Leo nimeshiriki tambiko, kumbe wazungu walitudanganya, hamna uchawi wowote kwenye tambiko

Leo nimeshiriki tambiko, kumbe wazungu walitudanganya, hamna uchawi wowote kwenye tambiko

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Wazungu ni watu wabaya sana, kumbe tambiko ni ibada kama nyingine na mnyama anayechinjwa anatolewa sadaka na analiwa na wote.

Tambiko lilianza kwa kumuweka ng'ombe kwenye matawi ya mti wa Ululambuli, kisha akachinjwa. Alipochinjwa akachunwa ngozi, akatolewa nyama za kifuani, zikatengenezwa mishikaki, sehemu nyingine zikakatwa katwa.

Nyama ikachomwa kuelekea jua linapotoka, maombi yakafanyika, hatukutaja mashetani, wala hatupandisha majini. Tulimwita Mungu ambaye humwita Sebah.

Baada ya kusali na kila mtu kutaja hitaji la moyo wake, ibada ikaisha, tukaanza kuzila zile nyama za kuchomwa kwa furaha.

Kwa kweli nilifurahi sana kufanya ibada ya kikwetu haswa, sio longolongo za kina Carl Peters na walaghai wengine

Lyubha, Wangaluke, Welelo, Mungu, Sebah.
 
Kwenye mahitaji yako ulikumbuka suala la kuongeza mke?
 
Kwa nini mlikosea mkaila hiyo minofu? Hamjui inapaswa kuliwa na mtambikiwa? In short, Tanzania ina safari ndefu sana, kwa sababu imepiga V-turn kuelekea ilikotoka.

#^Car-taaWar-who-knee!^
 
Wazungu ni watu wabaya sana, kumbe tambiko ni ibada kama nyingine na mnyama anayechinjwa anatolewa sadaka na analiwa na wote.

Tambiko lilianza kwa kumuweka ng'ombe kwenye matawi ya mti wa Ululambuli, kisha akachinjwa. Alipochinjwa akachunwa ngozi, akatolewa nyama za kifuani, zikatengenezwa mishikaki, sehemu nyingine zikakatwa katwa.

Nyama ikachomwa kuelekea jua linapotoka, maombi yakafanyika, hatukutaja mashetani, wala hatupandisha majini. Tulimwita Mungu ambaye humwita Sebah.

Baada ya kusali na kila mtu kutaja hitaji la moyo wake, ibada ikaisha, tukaanza kuzila zile nyama za kuchomwa kwa furaha.

Kwa kweli nilifurahi sana kufanya ibada ya kikwetu haswa, sio longolongo za kina Carl Peters na walaghai wengine


Lyubha, Wangaluke, Welelo, Mungu, Sebah.
Tukaanza kuomba kila mtu ..
Wewe uliomba kitu gani bwashee
 
Walituletea dini Ili tustaarabike. Mtu aliyeelimika na anaeijua vizuri dini yake uishi vyema na Jamii yake.
 
Naona lile jiwe walilikataa waashi limekuwa jiwe kuu la bujiji kujitwangia photo.

Sasa mkuu baada ya tambiko hamkushushia K VANT?
 
Back
Top Bottom