Leo nimemfungulia mdogo wangu wa darasa la tano akaunti ya JamiiForums

Leo nimemfungulia mdogo wangu wa darasa la tano akaunti ya JamiiForums

Nimeona bola ajiunge umu tu kuliko kujiunga fb naona mpaka akimaliza la saba atakuwa na uwezo mkubwa wa kujenga hoja.

Umefanya la maana sana Mkuu kwani Mimi binafsi tokea niwepo humu JamiiForums najiona tayari nimeshamaliza PhD zangu Oxford na Havard Universities. Kila siku niwapo humu Jamvini naona IQ yangu inazidi tu Kukua na nisikufiche huku mitaani naogopwa na ujengaji wa Hoja hadi nawaonea huruma wanaoniogopa. Huu mtandao umenijenga ' Kiakili ' hadi natamani sana ningekuwa ' Tajiri ' niweze kuwapa ' Nishani ' za Kutukuka ' Waanzilishi ' wa JamiiForums na pia niwape Vyeti vya Utambuaji wa Thamani ya Members wote wa JamiiForums sema tu ' umasikini ' umenitukuka hadi katika Kope zangu za macho. Ukitaka uninyime raha au tugombane nikataze nisiwepo humu nikitiririka na kuserereka.

Mwenyezi Mungu awape maisha mema, marefu na yenye baraka tele Waanzilishi wa JamiiForums, Watendaji wake wote, Moderators na Members wote na pia awape makazi mema wale wote waliotutangulia mbele ya haki na ambao walikuwa ni Wenzetu humu.
 
Mmh akiona mipicha ya misambwanda na vibamia je?
 
Hapa atapata mengi sana mazuri kuliko mabaya kwakuwa wachangiaji wa humu na watoa mada wengi wanaongea lugha ya kiswahili kuliko Tweter .aisee Kule hapafai English inapigwa huko utafikiri siyo Tz. Huku utamkuta Maria Sarungi,pale yupo Zitto kabwe,hapa utamkuta Mo Dewj, pale utamkuta January makamba, yaani hizo namba hatari sana hakuna kiswahili kule Mimi huwa nafunguaga halafu nabaki najishangaa tu
 
Back
Top Bottom