Let's talk about savings: Ikitokea umeachishwa/umeacha kazi leo, una akiba ya kukutosha kwa siku ngapi?

Let's talk about savings: Ikitokea umeachishwa/umeacha kazi leo, una akiba ya kukutosha kwa siku ngapi?

Kinachowaponza Hamna Vyanzo Vingine Vya Mapato Mnategemea Mshahara,mnabaki Kulalamika Na Kuchukia Kazi,hapo Nlikuwa Nafanya Ofisi Naenda Mpaka Jumapili Mtu Binafsi Napigishwa Mzigo Hatari,ila Najijua Napenda Maisha Mazuri Mbaya Zaidi Mimi Ni Bad Spender
 
Kulingana na usawa huu ulivyo, na jinsi kipato kilivyo kigumu upatikanaje wake na hata kinapopatinakana hakikidhi mahitaji na hapo hapo unahitajika uweke akiba i wonder how is it possible kwa uchumi huu nilionao!.

My personal story.
Ni kijana nmeajiriwa mahali mshahara wangu ni Tsh 250,000 per month najitegema lakini bado sijaoa! Kwa muda sasa nmekua nikipambana kufanya savings kwa sabab najua umuhimu wake hasa kwa wakati wa shida na pia hata kama si wakati wa shida unaweza jiwekea akiba ili uweze kufikia malengo flani ya kiuchumi like kupata mtaji wa kuanzisha biashara e.t.c! Lakini mambo yamekua si rahisi hivyo mshahara haunitoshi kulingana na mahitaji niliyonayo na pamoja na kujitahidi kujibana na kwa maana hiyo haufiki hata mwisho wa mwezi hua nakaaga natafakari hivi kwa mtindo huu mshahara kutotosha ikitokea nimeachishwa kazi sasa hivi ka akiba kangu kadogo ninakojiwekea kanauwezo wa kunitosha hata kwa wiki mbili zaidi kweli??
Nmeuleta uzi huu wa changamoto zangu binafsi kufahamu wenzangu linapofika suala la saving mnakabialiana nalo vipi na je, una kiwango cha kutosha cha saving ikitokea chanzo chako cha mapato mirija imekatwa? Mwenzangu unatumia njia zipi unazoziamini katika kufanya saving? Let me hear from you, let's talk about savings!
Tengeneza banda la chips au kitimoto kwaajili ya fedha ya ziada....
 
Mimi Siku Zote Na Principal Kutokugusa Mshahara,mishahara Ikutane Bank,nahamisha Napeleka Bank B Au Kwenye Mzunguko
Haya Yote Nayaweza Kupitia Kitu Kimoja Biashara Ndogo Tu,nkienda Kazini Natengeneza Juice Kuwauzia,chapati Au Maandazi,(hawanielewagi Sistaduu Wa Haja Nabeba Juice Nahangaika Na Ngano)napata Pesa Ya Kula,kutengeneza Nywele,n.K Mara Nyingi Mshahara Natumia Kulipa Kodi Kufanya Maendeleo,nikaumwa Mwaka Na Kukaa Nyumbani Miaka 2,mpaka Naumwa Nilikuwa Napesa Ya Kujikimu Mwaka Na Nusu,he He He Sasa Naelekea Kupona Kabisa Na Kurudi Kazini,sina Sh Moja Hapa Ila Nina Plan Za Biashara 3 Ndogo Ndogo,moja Kwa Ajili Ya Kupata Mahitaji Ya Nyumbani,nyingine Mahitaji Ya Mwanangu Na Jamaa Jamaa,matanuzi Nyingine Kufanya Saving,mishahara Lazima Ikutane Bank, Na Ofisini Lazima Mnipe Tuhuma Mimi Mwizi

Naruhusiwa kuja PM?
 
Mimi Siku Zote Na Principal Kutokugusa Mshahara,mishahara Ikutane Bank,nahamisha Napeleka Bank B Au Kwenye Mzunguko
Haya Yote Nayaweza Kupitia Kitu Kimoja Biashara Ndogo Tu,nkienda Kazini Natengeneza Juice Kuwauzia,chapati Au Maandazi,(hawanielewagi Sistaduu Wa Haja Nabeba Juice Nahangaika Na Ngano)napata Pesa Ya Kula,kutengeneza Nywele,n.K Mara Nyingi Mshahara Natumia Kulipa Kodi Kufanya Maendeleo,nikaumwa Mwaka Na Kukaa Nyumbani Miaka 2,mpaka Naumwa Nilikuwa Napesa Ya Kujikimu Mwaka Na Nusu,he He He Sasa Naelekea Kupona Kabisa Na Kurudi Kazini,sina Sh Moja Hapa Ila Nina Plan Za Biashara 3 Ndogo Ndogo,moja Kwa Ajili Ya Kupata Mahitaji Ya Nyumbani,nyingine Mahitaji Ya Mwanangu Na Jamaa Jamaa,matanuzi Nyingine Kufanya Saving,mishahara Lazima Ikutane Bank, Na Ofisini Lazima Mnipe Tuhuma Mimi Mwizi
Nmeipenda hii, hili la mishahara kukutana kwa wengine sisi tunaona kama ni miujiza pana dondoo kadhaa hapo nimezipata hasa za biashara ndogo thanks, be blessed!
 
