Kwa kuziacha takwimu ziongee, Mayanga ni bora. Ni ngumu kusema ni bora kuliko Mkwasa na Kibadeni lakini mafanikio yake yanasimama juu ya Mkwasa kwa kulinganisha kwa siku za karibu maana ndiye aliyemreplace.
Kucheza mechi 8 na kupoteza 1 ni rekodi ambayo haijafikiwa kwa muda mrefu. Najua tatizo kubwa Mayanga hajawahi kuwa kocha wa Simba au Yanga, na tatizo kubwa zaidi ni kwa sababu hachukui wachezaji kwa majina ila kachagua vijana wapya ili kujenga timu ya baadae, hapa ndio ulipo mzizi wa chuki dhidi yake.
Hata hivyo ni kweli kuwa jamaa hana exposure kubwa kama hao uliowataja, na tatizo la Tanzania sio kocha ila uzalishaji wa wachezaji wa kiwango cha kimataifa. Hapa ndio tatizo kubwa lilipo