Lesson learned from Nyamayao and Nyumba Kubwa..........What are your Two cents on this ....!

sasa kama mnabakana kuna mapenzi kweli hapo? naye mwanaume anajiskiaje kuwa na mahusiano ya hivyo na mkewe? kweli unapita proudly unasema 'there goes my wife?'. afadhali kuta zinaficha mambo,manake kuna watu wanapaswa wajidharau! bibi anakua kama katiwa super glue, cha kufia! hizo za kuwekewa chakula, sijui maji ya kuoga sio neno. ila hapo ndo kuna mtafaruku! well, tunarudi palepale, unachoruhusu ndicho utafanyiwa. nawaheshimu wamama wote wenye courage ya kuchukua maamuzi yao wenyewe!

 
Kumbe sipo pekeyangu.Mimi kuna siku aliniambia nikimfuatilia ni kama namwambia ongeza.Nilichaacha.siku hizi nikienda kuoga nikirudi namkuta yupo busy kuangalia simu yangu.akiniona anajidai kuirudisha.HAWA viumbe kumbe wapo sawa
 

Nakwambia king'asti afadhali tuyasikie tu nje lakini kuna yanaowakuta hata ukimwona muhusika unashangaa!! Wanawake wengi hawana say mpenzi ingawa kwa kiasi flani hawa wa kizazi cha sasa kidogo wako vizuri na ndio maana ndoa nyingi zinavunjika siku hizi kwa sababu hawako tayari kunyanyaswa kama wale wa zamani.

Kwa wenye wenzi waelewa jamani tukumbuke kumshukuru MUNGU kila kukicha kwa kutupatia watu wa aina hiyo maishani mwetu kwa sababu wapo wengine walionao hawafikii hata robo ya uliye naye. Appreciate penzi, msaada, ushirikiano na uelewa wake and let him/her ajue unaappreciate na kumpenda.
 
Wamama zetu walikuwa wavumilivu sana ndio maana waliweza kuishi bila kokoro na waume zao, kulikuwa hakuna majibizano enzi hizo kati ya mume na mke, embu angalia sasa wanawake wanataka kuchukua role ya wanaume unadhani kuna kitu kitaeleweka hapo? tusilalamike sana tunanyanyaswa, tuangalie na sie tumeplay role yetu kama wanawake wa kiafrika?
 
Kumbe sipo pekeyangu.Mimi kuna siku aliniambia nikimfuatilia ni kama namwambia ongeza.Nilichaacha.siku hizi nikienda kuoga nikirudi namkuta yupo busy kuangalia simu yangu.akiniona anajidai kuirudisha.HAWA viumbe kumbe wapo sawa

Aiseee.....napata picha kumbe baadhi ya wanawake wanaishi kwenye ndoa zao kwa uoga, lets say sijui ni ule msemo kwamba 'kubali yaishe' au unyenyekevu unazidi sana kiwango, hata sielewi! Yaani mtu anakuchimba kabisa mkwala eti ukimfuatilia ataongeza duh! Alafu nawe unaamua kuufyata mkia kwa maana kwamba umemruhusu abaki na alio nao ila tu asije akaongeza idadi! Mmmmh........ungekuwa ni mtihani kwakweli mi hapa ningeambulia zero kabisa!
 
King'asti hata mimi nashindwa kabisa kuelewa. Mtu anirudie nyumbani alfajiri, kuna ndoa hapo? Nadhani ni sulal la malezi na mila. Kuna watu wamekuwa prepared kukubali manyanyaso. NOT ME.
Kwani niki file divorce xxx itachacha???? Ni nini kinachokung'ang'aniza kwa mwanaume anayekujia alfajiri? Ndio pale hata ukiumwa kikoozi unajua tayari. Maisha ya wasiwasi na mashaka siwezi yavumilia. Narudia, sometimes tunawalea hawa wanaume wawe hivyo walivyo. Wanaume ni kama watoto. Anaanzaje kuja asubuhi??? Am sure alianza taratibu kuchelewa wife akawa anamkenulia.

My dad sent me to school ili niwe independent including kutokukubali mtu yeyote afanye maisha yangu a living hell. Na alikuwa akitukumbusha mara kwa mara kabla hatujaolewa kuwa tusikubali kunyanyaswa na mwanaume; and the only thing to escape that is to be financially independent.

