wazazi wake walihangaika ajabu lakini mpaka kesho ni kipofu.

Kijana ni mwenyeji wa wa Lindi, ilibidi wampeleke Mvumi akasoma huko katika shule ya vipofu. Akasoma msingi na sekondari akafaulu kwenda kusoma Chuo Kikuu UDOM.

Akiwa mwanafunzi UDOM akapata rafiki wa kike ambaye baadaye akawa mchumba miaka mitano iliyopita.

Jumapili ijayo wataposana (engagement) kanisani kwao. Kanisa lipo karibu na Sinza Makaburini.

Binti hakubweteka bali alipambana na shule pia na kwa sasa ana Masters.

Wanadamu hatupo sawa kuna wengine wapo ni tofauti. Mifano ni mingi sana ya wenye upendo wa kweli. Wakati mwingine wanawake wanakuwa na upendo wa kweli ila sisi midume tukianza kuchepuka ovyo tunawakatisha tamaa. Kumbuka nao ni binadamu wana mioyo yenye nyama. Sikatai kuna wanawake nao ni vichomi bali na kuna wengine ni Gifts from God.

Tulale sasa
Hapo bado you need to give them time , Wewe unadhani wote walio fanyiwa drama na kugeukwa na wapenzi wao Hao wapenzi hapo Awali hawakuwa watu wazuri na wema kwao!?
 
Dadeki 🙌🙌🙌
Experience yangu hata umfanyie wema gani atakuacha tu..
Arusha 2014 jirani yangu alikuwa anafanya kazi taasisi fulani, financially alikuwa yuko poa sana. Kulikuwa kuna binti alikuwa anakuja kwake mostly on weekends... Siku ndo akani tambulisha hii ni pisi yake ila inasoma mkoa x chuo kikuu mwaka wa pili... Miaka ikaenda ile pisi ikawa haionekani kumbe ilikuwa chuo.
Mambo yakaenda vibaya kwa yule dada alifeli chuo so hakuweza kumaliza chuo. familia ikamtema mazima kwamba atajua na maisha yake. Familia ilienda mbali na kumuambia pesa walizo nazo niza kusomesha wadogo wa yule binti. So binti akamshirikisha boyfriend wake ambaye ni jirani yangu. Jamaa akamuambia aje tu maana hata kwenda nyumbani aliogopa.
Basi jamaa kwa kujua one day in this life atakuwa mke wake, akalibeba lile jambo na kuamua kumpeleka chuo kikuu kimoja kiko Arusha, alim somesha, chakula, mavazi yaani kwa kifupi alikuwa mzazi na boyfriend at once. akawa anaenda chuo for all the three years tumekaa nae pale, ila this time alitoboa graduation kila kitu fresh. Walikuwa poa sana kiukweli, ilikuwa ni couple moja strong sana ile unajua demu aki graduate wanafunga ndoa.
Demu aliendelea kukaa pale hadi akapata nafasi katika kampuni flani hivi alianza kwa kujitolea baadae akapata ajira ya kudumu, ila kupatikana hii kazi ni kwa juhudi za huyu mwamba. sijui salary yake but alikuwa ana safiri sana. Matatizo ndo yakaanza kule ndani. Demu alikuja kubadilika ndugu zangu siyo poa, kama mara tatu wameshikiana visu mule ndani, alikuja kumuacha mwamba kama hamjui and familia ikamuambia arudi nyumbani huyo jamaa siyo mume wake.
Jamaa alifanya attempt kama mbili za kutaka kujiua, alikuja kuwa mtu wa pombe sana, sigara nyingi sana (wakati hakuwa mnywaji kivile, wala mvutaji wa sigara) alikuja kukonda, kwenda job late, ananukia na pombe, kwa kifupi aliyumba sana ile kampuni ilijaribu kumbeba sana because bosi pia alijua what he was going through. Alivyoachishwa kazi akaja kuniaga akarudi kwao. That brother he was torn apart because of love. he couldn't take it anymore... Dada yake alikuja kunipigia March 2023 the brother died. Yule dada yupo tu huwa namuona mjini na life lake tu.
Kwa kifupi after that scenario nimeona unaweza ukaigiziwa maisha vizuri tu, riziki ikapatikana zaidi kwa mke au mpenzi wako hamuwezi toboa tena...! Dharau zitaanza tu kama hiyo pisi ilishamrudia jamaa na lovebite. . . !
 