Kinachowaponza Hamna Vyanzo Vingine Vya Mapato Mnategemea Mshahara,mnabaki Kulalamika Na Kuchukia Kazi,hapo Nlikuwa Nafanya Ofisi Naenda Mpaka Jumapili Mtu Binafsi Napigishwa Mzigo Hatari,ila Najijua Napenda Maisha Mazuri Mbaya Zaidi Mimi Ni Bad Spender
Sasa ulijikwamuaje mkuu kutoka kwenye huu mtego ambao sisi ndugu zako tumenasa?
 
Tengeneza banda la chips au kitimoto kwaajili ya fedha ya ziada....
Thanks kwa ushauri mkuu, ngoja niendelee kudunduliza hivi hivi kwa ugumu ugumu ikiwezekana hata kukopa kuhakikisha napata chanzo cha mapato mbali na mishahara ili kinisaidie kukudhi mahitaji mengine ili hata ka hela ka kuweka akiba kapatikane mana kuna leo na kesho...
 
Umeuliza kitu sensitive sana ndio maana wadau wanapita kama hawaoni hivi.
Kabla hujawalaumu wanaopita kmy kmy mchango wako mkuu ni upi?

Kwa upande wangu pesa ya akiba huwa naiweka kwenye mchezo ambao siyo rahisi kuichomoa hata ukwame vipi
 
Saving nzuri ni Investment, najua hujanielewa, Yaani badala ya kuhifadhi cash wewe nunua vitu, Ardhi, Mashine, mitambo na vitu kama hivyo. Kwa kulipa kidogo kidogo unaweza kununua Mashine Za Kusaga na kukoboa, Mashine Za saluni, Mashine Za kumwagilia, kujenga mabanda ya mifugo na kuyakodisha, kununua Ardhi halafu siku huna kazi utaona vitakavyokua na msaada.

Cash ni ngumu Sana kuiweka
 
Biashara ndogondogo watu wanazidharau ila zinatoa balaa,kuna kipindi nlimpa wife tsh 20000 awe ana wachemshia chai na viazi vya kuchemsha mafundi waliokuwa wanajenga ghorofa za ofisi nnayofanyia kazi ila baada ya wiki mbili alinipa laki 3. Japo alikuwa amewekeza nguvu nyingi kwenye biashara yetu yenye mtaji mara 300 ya hiyo ila haikuleta faida kiwepesi namna hiyo,na tofauti yake ya kuuza chai inatumia masaa mawili yaan saa 2 hadi saa 4 wakati hiyo nyingine ilikuwa inachukua muda mrefu zaid ya masaa kumi
 
Hapo kabisa ni lazima ujue kwa mwezi unatumia shilingi ngapi,
Kuanzia nauli,
Chakula,
Bills,

Piga hesabu zote kwa mwezi, angalia kwenye mshahara wako utabakiwa na bei gani baada ya kutoa vyote hivyo, kinachobaki save.

yeah, i know i know its hard but my dear usipokua mbahili malengo huwezi kufikia na good thing bado hujawa na familia.

Make sure unanunua chakula unaweka ndani, anza kupika mwenyewe kama ulikua unakula chakula kwenyw migahawa, kila pesa unayotumia ipigie mahesabu kwa mwezi, hata hizi vocha ukiwa bingwa wa kukwangua tu mwisho wa mwezi utajikuta umetumia vocha ya laki moja jiulize kwenye mshahara umebakiwa na kiasi gani.

Jua kua kila pesa unayo spend ni ya kwako wewe na inapunguza kwenye mshahara.

Rafiki aliwahi kupata kazi akanitajia mshahara wake, nikampigia hesabu mwisho wa siku akabaki na elfu6 yaan kwa mwezi anapokea elfu 6 baada ya kutoa vitu vyote nilivyoorodhesha hapo juu.

Ndio unashangaa unafanya kazi miaka mingi lakini maisha hayabadiliki kumbe maskini kinachobaki ni sh elfu 2.
Lol.

NB: Fanya yote lakini lazima uwekeze ili kukuza kipato chako la sivyo kila siku utalia maisha magumu.
 
Saving ni nzuri sana km hiyo pesa itawekwa ktk investment..
 
Focus on earning more na sio on saving. Badala ya kusave hela ikae bank tu (au kwenye kibubu kama jiwe), tafuta namna ya kuiinvest na kuizungusha.

Kila mtu anaweza kuanza kufanya some savings no matter unaingiza shillingi ngapi. Wataalam wanasema unaweza kuanza na 10% (au chini ya hapo kwa kuanzia) ya kipato chako and then ukajifunza kuishi kwa 90% iliyobaki. Kuna vitu vingi "vya kipuuzi" tunavyofanya na vinatumalizia pesa. Ukikaa chini na karatasi ukaanza kuanalyse pesa yako unaitumiaga wapi na wapi, utapata jibu
 
Why mnapenda kwenda PM wakati hapa jukwaani ni kuelimishana tu? Toa ulichonacho na wenzio wafaidike au kama una swali uliza hapa upate majibu zaidi toka kwa wadau tofauti

Sasa mkubwa kama nimemuelewa amu niweke hapahapa hadharani? Unanitaka nini mkuu?

Nimeshaweka mchango wangu kwamba kila nnachokipata, naweka 10% kwanza ndio mambo mengine yanaendelea.
 
Hicho unachokiwaza (kibarua kuota nyasi) usiombe kikukute! Cha moto utakiona.
Duuu mwenzio anazungumzia savings not necessarily kufutwa kazi manake anaweza kupata kazi yenye kipato kikubwa zaidi ya hapo ungejikita hapo kwenye saving ingekuwa vema!
 
Back
Top Bottom