 

...aahhh, mapenzi ni kizungumkuti nyie, ...kwenye mapenzi kuna ujinga na upofu, kuna kipindi una justify hata yale kwa walio nje ya boksi mnaweza yaona ni 'limbwata' nini?...

haijalishi ni kwa mwanamke au mwanaume...na hapa namtetea sana tu mwanajamiione msimamo wake huo wa uvumilivu...hata kwa wanaume, binafsi nime experience hizo za mke kurudi nyumbani baada ya siku mbili, tatu, nne ...japo tulikuwa tunaishi mji mmoja!

...mpaka pale utapojikubalisha kukaa nje ya boksi ndipo utapogundua tulivumilia ili kumaliza sababu zote za huyo mwenza kusema hakupewa nafasi ya kujisahihisha.
 

Dah! dada ubarikiwe sana kwa hii painful truth ulioiweka. Nakubaliana na wewe hili uliloelezea ndio chimbuko la matatizo mengi.
 
...na hapa namtetea sana tu mwanajamiione msimamo wake ...
wewe tena usimtetee mwanajamiione ? mbona siku hiyo utatuacha midomo wazi ? hahahaha!
Nikirudi kwenye topic kuna kuvumiliana kwa vitu vidogo lakini haikubaliki kufumbia macho uozo au manyanyaso.
 

Nashukuru umeliongea wewe ulieko kwenye ndoa maana wengine tungeaitwa wabeijing na kuambiwa tusubiri yatukute! Kwakweli mi bado sijapata sababu za msingi za mtu kuendelea kuendekeza hayo kwa kisingizio cha ndoa ilihali ye mwenyewe ndo anaumia!!
 
wewe tena usimtetee mwanajamiione ? mbona siku hiyo utatuacha midomo wazi ? hahahaha!
Nikirudi kwenye topic kuna kuvumiliana kwa vitu vidogo lakini haikubaliki kufumbia macho uozo au manyanyaso.

hahahaha,...dahhh...kumbe nishazoeleka ee?
aaah, anaonewa kiasi cha kutosha bana...mimi naamini hajaeleweka tu mwj1 maskini,
she's an angel kwa nafasi yake.
 

SaraM umesema kweli wapo wanawake ambao ni vyanzo vya kunyanyaswa tena basi cha ajabu wanawake wa aina hii hubarikiwa kupata wenza wema kweli mpaka wa nje wanamtamani ile ya .....Dah mume yule masikini, ningempata mie!! Lakini pia mpenz tukumbuke kuwa hata wanaume wengi wa siku hizi si kama baba zetu au wazee wentu. Hata hizo role unazozisema kuna wengine hata hawazitambui roles zao both kama mume na pia kama baba/kichwa cha familia! Hebu nambie mwanaume ambaye anaondoka nyumbani hajui wanae wanakula nini/ hatoi ada wala hajali matibabu huyo kweli utasema anazijua roles zake kama mzazi? na si kwamba hana kipato. Mwanaume ambaye hana muda na familia yake, akitoka watoto wamelala, akirudi wamelala na weekend ndo siku za kukaa na marafiki zake viti virefu?
 

Kipipi aksante na hiyo niliyoikuza hapo kwenye post yako ndio hasa kiini cha thread hii. Nakumbuka kuna post nyumba kubwa aliibandika kuhusu hili (nadhani kwenye thread ya sms kwenye simu ya Mr). Ndio nikasema tulijadili hili kwa upana. Na wengi wetu tumekuwa tukiishi kiuwoga si kwa kuwa tumezaliwa waoga bali pengine ni kutokujua positions zetu kama mke. Nini maana ya kuwa mke wa mtu, je kumpikia, kumtunzia familia, kumchekea tu au pia kuhoji pale panapostahili au kumwongoza mume. ??
 

Hapa mwisho umehit the point... Ina maana msimo wako katika post hii (ambao hata mi naona ni rahisi kutekeleza), ni sawa na ungenza kwa kusema ....if you are financially independent.... then uendelee na hayo uliyoandika.

Hebu naomba msimamo wako kwa wale ambao sio financially independent... Kumbuka kuna dada zetu wengi sana wanateseka kwa sababu hawako financially independent.Wapo wanaolazimika kuwa nyumba ndogo kwa kuwa hawako financially independent... unawashaurije?
 
hahahaha,...dahhh...kumbe nishazoeleka ee?aaah, anaonewa kiasi cha kutosha bana...mimi naamini hajaeleweka tu mwj1 maskini,she's an angel kwa nafasi yake.
unajua mkuu Mbu limbwata lingine unabugia mwenyewe wala haina haja ya kulaumu kinadada lol!
 