Miaka 5 nyuma nilipatwa na hiki kisa, sijui huwa kuna nini kinatokea kwa wenzetu naweza kusema alikuwa mke kabisa maana kwao walinifahamu posa na mahari nilishamaliza na watoto wawili nimemzalisha sasa kipindi chote hicho alikuwa anafanya shughuli ndogondogo tu.

Sasa ikatokea fursa sehemu nikamwambia mama kwa haya maisha tunayoishi itachukua muda kutoboa hapa ebu kamatia iyo fursa ya kazi tusaidizane bwana bwana bwana kumbe ndio nilikuwa namaliza familia yangu wakuu kitendo cha yeye kupata ile kazi tu na vile nilimtumia mtu ninayemjua ilikuwa rahisi sana kwake kutoboa.

Picha linaanza kwanza amepangiwa mkoani akili ikacheza mmh nikiwa nipo kwenye dilema ya maamuzi kwao wakawa wapo karibu nae zaidi na wakamwambia aende huko kwa kuwa watoto bado wadogo waende kwa bibi yao yaani mama yake hadi mambo yatakapokuwa sawa kule then awachukue.

Basi mwezi ukaisha mwezi wa pili mara miezi sita nikaanza kuona mapicha picha kwanza sikuwahi kuona hela yake ingawa alikuwa analipwa mara 4 ya mshahara wangu bado nilitakiwa kutuma pesa ya matumizi kwangu hakuwa shida maana naelewa mwanaume ndio mtunza familia kifedha.

Alifanikiwa kurudi kipindi cha mwanzo mwanzo tu tena akaniletea nyodo hatari stori zake sasa ooh mwaka huu nanunua gari sijui wewe umeshindwa hiki na kile nikitaka tunda anajivutaa nikajisemea hii ngoma ndio imeshavuja hapa. Kwakweli haikufika hata mwaka tukabwagana.

Hakuna kipindi nilikonda kama kipindi kile full mawazo alafu ndugu zake wananichora tu kenge wale!
ilibaki kidogo nidondoke nifeee!

Kuna mama mmoja mtu wa makamo akanifuata na kuniweka chini kisha akanipa ushauri mmoja wa nguvu sana akaniambia kijana wangu usiwe mnyonge hivyo tafuta mwanamke mdogo na mzuri kuliko mkeo then furahia maisha haya maisha ni mafupi sana na utamsahau.

Kwa kweli namshukuru sana yule mama maana from there maisha yalibadilika taratibu nilianza kumsahau yule mwanamke na mambo yake ingawa bado muda mwingine naumia ila ndio maisha isee
tuishi nao kwa akili!

Kwanini nimeleta huu uzi?
Nataka vijana wenzangu hasa hawa wadogo ambao wanajianda kuingia kwenye maisha ya familia wawe makini na kujitaidi wajipende na wao wasijitoe sana kwa ajili ya familia zao things change na maumivu utayopitia sio ya kawaida mm nilikuwa najiona mgumu nilikuwa nashangaa wanaume wanaolalamikia wake zao ila yalivyonikuta nilijishangaa najikaza ila uso na mwili vilijionyesha kuwa nipo kwenye maumivu jamani maumivu ya mahusiano hayaelezeki tena kwa sisi ambao tulishakuwa na familia utashangaa chakula hakipiti wala maji hayashuki.

Kuna bond inayojitengeneza ukishazoea kuwaona watu wako wa karibu kila siku kuitoa hiyo ni ngumu sana yaani kuna muda nilikuwa nikikaa hivi fikra za watoto wangu wapo mbali muda niliopoteza kuwa na mwanamke yule nilikuwa nafamilia ghafla naishi mwenyewe machozi yanatoka yenyewe tu.

Nashukuru sana gospel music inafariji sana.
Mama watoto wako sasa hivi ana hali gani?
 
Back
Top Bottom