Lesotho wakishinda Taifa Stars itasonga mbele?

Lakini mbona Pointi zao na zetu ziko sawa!
Sheria inayotumika sio ya tofauti ya magoli linapokuja suala la kuamua nyie wawili mliofungana point. Wanaangalia mlivyokutana ktk kundi lenu matokeo yaliendaje. Ingekuwa walidroo zote mbili, wangeangalia nani alifunga magoli mengi kwao. Kama wangefungana hapo wanheluja kuangalia vitu vingine.
Sasa kwa stars, hawa jamaa tulidroo nao hapa tz na kwao walitufunga.
 
Haya mambo ya zima Moto ni mzoea ya CCM wakiongozwa na Bashite

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa nimeelewa.
Uzuri kidogo ni hata cape verde anaweza pita kama atashinda na sisi kukosa point tatu. Hivyo cape verde watapambana wakiwa kwao na kumuomba uganda msaada. Hivyo tuna chansi bado maana leaotho licha ya kudroo nasi ila ndio UNDERDOGS wa kundi.
 
Tatizo ni goal difference hapo ndo itaifanya taifa start iyaage mashindano
Ukiachana na goal difference pia head to head Lesotho vs Tanzania, Lesotho wametufunga so ni ombi tu kwa kamati hiyo ya hamasa pia wawaambie watu kwamba zamu yetu na Dua lisomwe Cape Verde ashinde laasivyo itakuwa zamu yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
BC viongoz wetu wanashida sana ,mipango zero kabsa
 
BC viongoz wetu wanashida sana ,mipango zero kabsa
Hamasa nzuri ni kusema kwamba sisi tufunge halafu tuone Lesotho nao kama watafungwa. Maana yake Mbumbumbu kama mimi kesho tukishinda na Lesotho wakishinda na sisi ikaonekana hatusongi mbele, kuna watu wataona kwamba wamedanganywa!!
 
Kwa maelezo ya barafuyamoto kuna jambo tunafichwa. Nadhani wanataka isemwe kuwa "tumepambana kiume" hata kama tumetolewa. Walikuwa wapi wakati ule hadi leo wawafanye watu waamini kama mechi yetu na Uganda ndiyo itakayoamua hatima yetu?
Kungekuwa na nia na hamasa toka mwanzo jumapili yungekuwa tunakamilisha ratiba. Tungekuwa tymemaliza shughuli kitambo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…