Reactions: Mbu
Dah! dada ubarikiwe sana kwa hii painful truth ulioiweka. Nakubaliana na wewe hili uliloelezea ndio chimbuko la matatizo mengi.

Hivi kutokuvumilia manyanyaso kama vile kupigwa nako nikuingilia majukumu ya mume? Kutaka kufahamu ukweli pale kunapokuwa na hitilafu mfano mume anapochelewa/kurudi alfajiri/harudi kabisa nyumbani, hilo nalo ni kosa? Wamama wengi wa zamani walikuwa ni waoga na sio kwamba wote walikuwa wanayafurahia haya!! Tusidanganyane jamani, kuishi kwa ajili ya kumridhisha mtu au jamii ni kujiumiza nafsi tu tena kwa ulimwengu huu uliojaa shida na magonjwa yasiyotibika! La sivyo kina Angela watazidi kuongezeka na mahakama zisitoshe!
 
...aahhh, mapenzi ni kizungumkuti nyie, ...kwenye mapenzi kuna ujinga na upofu, kuna kipindi una justify hata yale kwa walio nje ya boksi mnaweza yaona ni 'limbwata' nini?...


Aksante kwa kutukumbusha hili Soulmate........mpaka ujitambue na ku'step out' of that relationship ndo unaanza kujiona hivi nlikuwa mjinga kiasi kile? why did I let him/her do that to me n.k. Na wakati huo kumbuka kina nyumbakubwa walikuwa wanakesha na kukubigia gitaa wala huwasikii. Mimi binafsi kuna siku nyamayao aliniambia anatamani kushika fimbo aniibukie kwenye screen na kunitandika..... kuwa I was awake yet so sleepy, I had eyes yet so very blind.



Hahahaah we Soulmate, acha upendeleo bana ahaha eti unanitetea sana (ntadai kutetewa hata zikianza zile za .... ah bwana mi nimechoka leo...........hahahah).
Back to the Post: Mbu ni kweli kuwa wapo wanaume ambao wametendwa na wanawake to the extent kwamba anaapa kwa miungu yake yote hatokaa apende mwanamke tena. Ukimkuta mwanaume wa aina hii, ukafanikiwa kumbadilisha huo mtazamo, ninahisi anawezakukupenda hadi ukashangaa lol.

...mpaka pale utapojikubalisha kukaa nje ya boksi ndipo utapogundua tulivumilia ili kumaliza sababu zote za huyo mwenza kusema hakupewa nafasi ya kujisahihisha.
Hiyo sababu Mbu mara nyingi huwa inatuponza wengi lakini hakuna kitu kizuri kama kukamua jipu na kuhakikisha umetoa na kile kiini kabisa.
 
Dah! dada ubarikiwe sana kwa hii painful truth ulioiweka. Nakubaliana na wewe hili uliloelezea ndio chimbuko la matatizo mengi.
Ahsante klorokwini, unajua tumekuwa vipofu na hizi elimu zetu tunazopata wanawake siku hizi, tunasahau mambo hayo hayaingiliani kabisa na maisha ya ndoa, hasa kwetu huku afrika, tuna aply mambo ya kiwestern ambayo yanawasuit wenyewe huko kwao,basi na matokeo yake tuvumilie matokeo yake tu,nahisi ukimpa heshima yake na kumpa nafasi ya kuwa mwanaume kenye family mambo mengine yatajiseti tu, mie pia naamini katika uvumilivu
 

Hawana kwao? Warudi kijijini kwao huko wakalime au hata wakawe mama ntilie shwari tu! Sio eti wamezoea kupikia majiko ya umeme na kuendesha magari basi ndo maisha mengine wasiyaweze! Kwani mtu anaeuza vitumbua au maji ya sh.100 pale k/koo ni mjinga?
 
ni kweli kabisa wapo wanaume ambao hawabebeki kabisa,na kila ufanyalo haiwezekani kwake, hapo huna bidi kujidhatiti na kuchukua hatua either kutafuta washauri wenu waongee nae, na ww pia kumwelewesha umuhimu wa michango yake ktika family,kuna y a kuvumilia, kama vile amechelew kurudi hivi, sio ndio unaongea mpaka mishipa ya shingo inakutoka,kuna njia za kumfanya mumeo awe anatamani kurudi home mapema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…